Skip to main content

Mkurugenzi TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia

 




Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar.

“Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio nguzo kuu ya TAMWA–Zanzibar,” alisema.

Alisema kuwa katika kipindi cha kuwa mtendaji mkuu wa Tamwa Zanzibar alifarijika sana na waandishi wa habari kutokana na kutumia vyema kalamu na vipaaza sauti katika kueleza changamoto za kijamii hususan masuala ya haki za binaadamu pamoja na vitendo vya udhalilishaji vya wanawake na watoto.

“kalamu za waandishi ilikuwa ndio nguzo kuu ya kutegemea katika kipindi cha uongozi wangu nikiwa mkurugenzi kalamu zilipaaza sauti za wasio na sauti pamoja na kueleza changamoto za kijamii hususan katika masuala ya ukiukwaji wa haki za binaadamu”, alifafanua mkurugenzi.

Akieleza kuwa mashirikaino hayo ya karibu yameweza kwa kiasi kikubwa kusaidia jamii na kupungua changamoto za wanawake na watoto pamoja na makundi mengine ya pembezoni kama walemavu na wazee.

“Nguvu yetu ilikuwa ni ya waandishi wa habari tukiamini kuwa nguvu ya habari inaweza kuleta mabadiliko chanya katika jamii lakini pia kuibua kero za wananchi pamoja na kuizundua serikali” alisisitiza.

Kupitia miradi mbalimbali, TAMWA–ZNZ imefanikiwa kuwafikia zaidi ya wanawake na watu wenye ulemavu 11,120 kupitia vikundi 572 vya kuweka na kukopa, kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, na kuchangia mabadiliko ya sheria muhimu ikiwemo Sheria ya Ushahidi, Sheria ya Mahakama ya Kadhi na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Leo, TAMWA–Zanzibar ina wanachama 82 waandishi wa habari kutoka Unguja na Pemba, wafanyakazi 23 wenye weledi, mifumo imara ya kifedha inayoendeshwa na wahasibu wenye ithibati ya CPA, pamoja na ukaguzi wa hesabu unaofanywa na kampuni zilizosajiliwa kitaifa. Taasisi hiyo pia inamiliki majengo yake yenyewe ambayo yameanza kuchangia mapato ya ndani.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi huyo alitangaza rasmi kukabidhi majukumu kwa Bi. Nairat Abdulla Ali, aliyekuwa Meneja wa Programu, akimtaja kuwa kiongozi mwenye maadili, uwezo na maono thabiti ya kuiendeleza taasisi hiyo.

“Nawaomba wanachama, waandishi wa habari na wadau wote kumpa ushirikiano mkubwa. Taasisi imara haijengwi na mtu mmoja, bali hudumu pale uongozi unapobadilika na dira ikibaki ile ile,” alisema.

Katika hafla hiyo waandsihi wa habari waliohudhuria waliishukuru kwa dhati Tamwa Zanzibar kwa kuwa nao karibu pamoja na kuwajengea uwezo katika kuimarisha weledi na umahiri katika taaluma ya habari.

Khatib Suleiman kutoka Habari leo amesema kuwa Tamwa imetusaidi kutujengea uwezo hususan katika kuandika kwa weledi na kuimarisha uwezo wetu katika namna ya kuripoti masuala ya haki za wanawake na watoto pamoja na haki za binaadamu kwa ujumla.

“Tamwa Zanzibar imekuwa ni chuo katika kuimarisha taaluma ya uandishi na tumeweza kuandika kwa weledi na umahiri huku tukizingatia maadili ya wanahabari”, alifafanua.

Berema Suleiman kutoka Zenji Fm alisema kuwa tamwa Zanzibar imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha taaluma lakini pia katika kuwapatia mafunzo waandishi chipukizi katika kuimarisha utendaji wa kazi zao.

“Mafunzo tuliyoyapata yamesaidia katika kuimarisha taaluma na kutujengea uwezo hususan katika kufuatilia habari zetu pamoja na kuwa na vyanzo tofauti na kuwapa nafasi makundi ya wanawake na vijana pamoja na walemavu”, alifafanua.

Wafanyakazi wa tamwa Zanzibar walishukuru kwa uongozi wa Dk. Mzuri hususan katika kuimarisha utendaji wa kazi zao huku wakizingatia weledi na umahiri katika kuandika ripoti na pia kufanya kazi kwa kuweza kupata matokeo

Zaina Mzee Afisa mwandamizi wa Tamwa Zanzibar alisema kuwa ulipokuja kuongoza taasisi hii, hukurithi tu ofisi na majukumu, bali pia changamoto nyingi. Kwa busara, maono na uongozi wako thabiti, uliweza kuibadilisha taasisi yetu na kuifanya kuwa mfano wa uwajibikaji, mshikamano na utendaji bora. Chini ya uongozi wako, tulijifunza kuwa kazi si wajibu tu, bali ni wito na dhamana ya kulitumikia taifa kwa uadilifu.

Akitoa neno la shukurani mkurugenzi mpya wa Tamwa Zanzibar Nairat Abdulla amesema kuwa napokea dhamana hii nikiwa na ufahamu kwamba uongozi si kauli, bali ni vitendo; si ahadi, bali ni uwajibikaji. Ninapokea nafasi hii nikitambua kuwa taasisi huimarika si kwa mipango iliyoandikwa vizuri pekee, bali kwa utekelezaji thabiti, wenye nidhamu na mwelekeo unaofahamika.

Ninawaahidi kushirikiana nanyi kwa karibu, kusikiliza kwa makini, na kuchukua hatua kwa wakati. Milango yangu itakuwa wazi kwa hoja, mawazo na suluhisho, kwa sababu uongozi wa pamoja na mashirikiano ni muhimu katika kuimarisha kazi zetu, alisisitiza.

Hafla hiyo ilihitimishwa kwa kutoa zawadi mbali mbali kwa mkurugenzi aliyemalaiza muda Dk. Mzuri Issa ikiwa ni sehemu muhimu ya kutunza kumbukumbu ya utumishi wake uliotukuka.

End.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...