Skip to main content

VOSHOKA WA UBAKAJI PEMBA KIKAANGONI

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAMTANDAO wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji kisiwani Pemba, wamelaani kitendo cha watu wazima, kukimbilia kwa watoto wachanga, kuwadhalilishaji, kwani husababisha athari zaidi kwao.

Walisema, miongoni mwa athari hizo ni kuwasababisha kukosa kizazi, kuwatishia masomo, athari za kisaikolojia jambo ambalo linatajwa kuzima ndoto zao za maisha.

Wakizungumza kwenye kikao cha kuwasilisha ripoti za kazi zao, kilichofanyika ofisi ya TAMWA Pemba, walisema, sasa vitendo hivyo wadhalilishaji wameelekeza nguvu zaidi kwa watoto wadogo.

Walieleza kuwa, zipo kesi kadhaa zinazowahusu watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi 10, wakifanyiwa udhalilishaji na wanaume wenye umri kuanzia miaka 40 hadi 50.

Mwanamtandao kutoka wilaya ya Mkoani Haji Shoka Khamis, alisema sasa wabakaji wameelekeza nguvu kwa watoto wadogo, jambo linalokuwa gumu wanapofika mahakamani.

‘’Wadhalilishaji sasa wamehamia kwa watoto wadogo, na kisha huwapa lugha za vitisho, kwamba wasitowe taarifa kwa familia zao, jambo linalokuwa gumu mbele ya vyombo vya sheria,’’alieleza.

Kwa upande wake Rashid Hassan Mshamata mwanamtandao kutoka Wete, alieleza kuwa wamekuwa wakiziibua kesi hizo, ingawa changamoto ni baada ya kuzifikisha mahkamani.

‘’Ukishafika mahkamani, kesi za watoto hukataa kusema jambo lolote, hii inatokana na kupewa lugha za vitisho na wabakaji na wadhalilishaji,’’alifafanua.

Nae mwanatandao Rehema Mjawiri, alisema wapo baadhi ya wazazi wanaendelea kutafunwa na muhali, jambo ambalo hukosa nguvu wa kuziendelea kesi za watoto wao.



Aidha Seif Mohamed Abdalla, alisema pamoja na kuendelea kutoa elimu ya kupingana na vitendo hivyo, bado hali ya udhalilishaji inazidi kunawiri.



‘’Tunajipa moyo kuwa, kadiri vitendo vinavyoripotiwa, hutokana na jamii kupata uwelewa na kujua wapi sasa waende, kuripoti matendo hayo yanapotokezea,’’alifafanua.

Mtendji kutoka TAMWA Zanzibar Mohamed Khatib Mohamed, alisema TAMWA imefurahishwa kuona kazi za wanamtandao zinaendelea kufanywa, hata baada ya kumalizika kwa miradi.



‘’Suala la kutoa elimu kwa jamii ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ni jambo la kila siku, sasa TAMWA inawapongeza kuona mnaendelea,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, mtendaji huyo, aliwasisitiza kuendelea kufanya kazi hiyo, kwani jamii bado inahitaji uwelewa na hasa suala la muhali wa kutoa ushahidi mahakamani.

Akizungumza hivi karibuni, Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alisema suala la kushirikiana na vyombo vya sheria ni jambo jema.

 

‘’Zipo kesi hufutwa mahakamani, kwa kule mashahidi kutofika mahakamani, jambo ambalo huvizisha kesi za udhalilishaji,’’alieleza.

 

Afisa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wilaya ya Chake chake Salma Khamis Haji, alisema njia ya kutokemeza matendo hayo, ni kwa watendewa, kutoa taarifa, pindi wanakapoona viashiria vya ukatili na udalilishaji.

 

Sheikh Abdalla Nassor Mauli, alisema kama jamii itaamua kukifuata kitabu cha Allah kwa vitendo, matendo hayo yatapungua, hata kabla ya kufanyika kwa utafiti wowote.

 

Matukio ya ubakaji, ulawiti ambayo huwakumba wanawake na watoto hapa Zanzibar, yameripotiwa kupungua kiduchu kwa mwezi Machi, na kufikia 125, upungufu wa matukio 50 kwa mwezi Febuari mwaka huu.

 

Taarifa kutoka kwa ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inaonesha kuwa mwezi Febuari pekee kuliripotiwa matukio 175, sawa na matukio sita kwa siku.

 

Ingawa kwa mwezi Machi, kumeripotiwa wastani wa matukio manne kwa siku, ambapo ikaelezwa kuwa, kwa miezi hiyo mwili, kuliripotiwa matukio 300, ambayo ni wastani wa matukio 28, kwa kila wilaya, kati ya zote 11 za Zanzibar.

 

                 Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan