Skip to main content

WATUMISHI WAPYA WIZARA YA ELIMU PEMBA WAPEWA NENO




NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WATUMISHI  wapya wa  wizara ya elimu na mafunzo ya Amali Pemba, wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni za utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji katika utendaji wao.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu Idara ya uratibu na Utumishi kutoka wizra ya elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar Harith Bakari Ali, wakati akifungua mafunzo ya kuthibitishwa kazi kwa waajiriwa wapya yaliofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Michakaini Chake chake Pemba.

Alisema ufanisi wa kazi hutokana na kufuatwa ipasavyo kwa Sheria, miiko na maadili ya kazi ambayo humtengeneza mtumishi kua muawajibikaji katika utendaji wake wa kila siku ndani na nje ya eneo la kazi.

"Sheria,  maadili,  kanuni na miiko ya kazi ndio kichocheo muhimu cha uwajibikaji kwa mtumishi wa Umma, hivyo ni muhimu kuyazingatia yote haya ili kufanya kazi zenu vizuri na si katikamaeneoyakazi tu bali hata nje ya kazi, alieleza.

Alisema kua  kipengele chengine muhimu ni uzalendo katika kazi, ambayo  ni nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya msingi ya mfanya kazi, na elimu pekee si kigezo cha ufanyaji kazi  bora wa mtu,  bali uzalendo ndio msingi mkuu wa kufikia uwajibikaji.

Alieleza kua uzalendo humjenga mtumishi kuwepo kazini mda wote wa kazi pamoja na kufanya  kazi  kulingana taratibu zilizopo, jambo linalochochea upatikanaji wa huduma bora kwa jamii.

Alisema maendeleo ya elimu nchini yamefikiwa kutokana na uzalendo na uwajibikaji wa wafanya kazi wa wizara wakiwemo waalimu, ambao wanafanya kazi kubwa katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku katika kuwasimamia vyema wanafunzi wao.




Aidha alitoa wito kwa watumishi hao kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo uvunjifu wa kanuni na sheria za utumishi wa Umma, kwa kufanyia kazi yale yote waliosomeshwa ili lengo la utoaji huduma bora kwa jamii liweze kufanikiwa.

"Mafanikio ya elimu  tulionayo Zanzibar yamechochewa na uzalendo walionao wafanyakazi wa wizara wakiwemo waalimu, hivyo  ni muhimu na nyinyi kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo haya kwa kujiepusha na uvunjifu wa kanuni na sheria za utumishi wa Umma", alieleza.

Kwa upande wake Msaidizi Mkuu wa Chuo Cha Utawala wa Umma IPA tawi la Pemba Nuhu Abuubakar Ali lengo la kuwepo kwa watumishi wa Umma katika serikali ni kupambana na kuleta maendeleo endelevu kwa kutatua changamoto zilizomo katika jamii, hivyo aliwasihi watumishi hao kua ni sehemu ya mapambano hayo.



Aidha aliwataka watumishi hao watekeleze majukumu yao kama sheria kanuni zinavyoelekeza bila kujali ubaguzi ili kukuza ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla.

Nae Afisa elimu kutoka Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi (ZAECA)Mkoa wa Kusini Pemba Badria Salim Ali aliwataka watumishi hao kutoa huduma kwa misingi ya haki na usawa pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa na uhujumu uchumi,  kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Nao washiriki wa mafunzo hayo walisema mafunzo hayo yanawasaidia katika utendaji wao wa kazi wa kila siku na kuahidi kufanyia kazi  kwa maslahi mapana ya jamii na taifa.

Mafunzo hayo ya siku mbili yanayoyotewa kwa wafanyakazi wapya wa wizara ya elimu yameandaliwa na Wizara ya Elimu na mafunzo ya Amali Pemba kwa kushirikiana na Chuo Cha Utawala wa Umma IPA,  ikiwa ni sehemu ya kuwaongezea uwezo waajiriwa wapya katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.



                                                           MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...