Skip to main content

JAJI IBRAHIM ATUPILIA MBALI RUFAA KESI DAWA ZA KULEVYA

 


NA MARYAM NASSOR, PEMBA @@@@       

HUKUMU ya rufaa ya dawa za kulevya inayohusisha kete 1,678 iliyowasilishwa mahakama kuu Zanzibar, kanda ya Pemba, imekataliwa na Jaji wa mahakama hiyo, Ibrahim Mzee Ibrahim, baada ya kubaini kuwa, upande wa mashtaka tokea awali, ulithibitisha kosa pasi na shaka yoyote.

Jaji Ibrahim akitoa uamuzi wa rufaa hiyo na baada ya kujiridhisha, aliamuru mshtakiwa huyo Zubeir Jerad Said wa Bopwe Pemba, kutumikia chuoa cha mafunzo, kwa muda wa miaka 10, kama alivyohukumiwa awali mahakama ya mkoa.

 Alisema kuwa, mahakama yake imeitupilia mbali rufaa hiyo, kutokana na kuwa upande wa mashtaka, ulikuwa na mashahidi ambao walitoa ushahidi wa wazi na wakuaminika, hivyo hawezi kuipindua hukumu hiyo.

 

Jaji huyo alisema kuwa, mshtakiwa alikamatwa na na dawa hizo na kupewa jina la kielelezo ‘pw3 na pw4’, ambacho ni mfuko wa dawa za kulevya aina ya heroin kete uliokuwa na 1, 678  zenye uzito wa  gramu 41.53.

 Alieleza kuwa, wakili wa utetezi Abeid Mohamed Said wakati anaomba rufaa, aliieleza mahakama sababu ya rufaa, kuwa mteja wake, hakupatiwa haki kutokana na ushahidi uliyotolewa na kumtia hatiani, haukufikia kiwango au ulichezewa.

Wakili wa utetezi alidai kuwa, ukamataji wa mteja wake, haukufuata sheria na ulikuwa kinyume na kifungu cha 35 (1) na (4) cha sheria namba7 ya mwaka 2018.

Alidai kuwa, mteja wake alikamatwa hadharani na askari waliokuwa kwenye doria, lakini hawakuita shahidi  huru hata mmoja, ili kushuhudia kitendo hicho, hivyo inaoneshaa askari Polisi hao walikuwa na nia mbaya.

“Mteja wangu alikamatwa hadharani na Polisi waliyokuwa doria, lakini baada ya kumkamata hawakuita shahidi huru ambae angeshuhudia tukio hilo,” alidai wakili huyo.

 Aidha, alidai kuwa, pia mnyororo wa kesi ulikatika, hiyo inathibitishwa na kuwa vielelezo vilivyopewa majina ya ‘pw3 na pw4’ kwani kulikuwa hakuna ushahidi wa maelezo wapi kielelezo hicho kilihifadhiwa, mara baada ya kufikishwa kituoni.

Hivyo, kwa mantiki hiyo, wakili Abeid, aliiomba mahakama hiyo, itupilie mbali  hukumu hiyo, adhabu ibatilishwe na mteja wake achiwe huru.

Akijibu, tuhuma hizo, Mwendesha mashtaka wa Serikali Juma Ali, alisema kuwa ni kweli mshtakiwa alikamatwa hadharani, ingawa ilikuwa ni usiku majira ya saa 4:00 hivyo, ilikuwa vigumu kumpata mtu huru kwa wakati huo.



Alidai kuwa, muomba rufaa huyo, ushahidi ulimtia hatiani moja kwa moja, kutokana na kuwa alikamatwa na mfuko wa kete 1,678, aliyokuwa kautia ndani ya fulana yake.

Aidha alidai kuwa, mnyonyoro wa kesi haukukatika, mara baada ya mtuhumiwa kukamatwa na kufikishwa Polisi, pamoja na kielelezo chake, alikabidhiwa askari aliyekuwepo na ilipofika asubuhi, alikabidhiwa mtunza vielelezo na kupewa namba WIR2008/2021.

Alidai, kuhusiana na kukiukwa kwa kifungu cha 35(4) cha sheria namba 7 ya mwaka 2018 alidai kuwa, kifungu hicho hakijakiukwa, kwani mara nyingine sio lazima kufuatwa kwa kifungu hicho, hasa kutokana na mtuhumiwa hakubainisha ni watu wapi wapewe taarifa, kuwa yeye yupo kituoni.

 Baada ya kuupitia ushahidi huo, Jaji Ibrahim alisema kuwa, ameupitia kwa umakini  mkubwa ushahidi huo na kujiridhisha, kwa kuona upande wa mashtaka, ulifanikiwa kuthibitisha tuhuma hizo pasi na shaka, kwani ulikuwa na nafasi nzuri ya kuwaona mashahidi katika mazingira hayo.

Kwa mantiki hiyo, rufaa hiyo imekataliwa na mshtakiwa anatakiwa kutumikia kifungo chake cha miaka 10 chuo cha mafunzo, alichohukumiwa na mahakama ya Mkoa hapo awali.

Shauri hilo lilifunguliwa Juni 16, mwaka 2021, katika mahakama ya mkoa na mshtakiwa ni Zubeir Jerad Said (30) mkaazi wa Bopwe wilaya ya Wete Pemba.

Mshitakiwa huyo, alipatikana na dawa hizo, Juni 6, mwaka 2021 eneo la Bopwe majira ya saa 4:00 usiku, ambapo bila ya halali,   alipatikana na kete 1,678 zenye uzito wa gramu 41,53.

Kupatikana na dawa za kulevya, kinyume na kifungu cha 21 (1) (d) cha sheria za Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya Zanzibar, cha sheria namba 8 ya mwaka 2021, sheria za Zanzibar.

                                    MWISHO

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch