Skip to main content

SHUNGI: 'WATAKA KUJENGEWA BARABARA YAO KWA KIWANGO CHA LAMI'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wameikumbusha serikali, kuwajengea barabara yao ya Chanjamjawiri- Tundaua kwa kiwango cha lami, ili wapate kuitumia kwa utulivu.

Walisema, kwa sasa imesambaa mashimo na msingi yenye kina kirefu, jambo ambalo haliwapi utulivu, wakati wanapokwenda kwenye shughuli zao za kimaisha.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema barabara hiyo ambayo awali ilikuwa na lami, kwa sasa zaidi ya miaka minne imekuwa ikihataraisha waenda kwa miguu, achia mbali wanaotumia vyombo vya moto.

Mmoja kati ya wananchi hao Moza Suleiman Mohamed wa Misooni alisema, hasa wao akinamama wamekuwa wakipata usumbufu mara pale wanapokuwa wajawazito.

‘’Hutokezea sisi kutakiwa kuripoti hospitali ya Chake chake kwa huduma na uchunguuzi zaidi, lakini tunapoitumia barabara kutokana na mashimo yaliomo, hupata mtikisiko,’’alieleza.

Nae Asma Said Abdalla wa Chanjamjawiri, alisema barabara hiyo ndio wanayoitumia wanapotaka kwenda kwenye vijiji kadhaa vya shehia hiyo, ingawa hali yake imeshachakaa.

Nae Mbarouk Idrissa Omar, alisema kutokana na kuchakaa kwa barabara hiyo, imekuwa ikiwawiya vigumu wafanyabiashara pale wanaposafirisha bidhaa zao, kutoka kijijini kwao kwenda mjini.

‘’Kwa mfano, siku nyingine husafirisha ndizi, muhogo, matikti au nyanya, lakini hata zikifika sokoni zimeshashuka thamani, kwa kule kuvurugika kutokana na mashimo makubwa,’’alieleza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kushughulikia kero za watu wenye ulamavu shehiani humo, Khadija Mohamed Suleiman, alisema uchakavu wa barabara hiyo, huwa ni kikwazo kwa wenye ulemavu, wanapokuwa kwenye shuguhuli zao.

‘’Kwa mfano, hata wanafunzi wenye ulemavu wa viungo na wale wasioona, wamekuwa wakipata usumbufu, kuanzia wanapotoka nyumbani hadi skuli, kwa kule kuwepo miundombinu isiyorafiki barabarani,’’alieleza.

Nae mzazi Zulekha Nassor Hilali, alieleza kuwa ni vyema kwa serikali, kupitia wizara husika, kuangalia uwezekano wa kuwajengea kwa kiwango cha lami barabara yao, ili iwasaidie katika shughuli zao.

Sheha wa shehia ya Shungi Hamad Ramadhan Soud, alisema taarifa alizonazo kuwa, ni kuwa wakati wowote serikali, itaanza upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa barabara hiyo.



‘’Kwa hakika taarifa za moja kwa moja kuwa ujenzi wa barabara hii utaanza lini sijaambiwa, lakini tunaambiwa kuwa bado serikali inayo nia ya kuijenga barabara hiyo, kwa kiwango cha lami,’’alieleza.

Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Pemba Ibrahim Saleh Juma, alisema barabara hiyo, imo kwenye mpango wa ujenzi wa kiwango cha lami.

Alieleza kuwa, katika mpango mkuu wa wizara unaojumuisha kilomita 371, na barabara za ndani zimo ikiwemo hiyo ya Chanjamjawiri-Shungi hadi Tundaua wilaya ya Chake chake.

Alieleza, kwa sasa hawajaanza hata mpango wa tathmini kwa wananchi wanaoishi pembezoni wa barabara hiyo, ingawa wakati ukifika, wahusika wa zoezi hilo wataarifiwa mapema.

‘’Ni kweli barabara hiyo imeshachakaa na zipo nyingi kama hizo, lakini ipo kampuni imeshateuliwa kwa ajili ya ujenzi, na wakati ukifika wananchi wataarifiwa, ili watoe ushirikiano,’’alifafanua.

Akizungumza hivi karibuni kwenye ufunguzi wa barabara ya Kijangwani-Birikau, Waziri wa wizara hiyo Dk. Khalid Salum Mohamed, alisema baada ya muda mfupi, miundombinu ya barabara za ndani kisiwani Pemba, zitang’ara.


Shehia ya Shungi iliyopo wilaya ya Chake chake Jimbo la Chonga, inao wananchi 3,884 ambapo inaundwa na vijiji vya Missoni, Shungi, Kiziwani, Chanjamjawiri, inayo miundombinu ya elimu, afya, maji safi na salama na barabara.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch