Skip to main content

KAMATI YA MAADILI YAPIGA MARUFUKU 'BEACH' YA WAMBAA KUGEUZWA 'GEST BUBU'

  

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KAMATI ya maadili na taaluma ya shehia za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, imepiga marufuku kufanyika vitendo viovu, vinavyofanywa na baadhi ya vijana, katika ya fukwe ya bandari ya Kwakitunga Wambaa.

Kamati hiyo imesema, wamebaini kuwa, kila ifikapo siku za sikukuu na mwishoni mwa wiki, wapo vijana, wengi wao kutoka nje ya shehia hizo, huitumia fukwe hiyo, kwa kufanya mambo machafu.

Akizungumza kwenye kongamano la malezi na maadili, lililofanyika Wambaa sokoni, Mjumbe wa kamati hiyo sheikhe Mahamoud Hussein, alisema hawakatai vijana kusherehekea sikukuu, bali wanachopiga marufuku ni uvunjifu wa maadili.

Alisema, suala la furaha ni jambo jema, baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan, ingawa wanachokipinga ni kufanyikwa vitendo vya udhalilishaji.

Alieleza kuwa, uislamu haukatazi furaha kwa mtu yeyote, bali kinachotakiwa iwe ni kwa kufuata maadili na misingi ya dini ya kiislamu, ili furaha hiyo isigeuke nakama.

ā€˜ā€™Kamati ya maadili na taaluma, inapiga marufuku kwa vijana wanaozitumia vibaya neema za bahari na fukwe, kwani athari inapojitokeza humkubwa kila mmoja,ā€™ā€™alifafanua.

Katika hatua nyingine, aliwataka wazazi la walezi kuwaelimisha watoto wao, juu ya nidhamu nzuri za kusherehekea sikukuu, ili isigeuke adhabu.

Nae sheikh Hassan Khamis Othman, aliwataka waumini wa dini ya kiislamu, kushrikiana katika kudhibiti vitendo viovu katika fukweli hiyo, kwani athari yake inaweza kuwakumba walio wengi.

ā€˜ā€™Sualala la kuwaelimisha wenzetu juu ya matumizi sahihi na fukwe, sio la kamati ya maadili na taaluma pekee, bali kila mmoja kwa nafasi yake, anaowajibu huo,ā€™ā€™alifafanua.

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi wa shehia jirani za Wambaa na Chumbageni, kuwazuia watoto wao kutoitumia vibaya neema ya ujio wa sikukuu.

Kwa upande wake ustadhi Mohamed Juma, amewakumbusha wananchi wa shehia za Wambaa na Chumbageni, kushirikiana katika kudhibiti vitendo viovu, hasa vinavyofanywa katika fukwe za Kwakitunga shehia ya Wambaa. 

Baadhi ya wananchi wa shehia za Wambaa na Chumbageni, walisema ipo haja ya kuungana na kamati yao ya maadili na taaluma, ili kudhibi vitendo vya udhalilishaji.



Hivi karibuni akizungumza kwenye mashindani ya tano ya qur-an yaliofanyika Chumbageni, Mkuu wa wilaya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakari, amewakumbusha waumini wa dini ya kiislamu, kuwa kila mmoja anawajibu wa kuzuia machafu katika jamii.

Hata hivyo, alisema yuko tayari kushirikiana na wananchi wa shehia za Wambaa na Chumbageni, katika kudhibiti vitendo viouvu kwa vijana.

Hata hivyo aliwataka wazazi na walezi, kuwabidiisha watoto wao, katika kukifuata kwa vitendo kitabu cha Muumba, ambacho kimetoa njia ya maisha yasiokuwa na shaka.

..mwishoā€¦

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...