Skip to main content

JACKLIE "INTERNEWS KUENDELEA KUWANOA WAANDISHI TANZANIA"

                                                   



 NA HAJI NASSOR, PEMBA

MKUU wa mradi jumuishi wa vyombo vya habari kanda ya Afrika kutoka shirika la kuwajengea uwezo waandishi wa habari Jacklie Jidubwi, amesema shirika hilo litaendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kuwa waledi kwa kuibua maumivu yanayowakumba watu wenye ulemavu chini.
Mkuu huyo wa mradi aliyasema hayo machi 8, mwaka 2022 mjini Zanzibar wakati akiyaghairisha mafunzo ya siku2 kwa wanahabari wa Zanzibar juu ya uandishi bora wa habari za watu wenye ulemavu kupitia mradi wa jumuishi wa vyombo vya habari.
Alisema Internews imevutiwa mno na kazi na mwamko walionao waandishi wa habari wa Tanzania wakiwemo wa Zanzibar kwa kuibua changamoto na madhila yanayowasakili watu wenye ulemavu.
Alieleza kuwa kwa juhudi hizo za wazi wazi ndio maana shirika hilo limevutiwa na kazi hizo na kuahidi kuendelea kufanyakazi na vyombo vya habari.
"Kwa hakika Internews tumevutiwa mno kuona mradi huu unatekelezwa katika nchi kadhaa lakini kwa Tanzania mmezalisha habari 376 kwa kipindi kifupi na baadhi yao kuzaa matunda kwa watu wenye ulemavu," alisema.
Katika hatua nyingine Jacklie amewataka waandishi waliopatiwa mafunzo hayo kuendelea kuyafanyiakazi na sio tu kwa kuandika mabaya pekee kwa kundi la watu wenye ulemavu.
Mkuu wa program kutoka Internews Tanzania Shaaban Maganga alisema moja ya jukumu la lazima kwa mwandishi wa habari ni kuyafikia makundi yote katika utendendaji wa kazi zao.
Alieleza kuwa Internews imeona umuhimu wa kuwaunga nguvu waandishi hao na vyombo vyao ili kujikwamua kwa pale wanapokwa kiutendaji.
"Wapo baadhi yenu wameshapata hata kuungwa mkono kifedha na wengine watapewa ili sasa kufika huko ambako hamfiki katika kuwaandikia watu wenye ulemavu" alifafanua.
Nae mtendaji Temigunga Mahondo alisema ni vyema waandishi wa habari wakazingatia maadili ya kazi zao ili habari na vipindi wanavyofanya visiwaumize watu wenye ulemavu .
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar Mwalimu Ussi Khamis amesema baada kubaini uwepo wa chagamoto wanadhamiria kuifanyia mapitio sheria ya watu wenye ulemavu haki na fura nambari 9 ya mwaka 2006
Alisema kwa mfano vipo vifungu havina maelezo ya kutosha na wala havitaji adhabu ikiwa tasisi ya umma imejenga jengo lisilorafiki kwa wa watu wenye ulemavu.
Mwandishi Rahma Suleiman wa gazeti la Nipashe alisema mafunzo hayo yamemzindua katika kazi zake.
Nae mwandishi wa redio jamii Mkoani Amina Massoud Jabir alisema mafunzo hayo yamemjenga zaidi hasa katika utengenezaji wa vipindi.
Fatma Hamad Faki wa pembayaleo blog na Amour Khamis wa Zanzibar cable walisema wamefanikiwa mno katika kazi zao baada ya kupata mafunzo ya awali.
Awali mafunzo hayo yalifunguliwa na aliyekuwa waziri katika ofisi ya Makamu wa kwanza za wa rais Zanzibar na sasa waziri wa fedha dk. Saada Mkuya Salum.
MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch