Skip to main content

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI WANAWAKE WAMEJITOKEZA, VYAMA VIWATEUE.


                                                                                                   

 




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI WANAWAKE WAMEJITOKEZA, VYAMA VIWATEUE.TAREHE:                                                                                    27/07/2025. 

Wadau wa masuala ya wanawake na uongozi wanaviomba vyama vya siasa kuhakikisha kuwa vinawateua wanawake waliokidhi vigezo, kugombea nafasi za uongozi ndani ya vyama vyao kwenye uchaguzi wa ushindani ndani ya nafasi za uwakilishi, ubunge na udiwani. 

 Kwa muda mrefu wanawake wamekuwa nyuma katika siasa na kuelekezwa kugombea tu katika nafasi za viti maalum ambapo vinahusisha wanawake wenyewe kwa wenyewe na hivyo kutokuonesha uwezo wao halisi katika siasa za ushindani.  

Katika kipindi hiki ambacho vyama vya siasa mbali mbali viko katika mchakato wa chaguzi za ndani za vyama kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2025, wanawake wengi wamejitokeza katika siasa hizi za ushindani pamoja na kwamba bado ni kidogo kulinganisha na wenzao wanaume. 

Taarifa kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) zilizotolewa hivi karibuni kwa Zanzibar zinaeleza kuwa, jumla ya wanachama 1,640 wameweza kurejesha fomu kugombea nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani katika majimbo na wadi za uchaguzi Zanzibar, ambapo kati ya hao wanawake ni 406. 

Hii ni karibu asilimia 24.7 ya wagombea wote ndani ya chama hicho kikuu nchini. Kwa upande wa taarifa kutoka chama cha (ACT) Wazalendo iliyotolewa hivi karibuni imeeleza kuwa jumla ya wanachama 435 wamejitokeza kuchukua fomu kugombea nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani katika majimbo na wadi za uchaguzi Zanzibar. 

Taarifa hizo kutoka kwenye chama cha upinzani kikuu nchini kinaeleza kuwa kati ya hao wanawake ni 40 sawa na asilimia 9.2. 

Kwa pamoja vyama hivyo vinasubiri kamati maalum na kamati kuu za vyama vyao kupitisha rasmi idadi ya watia nia hao hasa wabunge na wawakilishi, michakato ambayo inategemewa kuanza mwishoni mwa mwezi huu na kumalizikia mwezi ujao.


Wadau wa masuala ya wanawake na uongozi wanawapongeza wanawake kwa ujasiri huo na kusisitiza kuwa hawapaswi kuishia kwenye hatua ya kuchukua fomu tu lakini wanastahili kupewa nafasi halisi ya kushindana majimboni. 

Katika uchaguzi uliopita wa 2020 Zanzibar ilipata wawakilishi wa nane tu katika Baraza la Wawakilishi sawa ana asilimia 16 na wabunge wanne sawa na asilimia 8 kupitia siasa hizi za kiushindani kwenye majimbo yake 50. 

Tunawashauri na kuwaomba wajumbe wa vikao vya uteuzi kuwapigia kura wanawake wakati wa mchakato wa kuwapata wagombea wa mwisho na kuwa sehemu muhimu ya mabadiliko katika kujenga Zanzibar njema inayofuata misingi ya heshima na usawa wa kijinsia. 

Kuwepo wanawake katika nafasi za uongozi ni dalili kubwa kuwa nchi inaweza kusonga mbele vizuri kimaendeleo ya kiuchumi, kijamii na kidemokrasia kwa vile tafiti nyingi ulimwenguni zimeonesha kuwa wanawake ni viongozi wanaoweka mbele zaidi maslahi ya familia na nchi pia ni waadilifu, wasikivu na wenye kujitoa na kujitolea zaidi.

 Mkataba wa Kimataifa wa Kuondoa Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) uliopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1979 katika kifungu cha pili kinahimiza kutetea haki za wanawake ambapo kinazitaka nchi wanachama ikiwemo Tanzania kuchukua hatua zote za kuzuia ukatili dhidi ya wanawake ikiwemo kuwa na michakato maalum ya kuongeza idadi ya wanawake katika vyombo vya maamuzi. 

Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa mashirikiano na Ubalozi wa Norway wanawahamasisha wanawake wote waliotia nia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, wasikatishwe tamaa na wendelee kuwa na nia njema ya uongozi kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

 Imetolewa na: JUWAUZA, PEGAO, ZAFELA na TAMWA ZNZ xxxxcxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...