Skip to main content

CHILO: WAGOMBEA CCM MTAMBILE KULIBADILI JIMBO

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmshauri kuu ya CCM taifa Khamis Hamza Chilo, amesema wateule waliopewa ridhaa na chama hicho, wanatosha kulibadili jimbo la Mtambile kimaendeleo.

Chilo, aliyasema hayo Septemba 27, 2025 uwanja wa mpira Kengeja jimbo la Mtambile, wilaya ya Mkoani, kwenye uzinduzi wa kampeni kwa nafasi ya ubunge, uwakilishi na udiwani wa jimbo hilo.

Amesema, CCM haijawi kufanya kosa katika kuteua wagombea, iwe ngazi ya udiwani, uwakilishi, ubunge na urais, kwani huwa tayari wameshaandaliwa kiutumishi.



Alieleza kuwa, wananchi wa Jimbo la Mtambile, wahakikishe kura zao ikifikapo Oktoba 29 mwaka huu, wanawapa kura za ndio wagombea hao, ili kuja kuwalipa maendeleo.

Chilo alifahamisha kuwa, wagombea wote hawana shaka, na suala la kushirikiana na wananchi, katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2025/2030.

‘’Mimi nawahidi wananchi wa Jimbo la Mtambile kuwa, wagombea mlioletewa sio maji taka, ni wapambanaji, wapiganaji na wenye uchu wa maendeleo,’’alifafanua.

Aidha Chilo, aliwakumbusha wananchi hao wa Jimbo la Mtambile kuwa, ili wagombea hao watekeleza vyema Ilani ya CCM, wawape kura wagombea urais wa Zanzibar na wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha alisema, tayari CCM imeshatekeleza mambo kadhaa ndani ya Jimbo la Mtambile, ikiwemo ujenzi wa soko, hospitali ya kisasa na barabara kadhaa za ndani.

Alifahamisha kuwa, CCM imekuwa ikiyatekeleza hayo kwa nia thabiti, ya kuhakikisha inazidi kuwapa neema bila ya ubaguzi wowote wananchi.

‘’CCM imeshatekeleza miradia kadhaa ya kimkakati ikiwemo ujenzi ambao umeshaanza wa uwanja wa ndege, bandari ya Shumba, upanuzi wa bandari ya Mkoani pamoja na hospitali za rufaa,’’alifafanua.



Akiwanadi wagombea hao, alisema mgombea Mwakilishi Ali Suleiman Juma, ana sifa za utumishi na anamfahamu vyema, hasa kwa usikivu wake.

Kuhusu mgombea Ubunge Mohamed Abdalla Kassim, anasema ni mtu sahihi kwa wakati huu sahihi, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

Awali Katibu wa CCM mkoa wa kusini Pemba Kajoro Vyohoroka, aliwapokea wanachama kadhaa, kwa niaba yao 10, kutoka chama cha ACT-Wazalendo jimbo la Mtambile.



Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mwanachama huyo Seif Khalfan ‘mkongwe seif’ alisema waliamua kutoka, huko baada ya kuona chama cha ACT-Wazalendo kukosa mwelekeo.

Mapema Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mkoani Ali Juma Nassor, alisema chama hicho, hakina sera za porojo na ubishi, bali ni nidhamu na heshima kwa watu wote.

Aidha, aliwaomba wananchi wa kukumbuka kuwa, ahadi zilizoahidiwa kwa miaka mitano iliyopita, CCM imevuuka lengo, na kuwaomba tena kuwapa ridhaa tena.

‘’Kwanini tunaomba muwachaguwe wagombea wa CCM, maana tulishatekeleza ahadi kwa miaka mitano iliyopita, tupeni tena ridhaa tuendeleze na kuanzisha mingine,’’alifafanua.

Nae mbunge mteule kwa nafasi ya vijana kanda ya Pemba, Zainab Abdalla Issa, aliwaomba wananchi hao, kura zao, wasijewakazipoteza kwa kuvipa vyama visivyo na dira.



‘’Wagombea waliomo ndani ya CCM na wenye hadhi na haiba na wale wa vyama vingine, ni wapita njia na msibabaike nao,’’alisema.

Aliongeza kuwa, akishirikiana na viongozi wa jimbo hilo, watahakikisha kila kijana anakuwa na usafiri wa kazi wa piki piki, pamoja na kuwepo kwa miradi mkakati.

‘’Kwanini vijana na mama mtilie, wapite wakilalamika juu ya namna ya kujiwezesha, wapeni kura wagombea wote wa CCM, waliomo ndani ya Jimbo la Mtimbile,’’alifafanua.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na uslama ya wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, amewakumbusha wananchi, kutokubali kushawisha kuvuruga amani, iliyopo.

‘’Wananchi wote washiriki kupiga kura kwa amani na utulivu, na mkimaliza mrudi nyumbani, kuendelea na shughuli zenu, msikubali kuzilinda kura, vipo vyombo maalum,’’alifafanua.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtambile Mohamed Abdalla Kassim, amesema ameamua kugombea nafasi hiyo, ili kulibalisha jimbo.




Alieleza kuwa, vijana na wananchi wingine, akipata ridhaa hawatojuta, maana ana hamu kubwa ya kuhakikisha, anawafariji.

‘’Kupitia Ilani hii ya CCM ya miaka mitano ijayo, mnaweza kutulaumu ikimalizika, kama hatujafanikiwa kuwaletea maendeleo, kama yalivyoahidiwa,’’alisema.

Kwa upande wake Mgombea uwakilishi wa jimbo hilo, Ali Suleimana Juma, amesema nia yake ni kuona, jimbo hilo linang’ara kimaendeleo.





‘’Kama niliaminiwa kuongoza wilaya na mkoa, siwezi kushindwa kuongoza Jimbo la Mtambile, maana miundombinu ipo ikiwemo Ilani ya CCM,’’alifafanua.

Uzinduzi huo wa kampeni, uliambatana na shamra shamra za wasanii kadhaa, akiwemo Mboso, Mashauzi na wasanii wingine.

         Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...