NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmshauri kuu ya CCM taifa Khamis Hamza
Chilo, amesema wateule waliopewa ridhaa na chama hicho, wanatosha kulibadili
jimbo la Mtambile kimaendeleo.
Chilo,
aliyasema hayo Septemba 27, 2025 uwanja wa mpira Kengeja jimbo la Mtambile,
wilaya ya Mkoani, kwenye uzinduzi wa kampeni kwa nafasi ya ubunge, uwakilishi
na udiwani wa jimbo hilo.
Amesema,
CCM haijawi kufanya kosa katika kuteua wagombea, iwe ngazi ya udiwani, uwakilishi,
ubunge na urais, kwani huwa tayari wameshaandaliwa kiutumishi.
Alieleza
kuwa, wananchi wa Jimbo la Mtambile, wahakikishe kura zao ikifikapo Oktoba 29
mwaka huu, wanawapa kura za ndio wagombea hao, ili kuja kuwalipa maendeleo.
Chilo
alifahamisha kuwa, wagombea wote hawana shaka, na suala la kushirikiana na wananchi,
katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030.
‘’Mimi
nawahidi wananchi wa Jimbo la Mtambile kuwa, wagombea mlioletewa sio maji taka,
ni wapambanaji, wapiganaji na wenye uchu wa maendeleo,’’alifafanua.
Aidha
Chilo, aliwakumbusha wananchi hao wa Jimbo la Mtambile kuwa, ili wagombea hao
watekeleza vyema Ilani ya CCM, wawape kura wagombea urais wa Zanzibar na wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Aidha
alisema, tayari CCM imeshatekeleza mambo kadhaa ndani ya Jimbo la Mtambile,
ikiwemo ujenzi wa soko, hospitali ya kisasa na barabara kadhaa za ndani.
Alifahamisha
kuwa, CCM imekuwa ikiyatekeleza hayo kwa nia thabiti, ya kuhakikisha inazidi
kuwapa neema bila ya ubaguzi wowote wananchi.
‘’CCM
imeshatekeleza miradia kadhaa ya kimkakati ikiwemo ujenzi ambao umeshaanza wa
uwanja wa ndege, bandari ya Shumba, upanuzi wa bandari ya Mkoani pamoja na
hospitali za rufaa,’’alifafanua.
Akiwanadi
wagombea hao, alisema mgombea Mwakilishi Ali Suleiman Juma, ana sifa za
utumishi na anamfahamu vyema, hasa kwa usikivu wake.
Kuhusu
mgombea Ubunge Mohamed Abdalla Kassim, anasema ni mtu sahihi kwa wakati huu sahihi,
kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Awali
Katibu wa CCM mkoa wa kusini Pemba Kajoro Vyohoroka, aliwapokea wanachama kadhaa,
kwa niaba yao 10, kutoka chama cha ACT-Wazalendo jimbo la Mtambile.
Akizungumza
kwa niaba ya wenzake, mwanachama huyo Seif Khalfan ‘mkongwe seif’
alisema waliamua kutoka, huko baada ya kuona chama cha ACT-Wazalendo kukosa
mwelekeo.
Mapema
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mkoani Ali Juma Nassor, alisema chama hicho, hakina
sera za porojo na ubishi, bali ni nidhamu na heshima kwa watu wote.
Aidha,
aliwaomba wananchi wa kukumbuka kuwa, ahadi zilizoahidiwa kwa miaka mitano iliyopita,
CCM imevuuka lengo, na kuwaomba tena kuwapa ridhaa tena.
‘’Kwanini
tunaomba muwachaguwe wagombea wa CCM, maana tulishatekeleza ahadi kwa miaka
mitano iliyopita, tupeni tena ridhaa tuendeleze na kuanzisha mingine,’’alifafanua.
Nae
mbunge mteule kwa nafasi ya vijana kanda ya Pemba, Zainab Abdalla Issa,
aliwaomba wananchi hao, kura zao, wasijewakazipoteza kwa kuvipa vyama visivyo
na dira.
‘’Wagombea
waliomo ndani ya CCM na wenye hadhi na haiba na wale wa vyama vingine, ni wapita
njia na msibabaike nao,’’alisema.
Aliongeza
kuwa, akishirikiana na viongozi wa jimbo hilo, watahakikisha kila kijana anakuwa
na usafiri wa kazi wa piki piki, pamoja na kuwepo kwa miradi mkakati.
‘’Kwanini
vijana na mama mtilie, wapite wakilalamika juu ya namna ya kujiwezesha, wapeni
kura wagombea wote wa CCM, waliomo ndani ya Jimbo la Mtimbile,’’alifafanua.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na uslama ya wilaya ya Mkoani Miza
Hassan Faki, amewakumbusha wananchi, kutokubali kushawisha kuvuruga amani, iliyopo.
‘’Wananchi
wote washiriki kupiga kura kwa amani na utulivu, na mkimaliza mrudi nyumbani,
kuendelea na shughuli zenu, msikubali kuzilinda kura, vipo vyombo maalum,’’alifafanua.
Mgombea
Ubunge wa Jimbo la Mtambile Mohamed Abdalla Kassim, amesema ameamua kugombea
nafasi hiyo, ili kulibalisha jimbo.
Alieleza
kuwa, vijana na wananchi wingine, akipata ridhaa hawatojuta, maana ana hamu
kubwa ya kuhakikisha, anawafariji.
‘’Kupitia
Ilani hii ya CCM ya miaka mitano ijayo, mnaweza kutulaumu ikimalizika, kama
hatujafanikiwa kuwaletea maendeleo, kama yalivyoahidiwa,’’alisema.
Kwa
upande wake Mgombea uwakilishi wa jimbo hilo, Ali Suleimana Juma, amesema nia
yake ni kuona, jimbo hilo linang’ara kimaendeleo.
‘’Kama niliaminiwa kuongoza wilaya na mkoa, siwezi kushindwa kuongoza Jimbo la Mtambile, maana miundombinu ipo ikiwemo Ilani ya CCM,’’alifafanua.
Uzinduzi
huo wa kampeni, uliambatana na shamra shamra za wasanii kadhaa, akiwemo Mboso,
Mashauzi na wasanii wingine.
Mwisho
Comments
Post a Comment