Skip to main content

'WAHARIRI MASHINE NYOOFU UKUZAJI, UIMARISHAJI LUGHA YA KISWAHILI'

 




NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIAR

 
JUHUDI za wahariri kutoka vyombo mbali mbali vya habari nchini zimesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza na kuleta mabadiliko katika matumizi  ya Kiswahili fasaha na sanifu nchini.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo katika Mkutano wa wahariri wakuu wa vyombo vya habari  kuelekea maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani uliofanyika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar. 

Amesema wahariri wakuu wana jukumu la kupitisha na kuweka sawa maandishi yote ndani ya Vitabu, Magazeti na majarida hatua ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza lugha ya kiswahili .

Aidha  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka wahariri kulinda Maadili ya kazi zao katika kuyaibua mambo mbali mbali yasiyoendana na mila, tamaduni na silka zetu bila ya kumuonea Mtu au Taasisi fulani.

Sambamba na hayo Mhe. Hemed  ameeleza kuwa kuna fursa nyingi zinazopatikana katika lugha ya Kiswahili na kuwataka wenye ujuzi wa Lugha hiyo kuchangamkia fursa hizo ikiwemo ukalimani, tafsiri, uhariri, uandishi na utangazaji wa habari pamoja na ufundishaji wa Lugha hiyo kwa wageni.

Ameeleza  kufurahishwa kwake kwa  kuona kupitia Baraza la Kiswahili la  Taifa (BAKITA) na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) kuweka mikakati katika Nchi mbali mbali ya kukizungumza na kukieneza kiswahili ikiwemo Ujerumani, Uholanzi, Italia, Nigeria, Nchi za falme za kiarabu, Malawi, Rwanda na Zimbabwe hatua ambayo ni dhahiri ya umahiri wao katika kutangaza Lugha hiyo.

Ameeleza kuwa mbali na juhudi hizo tayari Nchi zisizopungua Thalathini na Nane (38) kupitia Redio na vituo vya  Televisheni vinarusha matangazo yake kwa Lugha ya Kiswahili.
 
 




Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amelitaka Jukwaa la wahariri kushirikiana na Mabaraza ya Kiswahili nchini kuhakikisha vyombo vya habari vinatumia  kiswahili fasaha na Sanifu .

Kwa kuzingatia upekee wa lugha ya kiswahili Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi imeamua kuifanyia marekebisho Sheria ya Habari ili iendane na Mabadiliko yanayotokezea katika Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Habari,  Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita ameeleza kuwa Serikali ina Mkakati wa kukifanya Kiswahili kuwa ni bidhaa itakayowanufaisha wataalamu na Taifa kwa ujumla ikiwemo kupeleka walimu kusomesha Kiswahili nje ya Tanzania pamoja na kuwakaribisha wageni kusoma Lugha ya Kiswahili ndani ya Tanzania.

Aidha Mhe. Tabia amewataka wahariri wakuu kukemea tabia ya wachache wanaotumia Misamiati kinyume na maana zilizokusudiwa ili kudhibiti ufasaha wa Lugha ya Kiswahili.

Nae Naibu Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Khamis Mwinjuma ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinaendelea kuchukua jitihada mbali mbali katika kuhakikisha Lugha ya Kiswahili inakuwa ni Nembo ya Taifa la Tanzania.

Amesema ni wajibu wa wananchi kuhakikisha wanaitangaza Lugha ya Kiswahili ikiwemo kuibua Utalii wa Lugha ya Kiswahili ili kuhakikisha wageni wanaotembelea Tanzania wanatumia fursa zitokanazo na Lugha hiyo.



Akitoa maelezo kuhusu Jukwaa hilo Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKIZA) Bi Consolata Mushi ameeleza kuwa Jukwaa hilo litakuwa ni chachu ya kupunguza changamo to za Kiswahili zinazojitokeza katika Vyombo mbali mbali vya Habari.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch