Skip to main content

MAKAMU WA PILI AKIWA PEMBA, AWAPA DARSA WAALIMU WAKUU

 

                                               


NA ZUHURA JUMA,  PEMBA 

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah amewataka walimu wakuu wa skuli zote kisiwani Pemba kusimamia uwajibikaji na nidhamu kwa walimu wao, ili wafanye kazi kwa ufanisi na kuleta maendeleo kwa wanafunzi.

 

Alisema kuwa, kuna baadhi ya walimu hawafundishi vizuri, wanaingia na kutoka kazini muda wanaotaka, jambo ambalo linasababisha kudumaza maendeleo ya wanafunzi na hatimae kuwa na ufaulu wa kiwango cha chini.

 

Akizungumzia mara baada ya kusikiliza changamoto za walimu Mkoa wa Kaskazini Pemba, Makamu huyo alisema, wasiende kuchafua mafaili yao kwa chuki binafsi, bali wawape miongozo inayotakiwa kwa mujibu wa Sheria, ili kufikia yale yanayoitaka Serikali.

 

"Nawasisitiza kutimiza wajibu wenu kisheria na sio kwa chuki, kwa sababu kuna walimu hawasomeshi vizuri, wanaingia na kutoka kazini muda wanaotaka lakini kwenye taarifa zao zote zinazotetwa ni nzuri kwenye mafaili yao", alisema.

 

Alisema kuwa, Serikali ya awamu ya nane kupitia Dk Mwinyi imekusudia kuweka mkazo kwenye Elimu, kwani wanaamini kwamba kuekeza kwenye sekta hiyo ni mafanikio katika sekta zote nchini.

 

"Tuanze kufanya vizuri kwenye skuli za maandalizi, tutakuwa na wanafunzi bora na wenye uwezo wenye kiwango kinachokubaliwa, tunataka wanafunzi wawe na uwezo mzuri wa kufanya kazi", alieleza Makamu huyo.

 

Aidha Mhe. Hemed aliitaka Wizara hiyo kuhakikisha inawapa maslahi yote walimu, ili waendelee kufanya kazi vizuri na kuwanasihi kufanya kazi kwa amani kwani hakuna haki ya mtu ambayo itapotea.

 

"Natoa angalizo na muwape taarifa vizuri kwa kila alieomba ajira za uwalimu Pemba ajue anakuja kufanya kazi hapa hapa, kila mmoja aomba katika makaazi husika, Wizara izingatie hilo hakuna kupewa uhamisho, kwani ndio inayochangia uhaba wa walimu", alisema.

 

Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Mohamed Mussa alisema, lengo la mkutano huo ni kusisitiza uajiwajibikaji kwa walimu pamoja na kumaliza changamoto zinazowakabili, ili kuongeza ufanisi katika ufundishaji.

 

Waziri huyo alimshukuru Dk. Mwinyi kwa kuithamini sekta ya elimu ili kuona kwamba inaboreka zaidi katika visiwa vya Zanzibar kwa lengo la kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi.

 

Alisema kuwa, ni wazi kwamba Serikali ya awamu ya nane imewekeza katika elimu kwani kupitia fedha za UVUVO 19 wamepatiwa bilioni 68 ambazo ni sawa na bajeti ya miaka 11 ya Serikali ambayo inaipa Wizara kila mwaka.

 

"Mjitahidi kuzisema changamoto zenu zinazowakabili hapa, lengo letu ni kuboresha sekta ya elimu na kuhakikisha tunapata wanafunzi bora watakaofaulu vizuri ", alisema.

 

Nae Afisa Mdhamini Wizara hiyo Mohamed Nassor Salim aliishauri Wizara hiyo kuajiri waalimu ambao ni wakaazi wa maeneo husika, ili wapate fursa sambamba na kuepuka uhamisho kwa walimu.

 

"Wanapoajiriwa walimu wanaotoka eneo lile lile, kutakuwa na walimu wakaazi, kwa mfano Makangale tuna vijana 36 wamesomea fani ya ualimu hivyo tusichukue vijana wa nje", alisema 

 

Alisema, katika kuhakikisha wanaweka mazingira bora kwa wanafunzi, wanajitahidi kutatua changamoto mbali mbali ikiwemo kujenga vyoo zaidi ya 300 pamoja kuwaondoa watoto kukaa kwenye sakafu.

 

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alisema, watahakikisha wanaiunga mkono Serikali kwa kuwapa kipao kwenye ajira walimu wanaojitolea, kwani wamekuwa wakisaidia maendeleo ya wanafunzi katika skuli mbali mbali.

 

"Walimu wanaojitolea wanafanya kazi kwa bidii na kwa nguvu zote, hivyo tutajitahidi kuwapatia ajira kwanza", alisema Mkuu huyo.

 

Wakitoa changamoto zao, walimu wa skuli za Serikali walisema wanahitaji kurejeshewa nauli walizokuwa wakipewa, ili kufika skuli kwa wakati, kusaidiwa vifaa vya michezo pamoja na kijengewa madarasa kwa skuli zenye uhitaji.

 

"Walimu wanaokwenda kusoma tunaomba wanaporudi wasipelekwe wizarani, elimu watakayoipata wailete kwa wanafunzi, ili kuongeza kufanisi na ufaulu wa kiwango cha juu", walisema.

 

Nao walimu wa skuli za binafsi waliiomba Serikali kuwapunguzia kodi, ili kuendelea kuekeza katika sekta ya elimu sambamba na kuwasaidia kuwapatia usafiri kwa ajili ya wanafunzi wao, kwani hawana uwezo na tayari wameshazuiwa kutumia usafiri wa gari za abiria kusafirisha wanafunzi hao.

 

"Hatukatai kulipa Kodi kwani tunajua kuwa ni muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu, lakini zimekuwa nyingi kiasi ambacho tunakaribia kukata tamaa", walisema.

 

Mkurugenzi Sera na Mipango kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar alisema kuwa, Serikali imejitahidi kutatua changamoto ya kujenga skuli na madarasa kupitia mradi wa UVIKO 19 ingawa kwa hatua ya awali imeangalia skuli zenye uhitaji zaidi.

 

"Kazi za ujenzi wa madarasa zinaendelea hivyo tuwe wastahamilivu Serikali inaendelea kutatua changamoto hizo, pia tutahakikisha kila Wilaya kunakuwa na skuli zenye dakhalia kadiri uwezo utakavyoruhusu", alisema Mkurugenzi huyo.

 

Mkutano huo umewashirikisha walimu wakuu na wasaidizi wa skuli za Serikali na binafsi, walimu wakuu wa vyuo, wenyeviti na kamati za skuli, ukiwa na lengo la kutoa changamoto zao zinazowakabili na kuweza kutafutiwa njia mbadala ya kutatua.

 

                   MWISHO.

 

 

 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch