Skip to main content

IDARA YA KATIBA: ‘’KUJITOLEA KWA WASAIDIZI WA SHERIA NI TAKWA LA KISHERIA’'



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MKUU wa Divisheni ya Katiba na Sheria Pemba Bakari Omar Ali, amewasisitiza wasaidizi wa sheria, kukumbuka kuwa, bado dhana ya kujitolea kwa aina ya kazi yao hiyo, itabakia pale pale licha ya changamoto walizonazo.

Alisema, kwa mujibu wa sheria inayowaongoza, ni kosa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria na kisha kuomba malipo kwa mwananchi husika.

Mkuu huyo wa Divisheni, aliyasema hayo leo Febuari 09, 2025 ukumbi wa mikutano wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ wakati akitoa maoni yake, baada ya kuwasilisha matokeo ya awali ya utafiti kwa wasaidizi wa sheria, kisiwani humo.

Alisema, ijapokuwa sasa wapo wanaodai malipo kama baraka ya kufanyakazi zao, lakini bado sheria haitambuwi uwepo wa posho kama motisha wa kufanya kazi zao.

Alieleza kuwa, msingi mkuu wakati walipoomba kazi hiyo na sasa ikiingizwa ndani ya sheria yao, ni kufanyakazi kwa njia ya kutolea, na hasa kwa wananchi wanyonge na makundi maalum.



‘’Kwenye sehemu ya utafiti huu, kumeibua hoja kwa baadhi ya wasaidizi wa sheria, wakilalamikia kukosa posho, wakati wanapotekeleza wajibu wao, wakati kisheria hiyo ni kazi ya kujitolea,’’alifafanua.

Akizungumzia kipengele kilichoibuliwa cha vitendea kazi, alisema tayari hilo serikali kuu inalifanyia kazi kwa vitendo, ikiwemo kukabidhiwa kwa usafiri aina ya bajaji kwa baadhi ya jumuiya za wasaidizi wa sheria wa Unguja na Pemba.

Hata hivyo, aliwataka wakuu wa jumuiya hizo, kuzibeba changamoto zilizomo kwenye matokeo ya awali ya utafiti huo, ili kuziweka hai jumuiya zao.

‘’Kwa mfano kuna suala la kutokuwepo kwa fursa sawa za kimafunzo na safari kikazi, migogoro, kubaguzi na mambo haya ndio yanayoweza kuibua changamoto za kutoelewa baina ya viongozi na wanachama,’’alifafanua.



Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Divisheni ya Katiba na Sheria Pemba Bakar Omar Ali, aliwataka wanachama, kujenga utamaduni wa kudumu wa kupita katika taasisi zao, ili kupata taarifa mpya.

Akiwasilisha matokea ya awali ya sehemu ya utafiti huo, Msaidizi wa sheria kutoka wilaya ya Mkoani Saleh Mussa Alawi, alisema kiujumla Jumuiya ziko vizuri hasa katika eneo la upatikanaji fursa sawa.

Alisema eneo jingine, ambalo matokeo yanaonesha liko vizuri ni usahirikishwaji kwa wanachama, wakati viongozi wanapotaka kufanya uamuzi.

‘’Lakini hata la uwiyano wa wanawake na wanaume, katika fursa, nalo linaonesha katika jumuiya zetu, liko vyema ingawa changamoto ni wanachama wenyewe,’’alifafanua.

Akichangia mataokeo ya utafiti huo, Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO Mohamed Hassan Abdalla, alisema matokeo hayo, yanahitajika kuwasilishwa mbele ya wanachama wote.

‘’Hii itasaidia kuweka sawa zaidi, maana bado changamoto ipo kwa viongozi wa Jumuiya hasa katika kuifuata katiba kabla ya kufanya uamuzi,’’alifafanua.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Mkoani ‘MDIPAO’ Nassor Hakim Haji, alisema suala la uwiyano sawa kati ya wanachama wanawake na wanaume, linaweza kuwa na changamoto kutokana na idadi kutofanana.

‘’Kwa mfano MDIPAO inawezekana wanachama wanawake ni wingi, sasa fursa za watatu watano, inabidi wanawake wawe wingi, sasa hapo lazima shida itajitokeza,’’alifafanua.

Nae Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’ Hemed Ali Hemed, alipongeza waliofanya utafiti huo na uandishi wa ripoti, kwani umetoa taswira ya aina ya jumuia zao zinavyoendeshwa.

Mkurugenzi fedha wa CHAPO Riziki Hamad Ali, alisema itapendeza kama ripoti hiyo, baada ya marekebisho wanachama watawasilishiwa.

Mkutano kama huyo unatarajiwa kufanyika tena April 12, mwaka huu, kwa ajili ya kuwasilishwa mapendekezo yaliotokana na mkutano wa uliofanyika leo.

Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...