Skip to main content

MAJAALIWA ASEMA HEMED ATOSHA KIWANI, AWAAHIDI WANANCHI AMANI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@

MJUMBE wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM taifa Majaaliwa Kassim Majaaliwa, amewataka wanachi wa Jimbo la Kiwani, kuwachagua wagombea wote wa CCM kwenye uchaguzi wa mkuu mwaka huu.

Alisema, kama wananchi wanataka maendeleo ya kweli, wagombea waliopitishwa ndani ya jimbo hilo wanatosha, kufikia maendeleo yao.

Majaaliwa aliyasema hayo leo Septemba 21, 2025, Kwareni Mwambe jimbo la Kiwani wilaya ya Mkoani, alipokuwa akiwanadi wagombea ubunge, uwakilishi na madiwani wa jimbo hilo, kuelekea uchaguzi mkuu, mwezi Oktoba mwaka huu.



Alieleza kuwa, tayari CCM imeshandaa mpango kazi wa miaka mitano ijayo, ambapo ndani yake eneo la Jimbo la Kiwani, limeshaelezwa vya kutosha.

Alieleza kuwa, huduma zote muhimu ikiwemo maji safi na salama, afya, barabara na uwezeshaji wananchi kiuchumi, limetajwa ndani ya mpango huo.

Alieleza kuwa, kila mmoja ajitokeze kupiga kura kwa amani, ingawa kura zao wahakikishe wanawapigia kura mbunge, mwakilishi wa madiwani wote wa Jimbo la Kiwani.



Aidha, Majaaliwa, aliwahakikisha wananchi wa Kiwani, kama ikiwa watawachagua wagombea wote wa Jimbo hilo, wataendelea kushirikiano nao kwa karibu.

Akimnadi mgombea Ubunge, wa Jimbo hilo Hija Hassan Hija, alisema ni kinara wa maendeleo, kwa historia yake.

Katika hatua nyingine, Mjumbe huyo wa Kamati kuu ya hamlashauri kuu ya CCM taifa Majaaliwa Kassim Majaaliwa, ambae pia ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungaano wa Tanzania, aliwahakikisha ulinzi na usalama wananchi wote.



Alisema, serikali imeshajipanga kuhakikisha hakuna uvunjifu wa amani, kuelekea uchaguzi mkuu, hivyo kila mmoja ashiriki bila ya hofu.

Alieleza kuwa, Tanzania unaoutamaduni wake wa kufanya shughuli zake kwa amani, kama ilivyo kwa chaguzi zilizopita.

‘’Niwahakikishe wananchi kuwa, ikifika siku ya kupiga kura Oktoba 29, nendeni kwa kujiamini, maana ulinzi utaimarishwa,’’alifafanua.

Nae Mgombea uwakilishi wa Jimbo hilo Hemed Suleiman Abdulla, amesema kama wakipata ridhaa, watakuwa watumishi wao na sio mabosi.



Alisema, Kiwani ijayo ndani ya miaka mitano, itakuwa ya mfano, kama wakipata ridhaa kutoka kwa wananchi hao.

Alieleza kuwa, kila mmoja abakie na chama chake, ingwa kura zao ikifika Oktoba 29, wahakikishe wanawapigia kura wagombea wenzake.

Alifafanua kuwa, wanampango wa kuendeleza miundombini ya elimu, ikiwemo ujenzi wa skuli ya sekondari nyingine, ili kuwapunguzia mafasa wanaokwenda skuli nyingine.

Alifafanua hayo, anayowaahidi sio utani kwani tayari wameshafanya utafiti wa kujua, changamoto zao za Jimbo la Kiwani.

‘’Kwa mfano wananchi wa wadi wa Kendwa wayanyohospitali kwa ajili ya huduma za mama na mtoto, lakini na wale wa Mwambe watajengewa yao,’’alifafanua.

Aliahidi kuwa, kijana yeyote anayetoka jimbo la Kiwani, kwenda kusoma elimu ya juu, watamfuatilia ili kumsaidia na asome kwa utulivu.



‘’Tukifanikiwa, kuingia madarakani mimi, Mbunge na madiwani tutahakikisha tunawafuatilia kihuduma na hatutombagua kijana kwa sababu ya chama cha wazazi wake,’’alifafanua.

Aidha aliwaomba wagombea wenzake, kuhakikisha wananadi sera za chama na sio matusi, na kuwataka wananchi wanaofanya kinyume wawanyime kura wagombea hao.

‘’Sisi tumeshajipanga na kuendelea kunadi sera zilizomo ndani ya Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030, na sio matusi wala viashiria ya uvunjifu wa amani,’’alifafanua.

Mapema Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa Hamad Hassan Chande, alisema sifa zote za kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani, mgombea uwakilishi huyo anazo.

‘’Maendeleo yaliopatikana katika taifa letu, yamesimamiwa kwa kiasi kikubwa na Hemed Suleiman Abdulla, hivyo anafaa kwa nafasi hiyo,’’alifafanua.

Nae mjumbe wa Halmshauri kuu ya CCM taifa Mohamed Aboud Mohamed, wakati akiwanadi wagombea hao, alisema wana sifa za kuwa viongozi ya kuwatumikia wananchi.

Alisema, mgombea uwakilishis Hemed Suleiman Abdulla, akiwa Makamu wa Pili wa rais, amesimia umoja, mshikamano na kufanikiwa kuwaunganisha wazanzibari.

Alieleza kuwa, Hemed ni hodari wa kazi zake, mwamifu, mtiifu, machapa kazi na aliyetayari wakati wote kuwatumikia wananchi.

‘’Na ndio maana utekelezaji uliofanikiwa wa Ilani ya ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025, unaoongozwa na Rais wa Zanzibar, hivyo Hemed ameshusika kwenye eneo hilo,’’alifafanua.

Kwa upande wa mgombea ubunge wa jimbo hilo, Hija Hassan Hija, alisema anamfahamu vyema, jinsi alivyokuwa akipigania maslahi ya wananchi wa Kiwani, hata alipokuwa chama chake cha awali.



Nae kada wa Chama cha Mapinduzi Hamza Hassan Juma, alisema Mgombea uwakilishi Hemed Suleiman Abdulla, anafaa kushika nafasi hiyo, baada ya kuonekana utendaji wake kwa nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar.

‘’Kwa hakika Mgombea uwakilishi wa Jimbo la Kiwani, hakuna mbadala maana ni mpenda maendeleo na asiyependa majungu, katika kazi,’’alifafanua.

Kada wa chama hicho Machano Othman Said, alisema Mgombea ubunge wa jimbo hilo la Kiwani Hija Hassan Hija, amekuwa king’ang’anizi mkubwa kwa jambo lenye maslahi.

Alisema, anakumbuka vyema wakati akifanya nae kazi, katika baraza la Wawakilishi, ambapo alikuwa hapindishi maneno, kwenye jambo lenye maslahi ya umma.

Mabunge mstaafu wa Jimbo la Kiwani Rashid Abdalla Rashid na Mwakilishi Mussa Foum Mussa, wamesema wananchi wa Kiwani wanayosababu ya kuwachagua wagombea  wa chama hicho kwa makubwa waliyofanya.

Walisema, mgombea uwakilishi Hemed Suleiman Abdulla, ndie aliyemshauri Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, jimbo hilo kuwa huduma zote za kibinaadamu.



Walisema wanalo tenki la kuhifadhia maji safi na salama lenye ujazo wa lita milioni 1, vituo vya afya vyenye hadi ya huduma za juu pamoja na ujenzi wa skuli tatu za ghorofa.

‘’Kwa mfano katika skuli hizo tatu za ghorofa, zimesababisha kuwepo wa vyumba 103 vya kusomea na kuondoa mikondo mitatu, kwa wanafunzi,’’alifafanua.

                        mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...