Skip to main content

WADAU HAKI ZA WANAWAKE PEMBA: WATAJA YANAYOWAKOSESHA HAMU KUDAI HAKI ZAO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

IMETAJWA kuwa, wanawake wanapohaingaikia hudumza za kijamii kama vile maji safi na salama, huduma za afya ya uzazi, elimu ya lazima hupoteza mwelekeo wa kudai haki zao za kisiasa, demokrasia na uongozi.

Hivyo, mamlaka husika zimeombwa kuimarisha huduma hizo kwa haraka, katika vijiji mbali mbali kisiwani Pemba, ili kuhakikisha kundi la wanawake, linafikiwa na huduma hizo kwa ukaribu.

Ushauri huo umetolewa leo April 27, 2023 na wadau wa haki za wanawake, kwenye mkutano wa siku moja, wa kusikiliza changamoto na ufumbuzi wake, zinazowakabili wanawake kutodai haki zao, zilizoibuliwa na wahamasishaji jamii, waliomo kwenye Mradi wa kuwahamasisha wanawake kudai haki zao, unaoendeshwa na TAMWA, PEGAO na ZAFELA na kufanyika Chake chake.

Walisema, wanawake wanayo haki ya kuwa viongozi katika maeneo kama ya jimbo, kwenye jamii, serikali na hata kwenye asasi za kiraia, lakini kutokana na kukabiliwa na changamoto za utafutaji wa huduma za kijamii, hukosa kutilia maani jambo hilo.

Mmoja kati ya wadau hao, Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said Kisenge, alisema wanawake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za ukosefu wa karibu wa huduma zao muhimu.

‘’Ijapokuwa, kwa mfano kupitia TASAF serikali imeanzisha mpango wa kuziwezesha familia maskini, ili wanawake wafikirie namna ya kudai haki zao, lakini bado wapo wanaokabiliwa na changamoto,’’anasema.

Nae Afisa Mipango wilaya ya Chake chake Kassim Ali Omar, alisema ikiwa huduma ya maji safi na salama, huduma za afya ya mama na mtoto zitapatikana kwa urahisi, wanawake wanaweza kuongezeka, katika kudai haki zao za uongozi.

Nae Mjumbe kutoka chama cha siasa cha ACT-Wazalendo Saleh Nassor Juma, alisema wanawake wanayohaki ya kuongoza, iwe kwenye siasa, serikalini au katika asasi za kiraia.




Akifungua mkutano huo, Mratibu wa TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema huo ni mfululizo wa kukutana na wadau, ili kuibua changamoto zinazowakabili wanawake katodai haki zao.

‘’Wanawake wanayohaki ya kudai haki zao katika demokrasia, siasa na uongozi, na ndio maana zaidi ya mikutano 70 kwenye shehia mbali mbali kisiwani Pemba, tumeshaifanya ya kuihamasisha jamii, juu ya jambo hilo,’’alieleza.




Nae Mkurugenzi wa PEGAO Hafidh Abdi Said, alisema suala la utetezi wa haki za wanawake, sio jukumu la asasi za kiraia pekee, bali kila mmoja kwa nafasi yake.

Alisema, wizara ya elimu ikiweka mazingira ya upatikanaji elimu bora na wizara ya afya ikiimarisha huduma za afya, hapo mwanamke atakuwa na hamu ya kufikiria suala la uongozi.



Nae Mratibu wa mradi wa kuihamasisha jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia ‘SWIL’ kutoka PEGAO Dina Juma alisema, kila mmoja akitimiza wajibu wake, wanawake wanaweza kuongezeka katika nafasi mbali mbali za uongozi.

‘’Kinachoonekana, bado baadhi ya makundi ya watu hawajawaamini wanawake kuwa wanaweza kushika uongozi na kuongoza, sasa dhana hii ikiondoka wengine zaidi wataonekana,’’anafafanua.



Akiwasilisha changamoto na mafanikio, muhamasishaji jamii kutoka wilaya ya Chake chake Hassain Omar Salim alisema, baada ya kukutana na wanawake kadhaa kisiwani Pemba, wapo walioweka nia ya kuingia majimboni, katika uchaguzi mkuu ujao.

‘’Kwa mfano wilaya ya Micheweni pekee tumepata wanawake 35, lakini karibu kila wilaya wapo wanawake wasiopungua 25 walioweka nia, hii ni ishara nzuri na mafanikio ya ziara zetu,’’alifafanua.

Kwa upande mwengine, muhamasishaji jamii huyo, alisema baada ya kuibua changamoto kwa jamii, zipo zilizofanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba, vituo vya afya, ujenzi wa daraja na kurejeshwa skuli kwa wanafunzi watoro.

 Tayari wahamasishaji jamii kisiwani Pemba ambao wanatekeleza mradi wa ‘SWIL’ unaoendeshwa na PEGAO, ZAFELA na TAMWA-Zanzibar wameshazifikia shehia zaidi 70, kwa wastani wa wananchi 3,000 kuwapa elimu ya umuhimu wa wanawake kuwa viongozi.

                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch