Skip to main content

HAKI YA ELIMU KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU, SERA, SHERIA, MIKATABA HAINA CHANGAMOTO LAKINI.....

  


NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

SERA ya Elimu ya Zanzibar, imetaja elimu mjumuisho, ili kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki sawa kama ilivyo wingine.

Sera hiyo ya mwaka 1991 ya Zanzibar, kipengele cha elimu ya watu wenye ulemavu, ibara 4.9 kimeainisha kuwa hakutokuwa na kikwazo wala sababu ya kumnyima haki yake hiyo.

Imezungumzia Wizara ya Elimu na tasisi husika, itashirikiana ili kuhakikisha elimu inatolewa kwa misingi bora kwa watu wote.

Hapa nayo Sheria ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (1), kimesisitiza haja kwa watu wenye ulemavu, kupewa haki zote za msingi za kibinaadamu sawa na watu wingine.

‘’Watoto wenye ulemavu na wasio na ulemavu wote watachanganywa, ili tu kupatiwa elimu bora,’’ilifafanua shehemu ya sheria hiyo.

Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa wenye ulemavu nambari 19 ya mwaka 2024, inaelezea waraka wa Baraza la                            Mawaziri kuwapa huduma bora kupitia serikali, mamlaka husika na tasisi binafsi. 

Nayo sheria ya mama ya nchi, katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 10 (f), kinasisitiza kuwa serikali, inawapa huduma za kutosha kwa watu wote, fursa za kielimu katika madaraja yote.



 Mkataba wa kimataifa wa haki za watu mwenye ulemavu mwaka 2006, ibara ya 24 imeeleza kuwa nchi wanachama zilizoridhia Mkataba huu, wanawajibu wakuhakikisha kuwa haki za watu wenye ulemavu zinasimamiwa ikiwemo elimu.

 ‘’ Mfumo wa elimu hauwatengi watu wenye ulemavu na kwamba watoto hao hawabaguliwi, kwenye elimu kuanzia ya msingi hadi sekondari kwa mfumo jumuishi,’’unafafanua mkataba huo.

Aidha mkataba huo wa mwaka 2006 ukaenda mbali zaidi, kwa kufafanua kuwa watu wenye ulemavu, wahakikishiwe kuwa wanapata usaidizi unaohitajika ndani ya mfumo wa elimu, ili kuwawezesha kuelimika.

 

WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

Hanifa Hemed Abdalla ni mwanafunzi anasoma skuli ya Michakaini darasa la nne, anasema ingawa skuli hiyo wapo walimu wenye uwezo wa kuwafundisha, bado skuli haijazingatia miundo mbinu.

Anasema skuli yao limekuwa kikwazo kwao ya kushindwa kufika madarasa ya juu, kwani hakuna usaidizi ‘lift’ wala kisaidizi chingine hapo.

‘’Skuli yetu bado imekuwa kikwazo, hatuwezi kufika juu ya ghorofa wala hakuna kisaidizi cha aina yoyote, tunaishia madarasa ya chini,’’anasema.

Nae Sumaiya Saleh Juma ambae ni mwanafunzi wa darasa la kwanza skuli hapo, mwenye ulemavu wa viungo, anasema skuli yao imekuwa na vifaa vya kufundishia kwa watu wenye ulemavu.

‘’Ndani ya skuli yetu kuna vifaa vya kutosha vya kufundishia mpaka vya kuchezea, tunavyo na vyoo maalumu, ingawa kikwazo ni kwa wale wenye ulemavu wa viungo kufika umbali wa jengo,’’ anasema.

WAZAZI



Asha Khamis Faki wa kijiji cha Bomani shehia ya Mchangamrima mwenye mtoto mlemavu, anasema kukosekana kwa miundo mbinu ya elimu mjumuisho skulini hapo, haikuwa kikwazo cha kumpeleka mtoto wake.

‘’Nafahamu kuwa skuli ya Jonwe, anayosoma mtoto wangu hakuna mpango jumuishi wa elimu, vifaa ingawa niliona nisimfungie ndani, ajumuike na wenzake katika kutafuta elimu iliyozungurukwa na changamoto,’’ anasema.

Nae mzazi Salama Haji Mohamed, anasema haki ya kupata elimu kwa mtoto wake mwenye ulemavu, alihisi iko mbali kwa kutokuwepo mpango elimu jumuishi skulini hapo, ingawa hilo hakuliangalia.

Anasema mtoto wake anaesoma darasa la pili, ni mithili ya mwamanafunzi anaewapeleka na kuwarudisha wenzake, kutokana na uwezo wa ufahamu wake kuwa mdogo ukichangiwa na miundo mbinu hafifu jumuishi.

‘’Anakwenda tu nakurudi kama anaewapeleka wenzake, lakini bora aende changamoto na misukosuko ya elimu yatamkuta akiwa darasani,’’anafafanua.

WAALIMU

Mwalimu mkuu wa skuli ya Michakaini Fatma Ali Khamis, anasema ndani ya skuli hiyo kuna wananfunzi tisa wa madarasa mjumuisho na 24 wa kitengo. 

Anasema wanafunzi wote hao hupewa elimu ya mjumuishi, pamoja kuwazingati kwa pamoja ili kuhakikisha wanapata haki yao ya elimu.          

Aziza Juma Salim ni mwalimu wa skuli ya Michakini anaesomesha wanafunzi wenye ulemavu, anasema hapo skuli ya Michakaini kipo kitengo maalum kwa wanafunzi wenye ulemavu wa akili, uoni, hata viungo.

‘’Changamoto kubwa ni jengo kumekuwa hakuna visaidizi hawawezi kufika umbali wa madarasa ya juu kwa wale wanaohitaji japo kwa kutembea,’’anasema.

Amekuwa akiwasomesha wanafunzi hao, kwa hatua ya kwanza mpaka pale atakapopata uelewa wa kutosha, humpeleka darasa la elimu mjumuisho, kwa yule ambaye anauwezo wa kufikia na ikiwa changamoto kwa kutoweza kufikia humuacha madarasa ya hapo chini.

Zulekha Ali Rashid ni mwalimu wa skuli ya Jonwe anasema darasani mwake, kuna wanafunzi wenye ulemavu amekuwa akiwasomesha kibubusa, kwa kutokuwepo miindumbinu jumuishi.



Anasema hana uelewa wala ujuzi wa kuwasomesha wanafunzi wenye ulemavu, maana skuli yao bado sera ya elimu hajafikiwa, hakuna vifaa vya kuwasomeshea wala mkalimani wa lungha ya alama.

‘’Kwakweli skuli yetu bado, maana hapana mahitaji ya wanafunzi hawa, nimekuwa nikiwasomesha tu kibubusa na kiishara mpaka nikafikia pale nilipokusudia,’’anasema.

Fatma Mabrouk Khamis ni mwalimu wa skuli ya Michakaini elimu mjumuishi anasema sera ya elimu imefikiwa kwa kiasi, wamepata mafunzo kutoka kwa walimu wenzao, ya kuwafundisha wanafunzi wenye ulemavu.

WIZARA YA ELIMU                          


                                                                                                                                                                                                       Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim anasema, wapo katika mikakati ya kuwasaida wanafunzi, katika skuli za elimu mjumuisho kwa kuwapatia mafunzo walimu wa ukalimani wa lugha za alama.

‘’Niwatoe hofu wanafunzi, waalimu na jamii, tupo katika mchakato wa kubadilisha sera ya elimu, ili iweze kunufaika kwa watu wote.

Waziri Ofisi ya Makamu Kwanza wa Rais Zanzibar Harusi Said Suleiman, amenukuliwa akisema kuwa, wapo waalimu 40, waliokwishapewa mafunzo ya lugha ya alama.

‘’Hizi ni moja ya juhudi za kuhakikisha wanafunzi wenye ulemvu, wanapata haki ya elimu, kama walivyowingine katika skuli zetu za Unguja na Pemba,’’anasema.

Anasema, juhudi nyingine zinazofanywa na serikali ni kufanya ziara katika majengo mbali mbali zikiwemo skuli, na yapo 22 yalishatembelewa, ili kubaini changamoto.

 

JUMUIA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Mashavu Juma Mabrouk ni Mratibu wa Baraza la watu wenye ulemavu, anasema jamii jumuishi ni watu wote wasaidiwe wenye ulemavu, kwa kila kitu kinachofanyika wajumuishwe kupitia skuli wanazosoma.

Wamekuwa wakishajiisha masuala ya miundombinu rafiki, majengo yawe na ramsi, vyoo jumuishi hata wakalimani wa lugha za alama, ni jambo la lazima.

Mkurugenzi Mtendaji shirikisho la watu wenye ulemavu Ali Machano, anasema ni kweli mifumo ya elimu haijazingatiwa, katika skuli za mjumuisho na majengo ya kisasa hayapo katika mazingira wezeshi kwa wanafunzi.

    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...