Skip to main content

MEIYE HAMAD: MJASIRIAMALI WA PEMBA ALIYEANZA KAMA MCHICHA SASA NI MBUYU

 



NA MARYAM SALUM, PEMBA

 WATU wa zamani walishasema kuwa, maisha ni kutafuta na sio kutafutana.

Wengine wakaibuka wakisema kuwa, mtafutaji hachoki na mgagaa na upwa hali ugali mkavu.

Hapa walilenga mbali kuwa, mtafutaji hachoki na mafanikio yanahitaji juhudi binafsi na wala hayashuki tu kama mvua mawinguni.

Misemo hii sasa yamesadifu kwa vitendo kwa mjasiriamali Meiye Hamad Juma (47), akiishi kijiji cha Mavungwa shehia ya Mbuzini nje kidogo na mji wa Chake Chake Pemba.

ALIPOANZIA UJASIRIAMALI

Mwaka 2016, ndio bisummillah, mjasiriamali huyo alipofunuka macho yake mawili, na kuanza kama mchicha kwenye ujasiriamali wake.

Kwa wakati huo akiwa ni mmoja wa wanachama wa ushirika wa “Tupate Sote” na kujiunza shughuli mbali mbali za utengenezaji bidhaa.

Lakini 2018, Meiye alipoamua kuanzisha kikundi chake, kwa kutengeneza bidhaa mbali mbali ambazo kwa sasa zimemkomboa kimaisha.

‘’Bidhaa ambazo kwa sasa natengeneza baadhi ni zile nilizoziona kule kwenye ushirika wangu wa awali, kama vile sabuni ya maji, unga wa lishe unaotokana  na mchanganyiko wa  nafaka  na mbegu za boga.

Kwake bidhaa hizo zinampa mafanikio makubwa, ikiwemo kujiamini katika maisha, kupatikana kwa ada na kuendesha shughuli za familia yake.



Baada ya kuwiva kiujasiriamali, aliamua kusomesha wajasiriamali wa wengine kisiwani Pemba, ili waweze kutengeneza bidhaa zao zikiwa kwenye ubora zaidi.

Kumbe Meiye, ni wale wanaoitekeleza kwa vitendo, ile aya inayomtaka kila mmoja kufikisha aya japo moja kwa wenzake, na yeye aliamua kuwasomesha wengine.

“Nafasi hiyo ya kusomesha Wajasiriamali wenzangu nilipatiwa na watendaji wa TAMWA, kwa lengo la kuwaendeleza zaidi kiutendaji na kuboresha bidhaa zao”, aliongeza.

KUKUA KWA MIEYE KIUJASIRIAMALI

Mwaka 2017 alifanikiwa kutumia taaluma yake kwa kubuni mradi wa kupanda alizeti, na kwa bahati, walifanikiwa na kujipatia mafanikio makubwa.

“Baada ya kuvuna alizeti na kuuza, pia tulipatiwa mashine kutoka TAMWA ili kuendeleza mradi huo na tunajivunia  kwa  hilo”, anasema.

Mwaka mmoja baadae, alianzisha ushirika wake rasmi, unaojumuisha wanaume watatu na wanawake sita, kutoka maeneo tofauti kisiwani Pemba.

Mradi huo aliuanzisha kwa mtaji wa shilingi 40,000 baada ya kukosa kwenye kisanduku (hisa) na kwa sasa yupo na mtaji wa shilingi 4,000,000.

Ushirika aliouanzisha unajishughulisha na utengenezaji wa skrabu ya mwani, mafuta ya mwani, unga wa lishe kwa kutumia bidhaa tofauti, majani ya chai pamoja na karafuu za singo.

“Kipaji changu cha ujasiriamali kumenyanyua maisha yangu na familia pamoja na watu wengine, na hasa baada ya kuanzisha ushirika wangu mwenyewe,’’anasema.

MAFANIKIO

 Moja kuhwa ni kufanikiwa kujenga nyumba ya kisasa yenye miundombinu yote ikiwemo umeme na maji pamoja na kumiliki vifaa kama friji pamoja na majiko ya umeme.

Anayoma maduka mawili moja lipo kijijini kwao Mavungwa, na moja lipo eneo la Machomane kituo cha Boda boda wilaya ya Chake chake Pemba.

Safari za mikoa mbali mbali ya Tanzania, na kubwa zaidi na mshiriki wa zaidi ya miaka saba ya maonesho yanyofanyika Tanzania bara.


“ Mwaka  huu  nimempeleka kijana ambae nimemuajiri ili  apate kuona mengi, na kupata  uzoefu zaidi  na kutangaza biadhaa zake”,alisema.

 


CHANGAMOTO.

Moja ya changamoto kubwa ni ukosefu wa mashine ya kutengenezea mafuta, kwani hutumia sufuria kwa kutumia na mikono, jambo ambalo   linaweza kuathiri afya yake.

Jengine ni kuingia gharama za kuvifuata vifungashio nje ya Zanzibar, kutokuwa na soko la uhakika la kuuzia bidhaa zake, usafiri wakusambazia bidhaa.

“Hutembea kwa miguu hadi kwenye maofisi, jambo ambalo linanipa wakati mgumu,’’alisema.

Anasema baada ya kuuliza bei mashine hizo, zinauzwa kati ya shilingi milioni 18, na nyengine ni shilingi milioni 4 ya kupikia mafuta na shilingi milioni 3.5 mashine kwa ajili ya kusagia.

Hata hivyo amewakumbusha wanawake wenzake, pamoja na vijana kujiunga na vikundi vya miradi  ya maendeleo, ambavyo vitawasaidia katika kujiinua kiuchumi.

 

MUME WA MJASIRIAMALIA

Hamad Bakari (Meja), anasema, alianza kumsaidia na kumpa ushirikiano mke huyo, tokea anaanza sasa, ingawa kutokana na hali yake sasa amebaki kama mshauri.

Uamuzi wake, anasema ulitokana na kuogopa mke wake, kukata tamaa mapema, katika kuendeleza mradi wake, ambao kwa sasa anakiri umempa uhakika wa maisha.

 “Kwanza mke wangu tumeaminiana namuamini ananiamini popote anapokwenda, maana alianza kwa kasia na sasa anaiendeleza ambayo imenipa heshima mimi hapa mtaani,’’anasilimulia.

Mume huyo tokea mwanzo na hasa alipokuwa mazima wa miguu, alikuwa ndio msambaazaji mkuu wa bidhaa zinazozalishwa na mke wake.

‘’Sikuwa naona haya wala aibu kusambaaza bidhaa na kuwaeleza wateja hata wanaume wenzangu, kuwa hizi zimezalishwa na mke wangu,’’anaeleza.

Kwa sasana kutokana na kupevuka kwa mjasiriamali huyo, changamoto kubwa ni usafiri wa kusambaazia bidhaa zake na soko lisilo la uhakika.

 

WALIOPATIWA MAFUNZO NA MEIYE

Bikombo Abdalla Hamad, mkaazi wa Micheweni, yeye alimuelezea Meiye kwamba ni mjasiriamali mkubwa anayejulikana kwa kila sekta kwenye maeneo mbali mbali ndani ya nchi na nje ya nchi.

“Meiye hana roho mbaya katika kuwapatia mafunzo wengine kwenye ujasiriamali, lengo ni kuona wanatengeneza bidhaa zao kwa weledi na viwango na sio kimazoea,” alimsifia.

Alisema Meiye alipata mafunzo kutoka kwenye taasisi mbali mbali, lakini baada ya kupata mafunzo hayo, akaona ili elimu ifanye kazi ni vyema kuwapatia na wengine.

Mjasiriamali Bikombo alisema faida aliyoipata  kutoka kwa  Meiye  ni kupata elimu zaidi ya kusarifu zao la mwani katika kutengeneza sabuni, mafuta ya aina mbalimbali.

 

MTEJA WA BIDHAA ZA MEIYE

Fatma Juma Kombo, mteja maarufu wa kununua  bidhaa za Meiye kama sabuni, anasema hupendelea bidhaa zake kwasababu ni nzuri, hazina kemikali.

Anasifia akisema kuwa, bidhaa za Meiye ikiwemo unga wa uji  unamsaidia katika makuzi ya watoto wake, mafuta anayotumia huondoa maradhi kama mba, fangasi na kuzifanya nywele zake kupendeza na zenye kuvutia.




“Meiye ni mjasiriamali anaejali na kuipenda kazi yake na wateja wake, kwani hufuata mteja popote, ili kumfikishia bidhaa anayohitaji bila kujali changamoto anazopitia,” alisema Fatma.

 

TAMWA

Fat-hiya Mussa Said, Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzani TAMWA-Zanzibar, Ofisi ya Pemba anasema Meiye ni miongoni mwa wajasiriamali,  ambao wamewawezesha kitaalamu katika kubuni, kuanzisha na kuiendeleza miradi yao kiuutalamu zaidi na yenye ubora.

                              MWISHO.

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch