Skip to main content

DK. MWINYI AKIWA MAKOMBENI AWAKUNA WANAOYASHUGHULIKIA MASHAMBA YA MIKARAFUU YA SERIKALI

 

 

     


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Oktoba mwaka huu, suala la kuhubiri amani na utulivu liwe ndio ajenda.

Mgombea huyo wa urais aliyasema hayo jana, uwanja wa mpira wa Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni kwa chama hicho, kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.

Alisema, haiwezekana kutekeleza jambo lolote pasi na kuhubiri amani na utulivu, maana ndio msingi wa kila jambo.

Alieleza kuwa, kama kuna mtu anadhani hilo sio jambo la msingi, sio vyema kuungwa mkono, kwani hakuna jambo ambalo linaweza kutekelezeka pasi na amani na utulivu.

‘’Kwanza niwambie kuwa tutaendelea, kuhubiri amani, mshikamano na umoja maa andio msingi mkuu wa kila kitu,’’alifafanua.

Aidha, Dk. Mwinyi alisema anakusudia kuwa Zanzibar kusiweko na skuli hata moja, ambayo wanafunzi wanaingia mikondo miwili, bali ni mkondo mmoja, ili wapate muda kwa kwenda madrassa.

Alisema, tayari hilo kwa mkoa wa kusini Unguja, limeshafanikiwa na kutamani kwa miaka mitano ijayo, iwe ni kwa Zanzibar nzima.

‘’Suala la mikondo miwili sitaki kulisikia, maana wanafunzi wamekuwa wakipata changamoto ya kuhudhuria madrasaa, ambapo miaka mitano ijayo hilo litafondoka,’’alisema.

Katika hatua nyingine Mgombea huyo wa urais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema anakusudia kuendelea kuifungua Pemba, kwa ujenzi wa barabara wa Chake chake-Mkoani itakayokuwa na njia nne.

Alisema, hakuna haja kwa wananchi wanapotaka kusafiri, kutoka mji mmoja kwenda mwingine, kutumia muda mrefu jambo, ambalo ambalo ni kupoteza muda wa uzalishaji.

Alisema, hakuna shaka kuwa muda mfupi ujao, hakutakuwa na barabara ya ndani ya Pemba, ambayo haitokuwa ya kiwango cha lami.

‘’Ili kuimarisha maisha ya wananchi, yapo mingi hutakiwa kufanywa, ikiwemo miundombinu ya usafiri wa anga, nchi kavu na baharini,’’alisema.

Aidha Dk. Mwinyi ambae ni Rais wa Zanzibar, aliwataka wananchi kuwapuuza wanaodai kuwa, serikali ya awamu ya nane haijafanya jambo, kwani wana ajenda yao binfasi.

 

Kuhusu ajira 300,000 alizoziahidia kwa miaka mitano iliyopita, alisema walifanikiwa kuzipata 217,500, ingawa kwa awamu ya nyingine ijayo, itakuwa ndio kipaumbele chake.

‘’Vijana msiwe na wasi wasi, nikipata ridhaa ya kuiongoza nchi, suala la ajira na kupanda kwa gharama za maisha, itakuwa ndio kipaumbele changu cha kwanza,’’alisisitiza.

Kuhusu, namna ambavyo atapambana na gharama za maisha, alisema kwa kuanzia, ni ujenzi wa matenki ya mafuta katika eneo la Wesha kwa Pemba na Mangwapwani kwa Unguja.

‘’Hiawezekani, mafuta yakiadimika siku moja, iwe ni changamoto kwa wananchi, tutakuwa na matenki ya kuhifadhia mafuta pamoja na maghala ya kuhifadhia chakula,’’alisema.



Wakati huo huo Mgombea huyo wa urais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema zao la karafuu linaendelea kuwanufaisha wakulima, kwa kupata asilimia 80, baada ya serikali kuliuza.

‘’Bado zao la karafuu tunaendelea kulienzi, na miaka mitano ijayo, litaendelea kunusuriwa kwa kuwepo la umwagiliaji na mikopo kwa wakulima,’’alifafanua.

Kuhusu mashamba ya mikarafuu, ambayo yalikua ya eka, sasa serikali imeshatangaaza, kuwapatia hati maalum ambazo zitakuwa na uwezo wa kuyarithi.

Kada wa chama cha mapinduzi Khamis Hamza Chilo, aliwataka wanaccm, kuachana na sera za maji taka, zinazotolewa na baadhi ya wagombea.

Alisema, wapo baadhi yao, wanapitapita, na kuwaeleza wananchi, kwamba serikali ya awamu ya nane haijafanya maendeleo, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Kwa mfano ukifika hospitali ya Mkoani, unaona nyumba za kisasa 74 za madaktari, achia mbali upanuzi wa bandari, na ujenzi wa barabara za ndani kwa kiwango cha lami,’’alisema.

Mapema Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis, alisema kama kuna mtu analamikia kuwa serikali iliyopo madarakani sio halali, alishindwaje kukata rufaa.

Mapema Naibu Katibu mkuu wa CCM Zanzibar, Dimwa aliwaombea kura wabunge, wawakilishi na madiwani wa CCM, waliomo wilaya ya Mkoani.

Alisema, wagombea wote walioteuliwa na vikao vya juu vya chama, wanazosifa za utumishi na kuwaletea maendeleo wananchi.

‘’Niwaombee kura wagombea wote kuanzia, mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, na mwenzake wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, maana ukiichagua CCM, umechagua maendeleo,’’alisisitiza.

Kwa upande wake mgombea ubunge wa jimbo la Mkoani Prof: Makame Mnyaa Mbarawa, alimuahidi Dk. Mwinyi kumpa kumpa kura za ndio, kwa maendeleo ndani ya Mkoani.

Alisema tayari meli 24 kubwa zimeshafunga nanga bandarini hapo, pamoja na kushusha makontena 1,214 yenye bidhaa mbali mbali, tokea bandari hiyo ilipopanuliwa.

Aidha alisema, sababu nyingine wananachi kuwapa kura ni kutokana na ujenzi wa banda maalum, la kukaa abiria 1000 kwa wakati mmoja, ambapo ujenzi wake, unaendelea kwa kasi.

Jingine alisema ni ujenzi wa barabara ya Mbuguwani- Tironi, yenye urefu kilomita 3, na shilingi bilioni 6.31 zinaendelea kutumika, kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo.

‘’Kwa hakika Dk. Mwinyi umetufanyia mingi ndani ya Jimbo la Mkoani, maana na sasa ujenzi wa barabara ya Mkoani- Chake chake, utaanza wakati wowote, hongera sana kwa hili,’’alifafanua.

Nae Mgombea Uwakilishi wa Jimbio hilo, Khamis Hijazi, alisema tayari Dk. Mwinyi anaendelea na ujenzi wa soko la kisasa eneo la Mbuyuni, jambo ambalo, lilikuwa changamoto hapo awali.



Hivyo, amewakumbusha wananchi wa wilaya ya Mkoani, kutomnyima kura Dk. Mwinyi, ili aendeleze maendeleo anayoyakusudia.

Mgombea ubunge wa Jimbo la Kiwani Hija Hassan Hija, alimuahidi Dk. Mwinyi, asiwe na wasi wasi, kura za wananchi wa jimbo hilo, ni zake.

Hivyo aliwaomba wananchi wa Zanzibar, kuwachagua wagombea wote wa CCM, kwani wana uchu wa maendeleo.

Nae mgombea uwakilishi wa jimbo hilo Hemed Suleiman Abdulla, amewataka wanaccm kuwajibu wapinzani, kwa kuwapigia kura, wagombea wote wa CCM.

‘’Haipendezi kuona mwanaccm, anaingia kwenye malumbano yanayoashiria uvunjifu wa amani, bali wajibuni kwa kisanduku cha kura,’’alifafanua.

Mapema Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kusini Pemba Yussuf Ali Juma, alisema kwa kuvuuka lengo la utekelezaji Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, ushindi wake utakuwa mapema mwaka huu .

         Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...