Skip to main content

WANANCHI KASKAZINI PEMBA, ZITUMIENI SIKU 3 ZA KAMBI YA KISHERIA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa mkoa wa kaskazini Pemba, wametakiwa kuzitumia siku tatu za kambi ya kutoa masaada wa kisheria, ili kufikisha malalamiko yao ya kisheria, na kupatiwa ufumbuzi papo hapo.

Hayo yameelezwa leo Oktoba 17, 2024 na Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, katika hutuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakari, kwenye uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia, iliyozinduliwa uwanja wa Majengo Micheweni Pemba.

Alisema, siku tatu hizo watakuwepo wanasheria, Jeshi la Polisi, wasaidizi wa sheria, mahakim na mawakili, ili kusikiliza changamoto za kisheria na kuzitolea ufumbuzi papo hapo.

Alieleza kuwa, kuwapata wanasheria wakati mwingine huwa ni vigumu, ingawa kufuatia uzinduzi wa kampeni hiyo, wanapatikana papo hapo bila ya malipo.

‘’Niwatake wananchi wa mkoa wa kaskazini Pemba na hasa wa wilaya ya Micheweni, kufika hapa Micheweni majengo, ili kupata elimu na msaada wa kisheria tena bila ya malipo,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, mkuu huyo wa Mkoa aliipongeza wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora kupitia Idara ya Katiba na Msaasa wa kisheria, katika kufanikisha kampeni hiyo.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, alisema kampeni hiyo ni matokeo ya maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, juu ya upatikanaji wa haki kwa wote.




Alieleza kuwa, kampeni hii inawafikia wananchi moja kwa moja, ili kuhakikisha wanafikisha malalamiko yao ya kisheria na kupatiwa ufumbuzi bila ya malipo.

Aidha, aliwataka wananchi ambao hawatabahatika kufika Micheweni, kuendelea kuwatumia wasaidizi wa sheria waliomo katika shehia zao, ili kupata elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

Mapema Mwakilishi wa shirika la UN-Women Racho Ngoma, alisema uhitaji wa elimu ya msaada wa kisheria, umekuwa ikiogezeka siku hadi hapa Tanzania.



Katika hatua nyingine, Mwakilishi huyo wa UN-Women, alisema bado suala la ukatili wa kijinsia, limekuwa kubwa, na kusababisha wananchi 1,954 kwa mwaka 2023 kwa Zanzibar pekee kupewa msaada wa kisheria.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, aliipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, kwa kampeni hiyo ndani ya wilaya yake.

Alikiri kuwa, ndani ya wilaya hiyo ipo migogoro ya ardhi, matunzo ya watoto, utelekezaji, migogoro ya ndoa ambayo wananchi wanahitaji kupewa elimu na usaidizi wa sheria.



Afisa Mdhamini wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, alisema aliwataka watoa msaada wa kisheria, kuzingatia viwango wakati wanapowahudumia wananchi.






Awali Mkuu huyo wa mkoa, aliyapokea matembezi ya wananchi, wasaidizi wa sheria na wanasheria yalioanzia kijiji cha Chamboni hadi uwanja wa majengo, ambapo ujumbe wa mwaka huu ‘Msaada wa kisheria kwa haki, usawa, amani na maendeleo’.

Imefahamika kuwa, kuanzia leo Oktoba 17 kutakuwa na kambi ya utoaji wa msaada wa kisheria bila ya malipo hadi Oktoba 19, katika eneo hilo.

         Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan