Skip to main content

WANAWAKE WANAOWEKA VITU SEHEMU ZA SIRI KUUA MFUMO WA UZAZI



NA ZUHURA JUMA, KU@@@@

WANAWAKE wametakiwa kuacha tabia ya kuweka vitu kwenye sehemu za siri, kwani wanaweza kuathiri mfumo mzima wa viungo vya uzazi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa chama cha Waandishi Tanzania (TAMWA) Mkanjuni Chake Chake Pemba, Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba Ali Mbarouk Omar alisema, kuna baadhi ya wanawake huweka vitu katika sehemu zao za siri, jambo ambalo ni hatari kwa afya ya uzazi.

Alisema kuwa, ni vyema wakawa wanafika hospitalini na vituo vya afya kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara ili ikiwa wamepata matatizo waweze kupatiwa matibabu na sio kuweka vitu ambavyo vinaweza kuwapatia madhara zaidi.



"Kuna baadhi yao huweka vitu kama wanajitibu baada ya kupata magonjwa ya kujamiiana na kuna wengine wanaweka vitu hivyo kwa urembo, haya yote hayafai kwa sababu wanaweza kuathirika katika mfumo wa kizazi," alisema Katibu huyo.

Aidha, akielezea kuhusu maambukizi ya magonjwa ya kujamiiana alisema, pia yanasababisha kuathiri kizazi cha mama na kupeleka mtoto anaezaliwa kupata madhara mbali mbali.

"Maradhi ya kuambukiza ikiwemo ukimwi, saratani ya shingo ya kizazi, gonoria, pangusa, kisonono cha usaha ni hatari katika kuharibu mfumo mzima wa uzazi kwa mwanamke, hivyo waache tabia ya kufanya ngono zembe kuepuka magonjwa hayo," alieleza.

Mapema akifungua mkutano huo Afisa Uhusiano kutoka TAMWA Zanzibar Khairat Haji Ali alisema kuwa, elimu ya afya ya ni muhimu sana kuwafikia wanajamii, hivyo ipo haja kwa waandishi wa habari kutumia kalamu zao katika kuielimisha jamii.



Alisema kuwa, wameamua kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kusudi waelewe masuali ya afya ya uzazi, jambo ambalo litawasaidia kutoa elimu kwa jamii wakiwa na ujuzi wa hali ya juu.

"Wanawake wanapata shida kubwa kwenye mfumo wa uzazi bila kujijua, hivyo iwapo waandishi tutaweza kutoa elimu, jamii itaelewa na watakuwa ni wenye kupima afya zao na kuacha Yale ambayo yatawasababishia matatizo," alisema.

Kwa upande wao washiriki wa mkutano huo walisema kuwa, watahalikisha wanaibadilisha jamii kwa kuwapa elimu ya afya ya uzazi, ili kuondosha madhara yanayowapata wanawake na watoto.

"Tumejifunza mambo mengi ya afya ya uzazi, hivyo kupitia elimu hii, itatusaidia kuielewesha jamii ili wajitunze na kuepuka madhara mbali mbali," anaeleza.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliwahusisha waandishi wa vyombo vya habari mbali mbali kisiwani Pemba ambayo yameandaliwa na TAMWA Zanzibar.

                        MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...