Skip to main content

BARAZA LIJALO LA MAWAZIRI WANAHARAKATI WATAMANI 50 KWA 50 IANZIE HAPO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@

NOVEMBA 1, mwaka huu Rais mteule wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alikula kiapo cha uaminifu cha kushika madaraka ya urais kwa awamu ya pili.

Sherehe hizo zilifanyika uwanja wa New Amani Complex, kuanzia majira ya saa 12: 00 asubuhi, huku umati wa wananchi wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, wakijitokeza.

Sherehe hizo, ni ishara ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, uliopigwa Oktoba 29, mwaka huu na wazanzibari laki 448, 832 kumpa kura za ushindi, ambayo ni sawa na asilimia 74.8.

Kisha, Rais huyo wa Zanzibar, alimteua Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Mwinyi Talib Haji, hapo ni sawa na kusema, anaanza kupanga safu yake ya awamu ya pili.

Pamoja na kumtea Makamu wa Pili wa rais akiwa ndie mtendaji mkuu wa serikali, bila shaka sasa zamu ya baraza la mawaziri linafuata.

WANAHARAKATI WANASEMAJE

Dk. Mzuri Issa Ali, ambae ni Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, anampa heko Dk. Mwinyi kwa ushindi huo.

Anasema, hilo linatokana na utendaji wake uliotukuka, kwa awamu ya miaka mitano ya kwanza, huku akisaidiwa kwa karibu na watendaji wake, wakiwemo wanawake.



‘Nakumbuka vyema kwenye wizara 16, wanawake walikabidhiwa majukumu kwenye wizara tano, jambo ambalo ni la kupongezwa,’’anasema.

Mkurugenzi anasema, kwa awamu saba zilizopita, awamu ya Dk. Mwinyi nayo, iliwaamsha wanawake, kwa kukabidhiwa madaraka makubwa, kwenye wizara tano.

Anakumbuka hata idadi ya wakuu wa wilaya wanawake, nayo iliongezeka, maana kati ya wilaya 11, wanawake walikuwa kwenye wilaya nne, ikiwemo ya Micheweni na Magharibi Unguja.

Tatu Abdalla Msellem Mwenyekiti wa Jumuia ya Tumaini Jipya Pemva ‘TUJIPE’, anasema Dk. Mwinyi, amekuja kuwainua wanawake kiungozi, na kuwaonyesha watu, kuwa wanaweza.

‘’Kwa mfano hata kisiwani Pemba, walikuwepo maafisa wadhamani wanawake watatu, jambo ambalo ni la kutia moyo,’’anasema.

Yeye anaona, hata idadi ndogo kiasi wanawake hawakuwa wakipewa nafasi za kuongoza, maana ilionekana kama vile, hawana uwezo.

Mohamed Hassan Abdalla, Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’, anasema, awamu ya Dk. Mwinyi, ilikuwa na manufaa kwa wanawake na uongozi.

‘’Mimi niliposikia amemteua Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Mhandisi Zena Ahmed Said, nilipiga saluti,’’anasema.


Kumbe nafasi hiyo, tokea yalipofanyika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ilikuwa haijawahi kukaliwa na mwanamke, hadi alipokuja Dk. Mwinyi.

Ama kweli hawakukosea wahenga, waliosema mgaa gaa na upwa, hali ugali mkavu, kama vile kugaa gaa ni kule, kupiga kelele kuwa wanawake wanaweza.

NINI WANASHAURI KWA BARAZA LA MAWAZIRI LIJALO

Wanaharakati akiwemo Kaimu Mratibu wa TAMWA-Pemba Amina Ahmed Mohamed, kwamba sasa wakati wa 50 kwa 50 kwenye safu ya baraza la mawaziri, ionekanake.

‘’Dk. Mwinyi ni kipenzi cha watu, ni mpenda kusikiliza ushauri na kuufanyia kazi, na hili sasa ni wakati aone mawaziri wanawake na wanaume, wanakuwa sawa,’’anashauri.

Halima Haji Msiu wa Chambani Mkoani, anasema ili safu yake ya uongozi ikae sawa, wakati wa kuzingatia wanawake kwenye baraza la mawiziri, ndio huu.

Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alinukuliwa akisema, wanawake wamepata fursa ya kipekee, ndani ya awamu ya nane.

‘’Na hili la kuweka idadi sawa ya wanawake na wanaume, kwenye baraza la mawaziri Dk. Mwinyi ni msikivu mno,’’anasema.

Mratibu wa baraza la taifa la watu wenye ulemavu, Mashavu Juma Mabrouk, anasema ni vyema kwa Dk.  Mwinyi, kuwazingatia wanawake na hasa wale wenye ulemavu.

‘’Walau kwa awamu iliyopita, alikuwepo Katibu Mkuu mwenye ulemavu tena mwanamke, ni vyema kwa baraza lijalo, wakaongezeka,’’anashauri.

Mwanafunzi wa kidato cha sita skuli ya Kiwani Mkoani Amina Haji Khamis, anasema wziara ikiongozwa na mwanamke, mara zote hufanya vizuri.

‘’Nani asieoona maendeleo ya sekta ya elimu, barabara na hata makaazi ni wizara ambazo kwa awamu iliyopita, zilikuwa zinaongozwa na wanawake,’’anasema.

Issa Haji Mohamed wa Wete, anasema hakuna kashfa wala kesi kutoka kwa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchaumi Zanzibar ‘ZAECA’, ikiihusisha wizara inayoongozwa na mwanamke.

‘’Wanawake wamekuwa watii, wachapakazi, mahodari, wabunifu na wasiotumia vibaya madaraka yao, hivyo ipo haja kwa baraza jipya lijalo la mawaziri, wakafia idadi sawa,’’anasema.

AWAMU YA NANE ILIYOPITA











Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alikuwa na wastani wa wizara 16, ikiwemo ya Elimu na Mfunzo ya Amali.



Wziara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, wizra ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Makaazi, Ardhi na Mejenzi pamoja na ile ya wanawake na watoto, ambazo ziliongozwa na wanawake.

Eneo jingine ni nfasi nyeti ya Katibu Mkuu Kiongozi na Katib wa Baraza la Mapinduzi, Katibu Mkuu ujenzi na mawasiliano ambazo zilishikwa na wanawake.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, mkuu wa wilaya ya Magharibi, Chake na Mkoani na maafisa wadhamini ikiwemo wa Ikulu na uwekezaji zilishikwa na wanawake kwa ujasiri.


NYARAKA ZA KISHERIA

Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na kisiasa wa mwaka 1976, ukitaja moja ya haki za kila mmoja ni kushiriki, uongozi bila ya ubaguzi, wakiwemo wanawake.

Tena hata mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake ‘CEDW’ wa mwaka 1979, ukasisitiza  Ibara ya 7, kwamba lazima hatua zichukuliwe, kuhakikisha wanawake wanakuwa na ushiriki sawa kwenye ulingo wa siasa.

 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 21(1), kinasisitiza kuwa, watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki bila ya ubaguzi, kupata haki mbele ya sheria.

                         Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...