Skip to main content

DK. MWINYI AKIWA MAKOMBENI AWAKUNA WANAOYASHUGHULIKIA MASHAMBA YA MIKARAFUU YA SERIKALI

 

 

     


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Oktoba mwaka huu, suala la kuhubiri amani na utulivu liwe ndio ajenda.

Mgombea huyo wa urais aliyasema hayo jana, uwanja wa mpira wa Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni kwa chama hicho, kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.

Alisema, haiwezekana kutekeleza jambo lolote pasi na kuhubiri amani na utulivu, maana ndio msingi wa kila jambo.

Alieleza kuwa, kama kuna mtu anadhani hilo sio jambo la msingi, sio vyema kuungwa mkono, kwani hakuna jambo ambalo linaweza kutekelezeka pasi na amani na utulivu.

‘’Kwanza niwambie kuwa tutaendelea, kuhubiri amani, mshikamano na umoja maa andio msingi mkuu wa kila kitu,’’alifafanua.

Aidha, Dk. Mwinyi alisema anakusudia kuwa Zanzibar kusiweko na skuli hata moja, ambayo wanafunzi wanaingia mikondo miwili, bali ni mkondo mmoja, ili wapate muda kwa kwenda madrassa.

Alisema, tayari hilo kwa mkoa wa kusini Unguja, limeshafanikiwa na kutamani kwa miaka mitano ijayo, iwe ni kwa Zanzibar nzima.

‘’Suala la mikondo miwili sitaki kulisikia, maana wanafunzi wamekuwa wakipata changamoto ya kuhudhuria madrasaa, ambapo miaka mitano ijayo hilo litafondoka,’’alisema.

Katika hatua nyingine Mgombea huyo wa urais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema anakusudia kuendelea kuifungua Pemba, kwa ujenzi wa barabara wa Chake chake-Mkoani itakayokuwa na njia nne.

Alisema, hakuna haja kwa wananchi wanapotaka kusafiri, kutoka mji mmoja kwenda mwingine, kutumia muda mrefu jambo, ambalo ambalo ni kupoteza muda wa uzalishaji.

Alisema, hakuna shaka kuwa muda mfupi ujao, hakutakuwa na barabara ya ndani ya Pemba, ambayo haitokuwa ya kiwango cha lami.

‘’Ili kuimarisha maisha ya wananchi, yapo mingi hutakiwa kufanywa, ikiwemo miundombinu ya usafiri wa anga, nchi kavu na baharini,’’alisema.

Aidha Dk. Mwinyi ambae ni Rais wa Zanzibar, aliwataka wananchi kuwapuuza wanaodai kuwa, serikali ya awamu ya nane haijafanya jambo, kwani wana ajenda yao binfasi.

 

Kuhusu ajira 300,000 alizoziahidia kwa miaka mitano iliyopita, alisema walifanikiwa kuzipata 217,500, ingawa kwa awamu ya nyingine ijayo, itakuwa ndio kipaumbele chake.

‘’Vijana msiwe na wasi wasi, nikipata ridhaa ya kuiongoza nchi, suala la ajira na kupanda kwa gharama za maisha, itakuwa ndio kipaumbele changu cha kwanza,’’alisisitiza.

Kuhusu, namna ambavyo atapambana na gharama za maisha, alisema kwa kuanzia, ni ujenzi wa matenki ya mafuta katika eneo la Wesha kwa Pemba na Mangwapwani kwa Unguja.

‘’Hiawezekani, mafuta yakiadimika siku moja, iwe ni changamoto kwa wananchi, tutakuwa na matenki ya kuhifadhia mafuta pamoja na maghala ya kuhifadhia chakula,’’alisema.



Wakati huo huo Mgombea huyo wa urais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema zao la karafuu linaendelea kuwanufaisha wakulima, kwa kupata asilimia 80, baada ya serikali kuliuza.

‘’Bado zao la karafuu tunaendelea kulienzi, na miaka mitano ijayo, litaendelea kunusuriwa kwa kuwepo la umwagiliaji na mikopo kwa wakulima,’’alifafanua.

Kuhusu mashamba ya mikarafuu, ambayo yalikua ya eka, sasa serikali imeshatangaaza, kuwapatia hati maalum ambazo zitakuwa na uwezo wa kuyarithi.

Kada wa chama cha mapinduzi Khamis Hamza Chilo, aliwataka wanaccm, kuachana na sera za maji taka, zinazotolewa na baadhi ya wagombea.

Alisema, wapo baadhi yao, wanapitapita, na kuwaeleza wananchi, kwamba serikali ya awamu ya nane haijafanya maendeleo, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Kwa mfano ukifika hospitali ya Mkoani, unaona nyumba za kisasa 74 za madaktari, achia mbali upanuzi wa bandari, na ujenzi wa barabara za ndani kwa kiwango cha lami,’’alisema.

Mapema Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, alisema kama kuna mtu analamikia kuwa serikali iliyopo madarakani sio halali, alishindwaje kukata rufaa.

Mapema Naibu Katibu mkuu wa CCM Zanzibar, Dimwa aliwaombea kura wabunge, wawakilishi na madiwani wa CCM, waliomo wilaya ya Mkoani.

Alisema, wagombea wote walioteuliwa na vikao vya juu vya chama, wanazosifa za utumishi na kuwaletea maendeleo wananchi.

‘’Niwaombee kura wagombea wote kuanzia, mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, na mwenzake wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, maana ukiichagua CCM, umechagua maendeleo,’’alisisitiza.

Kwa upande wake mgombea ubunge wa jimbo la Mkoani Prof: Makame Mnyaa Mbarawa, alimuahidi Dk. Mwinyi kumpa kumpa kura za ndio, kwa maendeleo ndani ya Mkoani.

Alisema tayari meli 24 kubwa zimeshafunga nanga bandarini hapo, pamoja na kushusha makontena 1,214 yenye bidhaa mbali mbali, tokea bandari hiyo ilipopanuliwa.

Aidha alisema, sababu nyingine wananachi kuwapa kura ni kutokana na ujenzi wa banda maalum, la kukaa abiria 1000 kwa wakati mmoja, ambapo ujenzi wake, unaendelea kwa kasi.

Jingine alisema ni ujenzi wa barabara ya Mbuguwani- Tironi, yenye urefu kilomita 3, na shilingi bilioni 6.31 zinaendelea kutumika, kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo.

‘’Kwa hakika Dk. Mwinyi umetufanyia mingi ndani ya Jimbo la Mkoani, maana na sasa ujenzi wa barabara ya Mkoani- Chake chake, utaanza wakati wowote, hongera sana kwa hili,’’alifafanua.

Nae Mgombea Uwakilishi wa Jimbio hilo, Khamis Hijazi, alisema tayari Dk. Mwinyi anaendelea na ujenzi wa soko la kisasa eneo la Mbuyuni, jambo ambalo, lilikuwa changamoto hapo awali.



Hivyo, amewakumbusha wananchi wa wilaya ya Mkoani, kutomnyima kura Dk. Mwinyi, ili aendeleze maendeleo anayoyakusudia.

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kiwani Hija Hassan Hija, alimuahidi Dk. Mwinyi, asiwe na wasi wasi, kura za wananchi wa jimbo hilo, ni zake.

Hivyo aliwaomba wananchi wa Zanzibar, kuwachagua wagombea wote wa CCM, kwani wana uchu wa maendeleo.

Nae mgombea uwakilishi wa jimbo hilo Hemed Suleiman Abdulla, amewataka wanaccm kuwajibu wapinzani, kwa kuwapigia kura, wagombea wote wa CCM.

‘’Haipendezi kuona mwanaccm, anaingia kwenye malumbano yanayoashiria uvunjifu wa amani, bali wajibuni kwa kisanduku cha kura,’’alifafanua.

Mapema Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kusini Pemba Yussuf Ali Juma, alisema kwa kuvuuka lengo la utekelezaji Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, ushindi wake utakuwa mapema mwaka huu .

         Mwisho

 

Comments