Skip to main content

TIMU YA MPIRA WA PETE YA WANAWAKE MCHANGA MDOGO YATAKA LIGI

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ 

WACHEZAJI wa timu ya mchezo wa Pete ya Wanawake ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete, wamesema wanatamani kushiriki, ligi kuu ya mchezo huo, ili kukuza vipaji vyao.

Walisema, wameamua kuchagua kuanzisha timu ya mchezo huo, wakiamini kuwa wanaweza kusonga mbele kwenye eneo hilo kupitia ligi kuu ya Zanzibar, itayoanzishwa.

Hayo yameelezwa na wachezaji na viongozi wa klabu hiyo leo Machi 24, mwaka huu wakati wakizungumza na waandishi wa habari, kufuatilia tathmini ya mafanikio ya mradi wa ā€˜ā€™michezo kwa maendeleo,ā€™ā€™uliokuwa ukitekelezwa na TAMWA, ZAFELA na CYD.

Walisema, baada ya kupewa mafunzo na TAMWA ya umuhimu wa kushiriki kwenye michezo, kwa maendeleo wamehamasika kuanzisha timu ya mchezo wa pete.



Walisema, wanazotaarifa kuwa, kwa upande wa Pemba, mchezo huo haujawahi kuanzishiwa ligi kuu, iwe ngazi ya wilaya au mkoa, jambo linalotishia ndoto zao.

Mchezaji wa timu hiyo Zainab Rashid Said, amesema ni wakati sasa kwa viongozi kuhakikisha ligi ya mpira wa pete, unaingia kisiwani Pemba.

ā€˜ā€™Sera ya michezo ya mwaka 2018, inaelekeza michezo kwa wote, inahimiza kuimarisha miundombinu, ikiwemo kuwa na ligi maalum ambayo, itatuwezesha kuonesha vipaji vyetu,ā€™ā€™alieleza.

Nae mchezaji Amina Kudra Ali, alieleza kuwa ili michezo iwe kivutio kwa wanawake, lazima wawekezaji wajitokeza, ili iwe sababu ya kupata ajira kupitia sekta hiyo.

ā€˜ā€™Tumeamua kujiingiza kwenye mchezo wa pete, ingawa changamoto kubwa ni kutokuwepo kwa ligi maalum, ambayo ingekuwa kichechezo kwetu,ā€™ā€™alieleza.



Kwa upande wake, Katib wa klabu hiyo Bimkubwa Maulid Othman, alikiri kuwa, mafunzo waliopewa na TAMWA, yamewasaidia kukusanyana na kuanzisha klabu hiyo.

ā€˜ā€™Ni kweli timu hii imeasisiwa baada ya mafunzo ya michezo kwa wote, kutoka TAMWA, ingawa tokea zamani suala la uwepo wa ligi ni ngumu,ā€™ā€™alieleza.

Akizungumza namna ya kuielea timu hiyo, alisema wakati mwingine huomba kuingizwa kwenye mabonanza ya michezo, pamoja na kuanzisha mabonanza yao wenyewe.

ā€˜ā€™Kwa mfano mwaka jana, tulianzisha bonanza la shehia, na kucheza na timu mbali mbali, lakini yakimalizika timu inakosa motisha wa kuiendeleza,ā€™ā€™alieleza.

Hata hivyo alisema wamekuwa wakiwaomba viongozi wao wa Jimbo la Kojani, kuwaanzisha ligi maalum, kama ilivyo kwa mpira wa miguu, ingawa matokeo sio mazuri.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha net ball wilaya ya Wete Idrisaa Maulid Othman, alikiri kuwa kwa upande wa Pemba, hakujawahi kufanyika kwa ligi maalum, ya mpira wa pete.



ā€˜ā€™Fedha huwa ndio kikwazo, hata tunapowasiliana na viongozi wa juu, na hii ni changamoto ya kuukosesha nguvu na uhai mchezo huu,ā€™ā€™alifafanua.

Hata hivyo Makamu huyo Mwenyekiti wa CHANEZA wilaya ya Wete, amewataka wachezaji walioweka nia kwenye mchezo huo, kuendelea kufanya mazoezi, na kuahidi kuwaombea katika mabonanza mbali mbali.

Afisa Mawasiliano, kutoka TAMWA Zanzibar, Khairat Haji Ali, alisema kazi yao kubwa ni kuwahamasisha wanawake kuingia katika michezo.

Alisema, jamii haikuwa ikiwaangalia vizuri wanawake kwenye kukuza vipaji vyao, hivyo suala la kuanzishwa la ligi maalum, inaweza kufanya na mamlaka nyingine.

Hata hivyo alisema kupitia mradi huo, wanajivunia kwa timu ya Mchanga mdogo center, kuamua kujikusanya baada ya kupata mafunzo.



ā€˜ā€™Hata vifaa kama jezi na mpira, tukipata uwezo wa kifedha tutaziwezesha, ili ndoto zao zifikie mbali, kama ilivyo kwa wanamichezo wingine,ā€™ā€™alifafanua.

Hata hivyo, amewaomba viongozi kuwaunga mkono wanawake waliojiekeza kwenye michezo, kwani wana haki kama ilivyo kwa wanaume.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita, akisoma hutuba ya bajeti ya mwaka 2024/2025, alisema mradi wa uimarishaji wa viwanja vya michezo, unatekelezwa ndani ya programu ndogo ya uendeshaji na ukuzaji wa michezo.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2023/2024, wizara iliidhinishiwa kutumia shilingi mlioni 34.278 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbali mbali za ujenzi wa viwanja vya wilaya na ukarabati wa viwanja vya michezo.

Alisema mradi mwingine uliotekelezwa ni mradi wa ā€˜ā€˜Sports for Development in Africaā€™ā€™ ambao unafadhiliwa

na Shirika la Kimataifa la GIZ kutoka Ujerumani.

 

Mwaka 1978, Shirika la Umoja wa Mataifa, Sayansi na Utamaduni ā€˜UNESCOā€™ lilitoa tamko la kila mtu kupata fursa ya kufanya mazoezi na kucheza.

Hali ya ushiriki wa makundi yote katika baadhi ya michezo, haijawa ya kuridhisha ni kutokana na tathmini ya sera ya michezo iliyofanyika 2013, ambayo inaonesha asilimia 23 ya watu wote ndio wanaoshiriki michezo.

Sera ya Michezo ya Zanzibar ya mwaka 2018, ibara ya  3.5.1 imeelezea, serikali itahakikisha watu wote wanapata fursa ya kushiriki michezo, kwa kuwekewa miundombinu bora.

Aidha  sera hiyo ibara ya 3.5.2, imelezea kuwa, mkakati mwingine wa sera hiyo, ni kuandaa kampeni maalum  (mabonanza), zitakazowahamasisha watu wote wa rika zote na makundi yote kushiriki michezo.

Kifungu (d) ikafafaua kuwa, ni lazima kuwashajiisha wanawake kushiriki michezo na kuwawekea mazingira mazuri, ikiwemo viwanja, vifaa na mafunzo.

Aidha dira ya sera hiyo, imeeleza kuwa, ifikapo mwaka 2030, Zanzibar kuwa kitovu cha michezo kwa ubora wa maendeleo ya michezo kitaifa, kikanda na kimataifa.

Zanzibar ilianza michezo mwaka 1875 kufuatia ziara za manuwari za waengereza, wajerumani na zile kutoka Sweeden.

Michezo ilishika kasi zaidi kwenye miaka ya 1879 hadi 1898, na kabla ya vita vikuu vya dunia 1914 na 1918, baada ya vita vikuu vya dunia na miaka ya 1926 na 1942 wakati wa kipindi cha Ukoloni.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...