Skip to main content

TAMWA -ZANZIBAR "SHERIA, SERA ZINAZOLENGA KUPUNGUZA UDHALILISHAJI KWA WATOTO ZITUPIWE JICH0"

 


Na Najjat Omar – Unguja. 

Wadau wa masuala ya kijamii na kijinsia wamekutana kwa pamoja kuzungumzia sera na sheria zinahusu masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na mapungufu yake. 

Mkutano huo ambao umeendaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Zanzibar –TAMWA uliokutanisha wadau kutoka katika Taasisi mbalimbali za kijamii na kiserikali kujadili juu ya ufuatiliaji,utekelezaji na kutoa maoni juu sera na sheria zinahusu masuala ya udhalilishaji wa kijinsia kwa jamii hususan watoto. 

Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali inaonesha matukio hayo yameongezeka kutoka matukio 1,222 mwaka 2021 hadi matukio 1,360 mwaka 2022, ongezeko ambalo ni la matukio 138. 

Takwimu hizo zinaonesha kwamba kwenye matukio 1,361 yaliyotokea mwaka 2022, matukio 1,173 yalijumuisha watoto, 185 yalihusu wanawake na matatu yalihusu wanaume. Kwenye matukio 1,173 ya watoto, 889 walikuwa ni wasichana, huku 284 walikuwa ni wavulana. 

Akifungua mkutano huo Afisa miradi kutoka TAMWA –Pemba Fathiya Mussa amesema lengo la kukutana hapa ni kufahamu na kutambua masuala juu  sheria na sera mbalimbali ambazo zinakwamisha harakati za  kupinga vitendo vya  udhalilishaji wa kijinsia kwenye ngazi zote za kijamii. 

“Matukio kama haya ya udhalilishaji kuendelea kuyasikia ni jambo linaloumiza kichwa sana,ukizingatia Zanzibar watu wake wanaoamini dini hivyo lazima  kuwepo kwa jitihada  za pamoja kupinga vitendo vya udhalilishaji” Amesema Fathiya huku akiwakaribisha wadau katika mkutano huo. 



Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar SUZA kitengo cha Sheria na Sharia – Daktari Sikujua Omar alikuwa mmoja kati ya wawasilishaji mada ambapo yeye alijikita zaidi kwenye kuziangalia na kuzifafanua Sera 11 huku akiigusia Seraya watu wenye ulemavu  ya mwaka 2018 ambapo moja kati ya kipengele chake ni kuwaepusha watu wenye ulemavu na hatari ya unyanyasaji wa kingono. 

“Kwenye sera zote hizi zinamgusa mtoto kwenye kila hatua ,ila jee zinatekelezwa kwa ukubwa gani katika kumlinda mtoto wetu na masuala yote ya udhalilishaji ambayo yanaendelea hivi sasa hapa Zanzibar,licha ya kuwa na miongozo na wadau ambao wanasimamia masuala ya udhalilishaji?” Aliuza Daktari Sikujua. 

Usimamizi wa sheria katika ngazi za Mahakama ni moja kati ya kipengele ambacho kimekuwa kwenye mijadala ya wahanga,wadau na waathirika wa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia. 

Mohammed Saleh Idd Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka amewasilisha mada kwa upande kwa kisheria huku akitoa ufafanuzi wa jinsi sheria zinavyofanya kazi kwenye kesi za udhalilishaji kwa watoto .Amesema “ Sheria ambazo zinasimamia masuala ya udhalilishaji zinatakiwa kuthibitisha tukio ya binti au kijana kuingiliwa kwenye sehemu zake za siri, jambo ambalo linaweza kuzua taharuki kwa mhanga au pale ushahidi unapotakiwa ila ndio sheria inavyotaka” Amemalizia Mohammed. 



Akichangia hoja kwenye mwenendo wa Mahakama Hakimu wa Mkoa wa Vuga Khamis Ali Simai amesema masuala ya udhalilishaji sio tu ubakaji na ulawiti sheria zinatambua masuala ya makuzi,malezi,lishe na mengine yakikosekana kwa mtoto ni udhalilishaji pia. 

“Kwa mfano utasikia kesi au taarifa kuhusu mtoto kupigwa,kuchoma moto au hata kutelekezwa ila kesi hizo hazipo kwenye mahakama kwa wingi wake,sheria pia iangalie suala ya kuwapatia adhabu wote maana kesi zinazohusu watoto ambao wana umri wa miaka 18 kwenda juu zinakuwa na changamoto ya ushahidi na upande mmoja tu wa kiume ndio unatiwa kutiwa hatiani hivyo kama sheria ikabadilishwa na kuwaweka wote kifunguni haya mambo yanaweza kupungua” Amemalizia Hakimu Khamis. 

Shadida Omar ni mwanasheria kutoka THRDC  amesema suala la elimu kwa jamii kuhusu uelewa wa sheria na usimamizi wake ni jambo ambalo serikali na wadau wote wanatakiwa kulisimamia na kulipa kipaombele. 

“Elimu ni muhimu sana ,maana kwa mfano suala la dhamana lipo kisheria ila jamii inapoona mtu aliyeshukiwa amefanya kitendo hicho yupo nje anaona hakutendewa haki na mamlaka husika hivyo suala la elimu kwenye sera na sheria kujulikana lazima wananchi wapatiwa elimu “ Amemalizia Shadida. 

Wadau kutoka katika Taasisi zote wamekubaliana kwa pamoja suala la kuwepo kwa marekebisho ya baadhi ya sheria  pia kusimamia na kufuatilia sera zote zinazogusa masuala ya mtoto kwa ujumla. 

Mkutanao huo wa majadiliano juu ya sera na sheria zinazosimamia masuala ya udhalilishaji Zanzibar amefanyika katika ukumbi wa Kariakoo ulipo kisiwani Unguja. 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch