Skip to main content

VOSHOKA WA UBAKAJI PEMBA KIKAANGONI

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAMTANDAO wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji kisiwani Pemba, wamelaani kitendo cha watu wazima, kukimbilia kwa watoto wachanga, kuwadhalilishaji, kwani husababisha athari zaidi kwao.

Walisema, miongoni mwa athari hizo ni kuwasababisha kukosa kizazi, kuwatishia masomo, athari za kisaikolojia jambo ambalo linatajwa kuzima ndoto zao za maisha.

Wakizungumza kwenye kikao cha kuwasilisha ripoti za kazi zao, kilichofanyika ofisi ya TAMWA Pemba, walisema, sasa vitendo hivyo wadhalilishaji wameelekeza nguvu zaidi kwa watoto wadogo.

Walieleza kuwa, zipo kesi kadhaa zinazowahusu watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi 10, wakifanyiwa udhalilishaji na wanaume wenye umri kuanzia miaka 40 hadi 50.

Mwanamtandao kutoka wilaya ya Mkoani Haji Shoka Khamis, alisema sasa wabakaji wameelekeza nguvu kwa watoto wadogo, jambo linalokuwa gumu wanapofika mahakamani.

‘’Wadhalilishaji sasa wamehamia kwa watoto wadogo, na kisha huwapa lugha za vitisho, kwamba wasitowe taarifa kwa familia zao, jambo linalokuwa gumu mbele ya vyombo vya sheria,’’alieleza.

Kwa upande wake Rashid Hassan Mshamata mwanamtandao kutoka Wete, alieleza kuwa wamekuwa wakiziibua kesi hizo, ingawa changamoto ni baada ya kuzifikisha mahkamani.

‘’Ukishafika mahkamani, kesi za watoto hukataa kusema jambo lolote, hii inatokana na kupewa lugha za vitisho na wabakaji na wadhalilishaji,’’alifafanua.

Nae mwanatandao Rehema Mjawiri, alisema wapo baadhi ya wazazi wanaendelea kutafunwa na muhali, jambo ambalo hukosa nguvu wa kuziendelea kesi za watoto wao.



Aidha Seif Mohamed Abdalla, alisema pamoja na kuendelea kutoa elimu ya kupingana na vitendo hivyo, bado hali ya udhalilishaji inazidi kunawiri.



‘’Tunajipa moyo kuwa, kadiri vitendo vinavyoripotiwa, hutokana na jamii kupata uwelewa na kujua wapi sasa waende, kuripoti matendo hayo yanapotokezea,’’alifafanua.

Mtendji kutoka TAMWA Zanzibar Mohamed Khatib Mohamed, alisema TAMWA imefurahishwa kuona kazi za wanamtandao zinaendelea kufanywa, hata baada ya kumalizika kwa miradi.



‘’Suala la kutoa elimu kwa jamii ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ni jambo la kila siku, sasa TAMWA inawapongeza kuona mnaendelea,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, mtendaji huyo, aliwasisitiza kuendelea kufanya kazi hiyo, kwani jamii bado inahitaji uwelewa na hasa suala la muhali wa kutoa ushahidi mahakamani.

Akizungumza hivi karibuni, Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alisema suala la kushirikiana na vyombo vya sheria ni jambo jema.

 

‘’Zipo kesi hufutwa mahakamani, kwa kule mashahidi kutofika mahakamani, jambo ambalo huvizisha kesi za udhalilishaji,’’alieleza.

 

Afisa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wilaya ya Chake chake Salma Khamis Haji, alisema njia ya kutokemeza matendo hayo, ni kwa watendewa, kutoa taarifa, pindi wanakapoona viashiria vya ukatili na udalilishaji.

 

Sheikh Abdalla Nassor Mauli, alisema kama jamii itaamua kukifuata kitabu cha Allah kwa vitendo, matendo hayo yatapungua, hata kabla ya kufanyika kwa utafiti wowote.

 

Matukio ya ubakaji, ulawiti ambayo huwakumba wanawake na watoto hapa Zanzibar, yameripotiwa kupungua kiduchu kwa mwezi Machi, na kufikia 125, upungufu wa matukio 50 kwa mwezi Febuari mwaka huu.

 

Taarifa kutoka kwa ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inaonesha kuwa mwezi Febuari pekee kuliripotiwa matukio 175, sawa na matukio sita kwa siku.

 

Ingawa kwa mwezi Machi, kumeripotiwa wastani wa matukio manne kwa siku, ambapo ikaelezwa kuwa, kwa miezi hiyo mwili, kuliripotiwa matukio 300, ambayo ni wastani wa matukio 28, kwa kila wilaya, kati ya zote 11 za Zanzibar.

 

                 Mwisho

 

Comments