Skip to main content

KATIBU TAWALA MKOANI AWAPA NENO WAKULIMA WA KARAFUU

 

             


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::::


KATIBU Tawala Wilaya ya Mkoani Pemba Miza Hassan Faki amewakumbusha wakulima wa zao la karafuu Wilayani humo kutokuzichanganya karafuu zao na takataka nyengine ikiwemo makonyo kwani kufanya hivyo kunaweza kulipoteza ubora zao hilo.

Alisema karafuu za Zanzibar zina ubora wa aina yake kuliko maeneo yote Duniani hivyo, ni wajibu kwa wakulima hao kulifahamu hilo na kuenzi ili liweze kubakia katika ubora wake.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Mkoani alisema, ubora wa zao hilo ni vyema ukaanzia kwa wakulima iwe katika kulianika kwenye vyombo vinavostahiki.

Alieleza kuwa, uwanikaji wa karafuu katika saruji, lami, bati na katika vyombo sehemu inayoanza kupoteza ubora na kuanza kuingia takataka nyengine.

Katibu Tawala huyo alieleza kuwa, ubora wa zao hilo baada ya kuvunwa kwake hutakiwa kuanikwa katika vyombo maalumu kama vile majamvi na mikeka ili kudhibiti mafuta ya karafuu hizo yasipotee kabla ya kufikishwa kituoni kwa ajili ya kuuzwa.

“Niwakumbushe wakulima wa zao la karafuu waacha kuanika karafuu sehemu za ovyo ovyo na wahakikishe wanazifanyia usafi wa kina ikiwemo kutoa makonyo na taka nyengine kabla ya kufikishwa sokoni ili kudhibiti ubora wake,” alisema.

Katika hatua nyengine Katibu tawala huyo aliwataka wananchi kutoa taarifa wakati wowote wanapoona viashiria vya usafirishaji wa zao hilo kwa njia ya magendo.

Alisema, serikali imeweka bei muafaka ya zao hilo ili wakulima na wananchi wengine wauze katika vituo vya shirika la biashara la taifa la ZSTC hivyo kusiwe na sababu ya kusafirishwa kwa njia ya magendo.

“Maana kuna baadhi ya wananchi bado hawajakubali kuuza karafuu katika vituo vilivyowekwa hivyo ni vyema wakauza kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa kwani sheria zitachuliwa kwa watakaobainika,” alisema.


Wakati huo huo Katibu tawala huyo aliwataka masheha wa Wilaya hiyo kuendelea kutoa taarifa ya upigaji marufuku kwa baadhi ya wananchi kujihusisha na ununuzi wa zao la karafuu kwani ni kichocheo kikubwa cha wizi.

Wakulima wa zao hilo Wilaya ya Mkoani wameiomba serikali kuendelea kusimamia uuzaji wa zao hilo ZSTC na sio kwa wananchi waliomitaani kwani husababishwa kwa kiasi kikubwa wizi wa karafuu.



Mmoja kati ya wakulima hao Seif Salim Seif mkaazi wa Kengeja alisema, uwepo wa wanunuaji wa karafuu kiholela ndio moja ya sababu ya kuchangia kuibiwa kwa karafuu zao.

“Moja ya sababu inayochangia wizi wa zao hilo ni uwepo wa wanunuzi wasiokuwa ZSTC jambo ambalo hutupa wakati mgumu sisi wakulima wa zao la karafuu,” alieleza mkulima huyo.

Nae Mkulima Issa Mohamed Othaman mkaazi wa Kengeja aliwaomba masheha kuwashughulikia kisheria wananchi wanaonunua zao hilo ili kupunguza wimbi lililoibuka katika kipindi hichi.

Kwa upande wake Sheha wa shehia ya Ngwachani Mkoani Issa Ismail Juma alisema, ununuzi wa zao kwa wananchi ni kinyume na utaratibu uliopangwa na serikali hivyo aliwataka wananchi wafuate sheria zilizoekwa na sio kufanya wanavotaka wao.

Agosti 17 mwaka huu Waziri wa Biashara na maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaban alifanya uzinduzi wa uvunaji wa zao la karafuu katika mashamba ya zao hilo Wilaya ya Mkoani Kisiwani hapa.

                                               MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch