Skip to main content

WEMA PEMBA YAWAJENGEA UWEZO WASHAURI WA MASOMO

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA::::

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imewajengea uwezo washauri wa masomo, ili kuboresha zaidi katika kufanya ufuatiliaji, ushauri katika ufundishaji pamoja na upimaji kwa wanafunzi.

Akifungua mkutano kwa washauri hao, leo August 8, 2022 Kaimu Mratibu Idara ya Mafunzo ya Ualimu WEMA Pemba, Mzee Ali Abdalla alisema mafunzo hayo yatasaidia kuboresha kiwango cha ufaulu kwa wananfunzi.

Alisema kuwa, katika ufuatiliaji imeonekana kuwa kuna changamoto kwenyea kutunga maswali yenye umahiri katika pimaji na mitihani, hivyo Wizara imeona kwamba ipo haja ya kuliomba Baraza la Mitihani Tanzania kuwapa mafunzo washauri wa masomo, ili na wao waweze kuwajengea uwezo walimu.

‘’Kutokana na changamoto hiyo, tumeona kwamba tutumie fursa hii, kwani Baraza la mitihali limekuwa likitoa mafunzo haya kwa maafisa mitihani katika halmashauri na skuli mbali mbali’’, alisema Kaimu huyo.

Alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kwamba baada ya mafunzo wawe na uwezo wa upimaji unaozingatia umahiri, utungaji maswali, maswali ya kuchagua, kuoanisha, ya majibu mafupi, ya kweli au si kweli, insha, muundo wa mitihani na jeduweli la mtihani.

Alieleza kuwa, wanatumai kwamba kila mmoja atashiriki kikamilifu katika mafunzo hayo na kupata umahiri uliokusudiwa, ili kuweza kuutumia katika kazi za kila siku zinazohusu maswala ya upimaji na utahini.

‘’Tunategemea kuwa mtatumia ujuzi na maarifa mtakayoyapata, ili kwenda kuwajengea uwezo walimu na kufanya ufuatiliaji ili kuona namna wanavyoandaa mitihani ya ndani kama inavyotakiwa’’, alieleza.

Kwa upande wake muwezeshaji kutoka NECTA Beata Xavery alisema kuwa, suala la elimu katika Taifa ni la msingi sana kwa sababu fani zote zinatoka katika elimu, hivyo jukumu la kusimamia utoaji wa elimu na upimaji ni suala nyeti katika Taifa lolote lililopiga hatua.

‘’Nimeona fahari kutokana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia viongozi wa Wizara hii kuona umuhimu wa mafunzo haya ya upimaji unaozingatia umahiri kwa lengo la kuimarisha elimu katika skuli kwa ajili ya watoto wetu’’, alieleza.

Alifahamisha kuwa, upimaji bora katika skuli ndio unachochea ufundishaji, hivyo aliwaomba kuitumia fursa hiyo watakayoipata kwenye mafunzo hayo kwa ajili ya kujenga Taifa bora la baadae.

Mkuu wa Seksheni ya Mafunzo ya ualimu Kazini Fatma Ali Salim alisema kuwa, mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuwawezesha washauri wao wa masomo katika vituo vya walimu (TC), ili kuweza kwenda sambamba na mtaala mpya wa CBC ambayo itawafanya walimu kuwa na umahiri mkubwa katika kufundisha na kuwatathmini wanafunzi.

‘’Baada ya mafunzo haya tunatarajia kwamba washauri wetu wa masomo watakuwa wanajengeka kiuwezo na kiumahiri zaidi kuwapitia walimu kuwafundisha namna bora ya utungaji mitihani na namna gani wataweza kuwapima wanafunzi kwa hatua tofauti’’, alisema.

Nae Afisa Ufuatiliaji na Tathmini Idara ya Mafunzo ya Ualimu Pemba (DTA) Khamis Adam Suleiman alieleza kuwa, mafunzo hayo yataongeza ufanisi kwa walimu ambao utafanikisha kuwaboresha wanafunzi na kufaulu vizuri katika mitihani yao kwa kiwango cha juu.

Mafunzo hayo ya siku tano kuhusu upimaji unaozingatia umahiri, yamewashirikisha washauri wa masomo na maafisa kutoka Idara ya Elimu Pemba.

                                                       MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch