Skip to main content

KHADIJA ALI WA CHIMBA: MNUFAIKA WA TASAF ALIYEJIKUSANYIA SHUNGU YA MIRADI, MBIONI KUJENGA NYUMBA YA KUDUMU

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KHADIJA Ali Mohamed 45, wa Chimba Micheweni Pemba, sasa ana mtaji wa zaidi ya shilingi 700,000, anayo matofali 500 na kiwanja, biashara ya mitumba nchini Kenya.

Mpango wake huo, ni zao la ule mpango wa kunusuru kaya maskini, unaosimamiwa na TASAF tokea mwaka 2014, ambapo kila baada ya miezi mwili, hujipatia ruzuku kati ya shilingi 30,000 hadi shilingi 44,000.

Ijapokuwa mlengwa mmoja na mwengine hutofautiana upatikanaji wa ruzuku hiyo, lakini zipo fedha za msingi (lazima) ambapo kila mlengwa, hupata shilling 20,000.

Anakiri kuwa, mpango ya kuingizwa kwenye utaratibu wa TASAF, kwake ulikuwa sahihi, kwani hapo kabla, alikuwa akiishi kiwango cha shilingi 5000 kwa mwezi.

KABLA YA KUINGIA TASAF

Kwake mlo wa siku, hakuwa na hakika nao, kutokana na kutokuwa na hata njia moja, ya uhakika ya kujiingizia kipato, licha ya kutegemewa na watoto wake wanne wakati huo.

“Asubuhi nikiamka, ilikuwa najiuliza kwanza nisuke makuti ya mnazi niuze nipate kiamsha kinywa, au niende shambani kulima muhogo, jambo hilo lililoniweka roho juu,’’anasimulia.

Kwa wakati huo, huku akipambana na maisha bila ya mafanikio, alikuwa akiishi kwenye nyumba ya tope, iliyoezekwa makuti ya mnazi, iliyokuwa na mlango mmoja wa bao moja lisilo rasmi.

Huduma za watoto alioachiwa na mume wake, zilikuwa za omba omba tena bila ya mafanikio, na wakati mwengine kujifungia ndani, pasi na kifungua kinywa.

Suala la watoto wake kwenda skuli, kutasaka haki ya elimu na madrssa, lilikuwa la kubahatisha, kutokana na maisha yake kuzungurukwa na changamoto hasa za kipato.

“Ilikuwa nikihitaji shilingi 1000, kama ninae hitajia shilingi 500,000 hapo ni kusuka makuti, ili kutatua changamoto zangu na watoto wangu za kimaisha,’’anasimulia.



Anakumba vyema, wakati anapodaiwa michango ya familia, iwe ya kufiwa, harusi na ugonjwa na kuieleza familia juu ya kukosa kwake, hakuwa akifahamika juu ya hilo.

Hakuna hata siku moja, aliyoota ndoto ya kuondokana na hali hiyo ngumu au kuishi kwenye nyumba ya kisasa, kama walivyo wetu wengine.

Hii ni kutokana na mipango yake ya kimaisha, hasa ya kutafuta fedha, haikuwa na mwelekeo, achia mbali mlo wa kila siku ambao ni wa lazima.

BAADA YA TASAF

Kuanzia mwaka 2014, anasema baada ya kuitwa na kuhojiwa na uongozi wa shehia ya Chimba wilaya ya Micheweni, hakuamini alichoelezwa.

“Si unajua kila mmoja atapita, huyu atakuhoji, huyu atakuandika, yule atakupiga picha na mwengine hadi kuchora ramani ya unapoishi, lakini mwisho wa siku, hakuna jambo,’’anasema.

Hata kwa upande wa mpango huo wa kunusuru kaya maskini, rasmi alijenga roho ya tamaa na furaha, baada ya mara ya kwanza kupokea ruzuku ya shilingi 44,000.

“Fedha hizo, kwanza niliwanunulia watoto wangu vifaa vyote vya skuli na madrassa, na kisha saa siku hiyo 7:00 mchana nilipika chakula kizuri na samaki mnene,’’anahadithia.

Miaka nenda miaka rudi, Khadija sasa akawa anaendelea kupokea fedha hizo, kati ya shilingi 30,000 hadi shilingi 80,000 wakati mwengine, hutegemeana uwepo wa ajira za muda.

Baada ya miezi minane, kuona mpango huo umedumu mikononi mwake, alianza mikakati ya kuziendeleza fedha hizo, huku moja akipiga hesabu, namna ambavyo ataanzisha ujenzi wa nyumba ya kisasa.



‘’Hapo baada ya kuzaa wazo la ujenzi, nikaanza kuzigawa fedha nusu nakula na kuhudumia watoto, na nyingne nafundika (akiba) pembeni hadi zikatimia shilingi 150,000,’’anasema.

Hapo sasa aliwaita watoto wake, na hasa baada ya familia kumkubalia ombi la kununua kiwanja cha ujenzi wa nyumba.

‘’Kiwanja niliuzia shilingi 300,000 na mimi nikatoa shilingi 150,000 na watoto wangu wakanisaidia kima kama hicho, na sasa nn ummiliki rasmi,’’anasimulia.

 Huku watoto wakienda skuli, bila ya shaka na kazi zake nyingine aliendelea zao kama vile kilimo, kuuza nazi naususi wa makuti ya mnazi, wazo sasa likawa ni kuanzisha biashara.

“Nilimshauri mtoto wangu anaekwenda kwa uvuvi nchini Kenya, aninunulie nguo za mtumba, na kisha azipeleka huko, maana biashara hiyo inakwenda,’’anasema.

Kwa hatua za mwanzo, alinunua mitumba ya shilingi 150,000 na baada ya kuuza, alipata faida ya shilingi 50,000 na kuingia ari mara mbili.

Walishasema wahenga kuwa, utamu wa sukari huja mwisho, nae sasa baada ya kupata faida hiyo ya awali, mara ya pili alituma mzigo wa shilingi 250,000.

Kwa awamu ya pili, biashara haikuwa mzuri, ingawa mlengwa huyo wa kaya maskini, alijipatia faida ya shilingi 30,000 ambapo mara ya tatu, alituma tena mzigo wa shilingi 300,000.




“Kwa sasa sipungui wastani wa mtaji wa shilingi 700,000 kama mtaji ambapo naendelea na biashara yangu hiyo, na tayari pia nimeshanunua matofali 500,’’anaeleza.

Kumbe wakati huu akiendelea na ujasirimali wake wa nguo za mitumba, akiwa anamilki kiwanja cha kujenga nyumba na matofali yake 500, pia ni mkulimwa wa mboga.

“Nataka nyumba yangu iwe na vyumba vinne na vyoo viwili, ili sasa familia yangu na hasa wajukuu, wapate utulivu zaidi kupitia matunda haya ya TASAF,’’anasema.

Kwenye kilimo cha mboga, alikojiegesha na wenzake wa mpango wa kunusuru kaya maskini, hujipatia faida kati ya shilingi 30,000 hadi shilingi 40,000 kwa mwezi hutegemea na soko lilivyoamka.

Kwenye mfuko wa ushirika wao wa kuweka na kukopa, mlengwa huyo anatimiza shilingi 350,000 kama mtaji wake binafsi, ambpo wakati mwengine, hukopa na kulipa.

‘’Unajua TASAF ilitutaka tuhakikisha fedha za ruzuku wanazotupa zisiishie kwenye dishi pekee, bali tuziekeze ili zizae, na hili nalifanya kwa vitendo,’’anasema.

Kwake yeye anaamani siku moja TASAF itakapoondoka mikononi mwake, na kwenda kwa wenzake, awe na jambo la kujisifia kimaisha.

MALENGO YAKE BAABADAE

Moja ni kuwa na mlango wa wa duku, ambapo hapo sasa anatarajia kuwa na biashara ya nguo, zisizokuwa za mitumba, na kuhakikisha wajukuu anaowalea, anasomesha hadi chuo kikuu.

Kwa sasa mlengwa huyo wa kaya maskini, anaendelea na shughuli zake kama kilimo, ususi wa makuti akiongeza na ujasriamali wa nguo za maitumba.

SHEHA 

Sheha wa shehia ya Chimba wilaya ya Micheweni Saleh Salim Khamis, anasema shehia yake, inawananchi 168 waliomo kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini, kati ya wananchi 4,215.

Anacho cha kujivunia ndani ya shehia yake, ikiwemo walengwa hao kuanzisha vikundi saba vya ushirika, vyenye wanachama zaidi ya 150.

“Kwenye shehia yangu, pamoja na mlengwa mmoja mmoja kujiajiri, ipo miradi ya mikubwa, ambayo wananchi wote wamenufaika nayo,’’anasema.

Hata hivyo Katibu wa sheha wa shehia hiyo Omar Salim Hamad, anasema TASAF, imeikomboa shehia yao kwa kuwepo vikundi ambavyo kwa njia ama nyingine, wanachama wake wameshaondokana na umaskini wa kipato.



‘’Mfano ushirika wa maskini hajengi, wanaolima mboga na ufugaji wa kuku, lako jicho ni ushirika wa ufugaji, uwekaji hisa na kilimo cha mboga na kukusanya walengwa 20,’’anasimulia.

TASAF

Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said, anasema wapo walengwa 14,280 kwa Pemba ambao wanaendelea kupata fedha za kunusuriwa na umaskini.

Walengwa hao wapo kwenye shehia 78, ikiwemo za Tumbe Mashariki, Chimba, Makangale, Kiwani, Ndagoni, Ukunjwi na Fundo.

Ambapo tayari TASAF Pemba, imestumia shilingi bilioni 14.4 kwa ajili ya kuwapa ruzuku walengwa hao, fedha za kazi na zile za msingi, pamoja na za masharti.

Tayari kila shehia, kati ya hizo 78, zimesafikiwa na wastani wa zaidi ya shilingi milioni 230, ambapo kwenye walengwa wote 14,280 wa Pemba, na kila mmoja ameshasaini shilingi milioni 274.619, ingawa inategemeana na eneo husika.

Mratibu wa TASAF, alimtolea mfano wa kuigwa mlengwa Khadija wa Chimba, Amina wa Mgogoni na mwenzake Mfaki kuwa wameyatekeleza kwa vitendo malengo hasa ya mpango huo.

‘’Wenzetu kama hawa ambao wapo zaidi ya 50,000 kwa Pemba nzima, wamekwenda sambamba hasa na malengo na mwelekeo wa TASAF, wa kumtoa mwananchi katika unyonge hasa wa kipato,’’anasema.

Jengine ambalo ni jema, ni kwa walengwa hao kuanzia mwaka   2014 hadi mwaka 2018 kuibua miradi ya jamii 146, kwa ajili ya wananchi, kama vile ufufuaji wa mito ya asili na ujenzi wa daraja ndogo.

‘’Mfano wa miradi hii hata Makangale upo wa upandaji miti, ujenzi wa matuta ya kuzuilia maji ya chumvi, mfano Ndagoni, Tumbe na Micheweni,’’anafafanua Mratib wa TASAF Pemba.

 Achia mbali idadi ya watu 50,000 waliojiwekeza wenyewe, vipo vikundi 942 vikizaa walengwa 12,000 vilivyoanzishwa, kuanzia mwaka 2014 hadi sasa, ingawa vilivyosajiliwa ni 700.

SERIKALI KUU  

Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdall, anasema lengo la TASAF ni kuona mwananchi mmoja mmoja anaondoka kwenye wingu la umaskini hasa wa kipato.

Anasema, fedha zilizotumiwa na TASAF Pemba pekee wastani wa shilingi bilioni 14.4 lazima zizae matunda, ili wananchi waweza kuongeza pato lao.

                     Mwisho            

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch