Skip to main content

Polisi waua watuhumiwa watatu Kibiti

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewaua kwa kuwapiga risasi watuhumiwa watatu wa ujambazi, lilipokuwa katika doria ya kuwasaka watu wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji ya Kibiti mkoani Pwani.
Polisi wamesema baada ya kuwapekuwa, watuhumiwa hao walikutwa na mabomu saba, SMG moja ikiwa imefutwa namba zake na ‘magazine’ moja ndani yake ikiwa na risasi 16, maganda 10 ya SMG na pikipiki aina ya Fekon.
Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, aliwaambia waandishi wa habari jijini jana kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa Jumatatu maeneo ya Msongola wilayani Ilala.
Mambosasa alisema askari wake wakiwa katika doria ya kusaka watuhumiwa wa mauaji ya Kibiti, walitilia shaka pikipiki iliyokuwa imebeba watu watatu ikiwa haina namba.
“Polisi walianza kuifuatilia na walipogundua kuwa wanafuatiliwa waliongeza mwendo na kukatisha njia kuingia barabara ya vumbi na walianza kufyatua risasi na polisi walijibu mashambulizi na kuwajeruhi,” alisema.
Kamanda Mambosasa alisema baada ya watuhumiwa hao kupigwa risasi walianguka na pikipiki yao.
“Katika upekuzi, watu hao walikutwa na silaha aina ya SMG moja ikiwa imefutwa namba zake na magazine moja ikiwa na risasi 16, maganda 10 ya SMG, mabomu aina ya Graned saba na pikipiki moja aina ya Fekon,” alisema Kamanda Mambosasa.
Aliongeza kuwa watu hao ambao wanakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 40 hawakutambuliwa majina yao na juhudi za kuusaka mtandao waliokuwa wakishirikiana nao zinaendelea.
Alisema watuhumiwa hao walipofikishwa Hospitali ya Temeke, daktari wa zamu siku hiyo alithibitisha walikuwa wameshafariki dunia na miili yao imehifadhiwa hospitalini hapo.
Katika tukio lingine, Kamanda Mambosasa alisema wamewaua watuhumiwa wengine wawili wa ujambazi eneo la Kibonde Maji, Mbagala Zakheim jijini Dar es Salaam.
Alisema watuhumiwa hao waliuawa Jumamosi usiku wakati askari wakiwa katika doria na kupata taarifa kuwa kuna majambazi wamepanga kupora katika maduka ya M-Pesa na Tigo-Pesa.
“Polisi walifika mapema na kuweka mtego wao ndipo ilipofika saa mbili usiku watuhumiwa walikuja na pikipiki moja ikiwa haina namba wakiwa wamebebana watatu,” alisema.
Kamanda Mambosasa aliongeza kuwa wawili kati yao walishuka na kumuacha mmoja kwenye pikipiki ambaye alidai ndiye aliyekuwa dereva wao.
Alisema askari walipowafuata ili wawakamate, dereva wa pikipiki alishtuka na kukimbia na mmoja wa majambazi alichomoa bastola na kufyatua risasi ndipo polisi walipojibu mapigo.
Alisema polisi waliwashambulia kwa risasi na kuwajeruhi watuhumiwa wawili ambao baada ya upekuzi walikutwa na bastola ikiwa na magazine yake na risasi moja na maganda matano ya risasi.
Alisema silaha hiyo ilikuwa imepakwa rangi nyeusi ili kuficha utambuzi wa aina ya silaha hiyo, lakini uchunguzi umebaini kuwa ni bastola aina ya CZ ambayo imefutwa namba zake.
Alisema watu hao walifariki dunia na miili yao imehifadhiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ikisubiri kutambuliwa.
Kamanda Mambosasa pia alisema wanawashikilia watu tisa akiwamo raia wa Yemen ambao wanadaiwa kujihusisha na vitendo mbalimbali vya uhalifu.
Alisema watuhumiwa hao walikamatwa maeneo ya Magomeni Mikumi baada ya kupokea taarifa ya kuwapo kwa mtandao huo.
Alisema watuhumiwa hao walikutwa na magari mawili wanayodaiwa kuwa ni ya wizi, mirungi bunda sita, simu 100, kompyuta mpakato tatu huku mmoja wao akibainika ni mhamiaji haramu.
Kamanda Mambosasa alisema watuhumiwa hao walikutwa na magari mawili yanayohisiwa kuwa ni ya wizi na ndani ya magari hayo kulikutwa na namba za bandia ambazo ni T 937 DJE aina Toyota IST rangi ya bluu bahari na T 774 DHY ambazo gari lake halikufahamika.
Alisema ndani ya gari hilo kulikutwa simu 100, kompyuta mpakato tatu na nyaya mbalimbali na kwamba gari jingine lilikutwa na namba za bandia ambazo ni T 375 CQP aina ya Toyota Vits rangi ya fedha.
Kamanda Mambosasa alisema katika mahojiano na watuhumiwa hao, ilibainika mmoja wao aitwaye Osman Ahmed (25) ni raia wa Yemen ambaye anaishi nchini bila kibali.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch