Skip to main content

‘PPC’ KLABU ILIYOWATOA MAFICHONI WAANDISHI WA HABARI PEMBA KIMAFUNZO

 



NA HANIFA SALIM, PEMBA

WAANDISHI wa habari ni watu muhimu katika jamii yoyote ile ulimwenguni.

Maana moja ya majumku yao ambayo sio rahisi kufanya na kundi jengine la watu ni kule, kuelimisha, kuburudisha na kuhabarisha iwe kijamii, kisiasa,kiutamaduni na kiuchumi.

Licha ya changamoto ambazo wanakumbana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, bado wana dhima kubwa ya kuipatia jamii taarifa ambazo zinatokezea kila siku.

Pamoja na kadhia hiyo taasisi kama hizo za vilabu vyao, ‘Press Club’ huwa zinasimama wima, kuwatetea waandishi hao wanaokumbwa na madhila kadha.

Mei 3 ya kila mwaka duniani kote, kunaadhishwa siku ya uhuru wa vyombo vya habari, ni siku muhimu kwa waandishi wa habari.

Waandishi wa habari wamekuwa wakifanya kazi zao kwa mujibu wa katiba zote mbili, ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Zanzibar ya mwaka 1984 ambazo  zinahimiza upatikanaji wa habari na kutowa habari kwa wananchi.

Kwa kawaida kila jambo ambalo linamaslahi na watu ili liweze kuenda sawa ni vyema kuwa na umoja wao kama vile vyama, jumuiya na vyenginevyo.

PPC

Klabu ya waandishi wa habari Pemba, ndio ndio kimbilio pekee kwa waandishi wote wa habari na watangazaji kisiwani humo.

Kama ilivyo miunganiko yote, nao PPC waliamua kuanzisha umoja, wao kwa malengo kadhaa moja wapo ni kuwa na suati moja.

Pemba Press Club (PPC) tokea kuanzishwa kwake mwaka 2002, imefanya mambo kadhaa yenye kuwajengea uwezo waandishi wa habari, juu ya utendaji wa kazi zao za kila siku yakiwemo mafunzo na ziara za kimasomo.

MWANZILISHI WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI (PPC)

Klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) ilianzishwa mwezi Disemba mwaka 2002, ikiwa na wanachama 30 wakati huo, chini ya Mwenyekiti Azizi Simai Alawi.

Chimbuko la klabu hiyo, lilianzia mwaka 1986, wakati Mwenyekiti huyo alipopata safari ya kwenda Ujerumani, katika matembezi ya kujifunza kitaaluma.

“Nilipata ushauri kutoka kwa uwongozi wa Ujerumani, tuanzishe Klabu na watatusaidia, baada ya kurudi nilikaa na uongozi wa wizara ya habari, wakatupatia ofisi tukaanza kufanya kazi,’’anaeleza.

Baada ya hapo waandishi wa habari wa Unguja, walikua na jumuiya ya waandishi wa habari wa Zanzibar (JAZZ), ambayo ilimteua kuwa Mratibu wa jumuiya hiyo Pemba.

Mwaka 2002, alichaguliwa kwenda mkoani Mwanza Tanzania bara, kuhudhuria mafunzo na alitakiwa kuanzisha tena Klabu ya waandishi wa habari Pemba.

“Kwa mara ya pili tulipoanzisha (PPC) tulikuwa na ofisi katika eneo la stendi kuu ya gari sokoni mjini Chake chake, tulipata misaada mbali mbali kutoka kwa Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC),’’alieleza.

Walianza kwa kuandika miradi ya kuelimisha waandishi wa habari, kuandika habari za uchunguzi kwa kushirikiana na uongozi wa klabu ya waandishi wa habari wa Zanzibar ‘ZPC’.



Anasema PPC imesaidia waandishi, kwa kuwaelimisha maadili ya uwandishi wa habari, kuandika habari za uchunguzi, habari za michezo, za vijijini, za uchaguzi na makala za aina mbali mbali.

Kuwepo kwa PPC kumekuwa na faida kwa waandishi wa habari, kwani wamepata fursa za kujifunza, sambamba na tasisi zao walizoajiriwa.

MALENGO YA KUANZISHWA PPC

Ni kuibua vitu ambavyo vitapelekea klabu yao kukuwa na kujiimarisha na kujitegemea wenyewe, katika kuwahudumia wanachama wao.

“Tulikuwa na lengo ni kuanzishwa ‘Pemba Gazeti’ ambalo waandishi wa habari wangelazimika kuleta habari zao ambazo zitatolewa kupitia gazeti hilo iwe kama ni ajira,” anasema.

Mwazo yake kabla ya kuundwa kwa (PPC) ni kuanzisha redio jamii ya klabu hiyo, hivyo anawashauri viongozi wa (PPC) kutafakari namna ya kuwa na chombo bora cha kisasa kitakacho habarisha wananchi.

Aidha anasema walianzisha PPC baada ya kuona kundi kubwa la waandishi wamekuwa wakikosa eneo la kujifunza zaidi, kutokana na uhaba wa vyombo kwa wakati huo.

MWENYEKITI WA SASA WA PPC

Bakar Mussa Juma ambae ni Mwenyekiti wa nne wa PPC, anasema, klabu za aina hiyo zipo kila mkoa wa Tanzania.

Lengo lake ni kuwaunganisha wanahabari na kuwa ni chombo cha kupeleka malalamiko yao na kuwa ni chombo cha kuwatetea pale wanapokumbana na matatizo.

Klabu inatafuta miradi kupitia taasisi mbali mbali, ikiwemo shirika la Internews, wizara ya Afya na badala yake kutoa taaluma juu ya miradi hiyo.

“PPC imeshatoa mafunzo juu ya maradhi yasiyoambukiza, mafunzo ya uwandishi wa habari za biashara, uchunguzi na makala kadhaa, ambapo hivi karibuni tumetoa mafunzo ya uwandishi wa habari na changamoto za kidigitali,”anasema.

WAANDISHI WANAJIUNGAJE NA PPC?

Waandishi wa habari ‘wanachama’ wanapatikana kwa kupeleka maombi na kulipia kiingilio na ada ya kila mwezi, ambayo inatumika kwa uwendeshaji wa shughuli za ofisi.

Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) ni mlezi wa klabu za waandishi wa habari zote Tanzania, ambayo husaidia kutoa kodi ya ofisi, kumlipa mratibu wa klabu pamoja na kutoa vifaa vyengine vya kiutendaji.


PPC hutekeleza miradi ambayo hulenga zaidi kutoa taaluma kwa waandishi wa habari, juu ya kutumia kalamu zao kuihabarisha jamii ambapo ndio jukumu lao kubwa la kikatiba.

‘’Hata mafunzo kuhusu matumizi ya kanuni, miiko na maadili ya uwandishi wa habari ili habari zao zisiende kinyume na kazi yao, ‘’anafafanua.

MIKAKATI

Moja ni kuwafanya waandishi wa habari waweze kutumia kalamu zao na vyombo vyao ikiwemo televisheni, redio, mitandao na magezeti katika kuuhabarisha umma kupitia mambo mbali mbali.

Jambo la kujivunia kupitia klabu ya waandishi wa habari wa Pemba ni kutoa waandishi wa habari weledi, wenye taaluma za juu na uwezo mkubwa wa kuandika mambo mbali mbali.

MRATIBU WA PPC

Mratibu wa Klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) Mgeni Kombo Khamis anasema, wamekuwa wakitoa mafunzo ya kihabari, kukumbushana maadili na miongozo ya kazi zao.

Pamoja na hilo wamekuwa wakiwapatia mafunzo ya uandishi wa habari za afya, mazingira, mahakamani, uchunguzi, sera na utafiti na habari za vijijini ambazo zinawalenga wananchi.

PPC imeshatekeleza miradi mingi ikiwemo mradi wa kuelimisha wanawake kushiriki katika masuala ya usajiriamali kwa kutumia vyombo vya habari kupitia mradi wa sauti yangu mtaji wangu uliofadhiliwa na Tanzania media Fund (TMF) uliotekelezwa mwaka 2017/ 2018.

“Pia tulitekeleza miradi kupitia klabu yetu hata wa kudumisha amani mradi ambao ulifadhiliwa na shirika la Internews katika kipindi cha mwaka 2020,” anasema.

Mradi mwengine ni wa kuelimisha jamii juu ya maradhi ya kifua kikuu ambao unatekelezwa kupitia kitengo shirikishi kifua kikuu, ukimwi na ukoma kutoka wizara ya afya kwa ufadhili wa Global fund, ulioanza mwaka 2019 na unaendelea hadi sasa.

PPC kwa sasa ina wanachama 54 wakiwemo wanawake 26 na wanaume 28, .

MWENYEKITI MSAAFU WA PPC

Mwenyekiti mstaafu wa klabu ya waandishi wa habari wa Pemba ‘PPC’ Said Mohamed Ali anasema, PPC iliundwa kwa kuwaunganisha waandishi kwani kwa wakati huo hakukua na chombo kiichowaunganisha.

PPC ni miongoni mwa klabu kongwe za waandishi wa habari ambazo zinatoa fursa za kuwapa mafunzo waandishi kupitia miradi mikubwa.

“Chanzo cha kuanzishwa kwa eneo la wafanyabiashara juakali mjini chake chake ni ‘PPC ‘tuliwakusanya kutoka sehemu tofauti, kushirikiana na BBC kuandika habari za vijijini ambazo ziliibua changamoto nyingi na kuwawezesha wananchi kupaza sauti kueleza kero zao,” anaeleza.



PPC ilitoa mchango wake mkubwa wa kuwepo kwa chuo cha habari Pemba, ambao walipata mafunzo ya ngazi ya cheti na diploma.

Aliwataka waandishi wa habari wafanye kazi kwa kujituma wao wenyewe na waache tabia ya kusubiri kupangiwa kazi, wajiamini, waache kushabikia siasa na pia wakumbuke wajibu wao kwa jamii.

Mjumbe wa kamati tendaji wa klabu ya waandishi wa habari Pemba (PPC) anaewakilisha kundi la vijana Gasper Chales anasema, klabu hiyo ina faida nyingi ikiwemo kujenga uwezo kwa wandishi kwa kutoa taaluma.

Kwa Pemba waandishi wa habari wengi ni vijana ukizingatia wana mahitaji yao mengi ikiwemo muendelezo wa kukuzwa kielimu.

“Kama kijana kazi ambazo tunazifanya ni kupeleka mawazo na kushauri kuwepo kwa miradi ambayo itatunufaisha sisi waandishi vijana kwani tunahitaji kuendelea kujifunza hiyo ndio kazi yangu kubwa,” anasema.

WANACHAMA

Mwandishi wa habari wa shirika la Magazeti ya serikali Pemba, Habiba Zarali Rukuni ni mwanachama wa Pemba Press klab anasema, klabu hiyo ina mchango kumbwa kwa waandishi wa habari kutokana na fursa wanazozipata.

‘’PPC imetunufaisha sana, moja ni kutuunganisha waandishi wa habari kuwa kitu kimoja pamoja kutupatia mafunzo ya ndani na nje ya Pemba,’’ anasema.

Meneja wa ZENJ FM Pemba Is-haka Mohamed Rubea anasema, PPC imewanufaisha kupata mafunzo ambayo hawakuweza na hata kutarajia kuyapata katika taasisi wanazozifanyia kazi.

‘’Klabu hii ni muhimu kwa waandishi wa habari, inatusaidia kuongeza ujuzi na maslahi yetu waandishi wa habari, tumepata sehemu ya kuwasilisha malalamiko yetu tunapopata changamoto,’’ anasema.


Mwandishi wa habari wa kituo cha Swahiba FM, Fatma Hamad Faki anasema, klabu hiyo ni muhimu imewasaidia waandishi wa habari waliowengi wamepata fursa za kuongeza taaluma za juu za kimasomo.

                                      MWISHO.

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch