Skip to main content

TAMWA CHAWAKUTANISHA WADAU WA TEKNOLOGIA NAMNA YA KUPUNGUZA UDHALILISHAJI

 



 Na Najjat Omar – Unguja. 

 

Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Zanzibar –TAMWA, wamewakutanisha wadau mbalimbali katika kujadili masuala ya ukuaji wa teknolojia kwenye dhana ya kupunguza vitendo vya udhalilishaji. 

Majadiliano hayo yalifanyika katika ukumbi wa Raha Leo ulipo kisiwani Unguja kwa kuwakutanisha wadau wa masuala ya kijamii kama viongozi wa kisiasa,walimu,wanafunzi,viongozi wa dini,Jeshi la Polisi,Mahakimu pamoja wadau kutoka Mahakamani. 

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake TAMWA –Zanzibar Asha Abdi amesema licha ya ukuaji wa teknolojia kurahisisha masuala ya ujifunzaji kwa watoto ila kwa  upande mwengine unachochea udhalilishaji wa watoto kuiga hata kufanya na kujifunza mambo mabaya. 

“Ukuwaji wa teknolojia umekuwa mkubwa ambapo nao una changamoto zake ,watoto wanajifunza mambo huko kwenye mitandao na kujaribu kwa kufanya sasa hii teknolojia pia inachochea sana masuala ya udhalilishaji kwa watoto kama jamii tunatakiwa tujitahidi sana kuwalinda watoto na masuala haya kwa kuwa makini.” Amesema Asha Abdi wakati akifungua majadiliano hayo. 

Akiwasilisha hoja Mkufunzi kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar – SUZA Daktari Sikujua Omar amesema simu janja zimekuwa na msaada mkubwa kwa watoto kwenye ujifunzaji ila watoto pia wanapitia masuala ya udhalilishaji kwenye matumizi ya simu hizo ikiwemo kurusha au kurushiwa picha chafu. 

“Wengi wenu hapa mnatumia simu janja na mnajua hasa kutumia mambo mbalimbali kwenye mitandao ila muangalie pia suala la kujilinda na udhalilishaji nyinyi wenyewe kama watoto kwa sababu ulinzi unaanza na wewe kwanza” Amemalizia kusema Daktari Sikujua. 

 

 


Baadhi ya viongozi wa majukwaa ya vijana kutoka Shehia mbali mbali wamesema suala la udhalilishaji na teknolojia ni jambo ambalo linatakiwa kuangalia na familia pale inapotoa fursa ya kijana wao kutumia simu. 

Talhiya Juma ni Mwenyekiti wa Baraza la Watoto shehia ya Kama amesema kuwa suala  la wahanga wa udhalilishaji kufichwa au hata kutumia simu kuwatangaza au kuwarekodi bado linawaathiri watoto hivyo jamii iliangalie hili kwa umakini. 

“Si vibaya sisi vijana kutumia simu ila hata watu wazima unaotumia simu kuwaposti watoto wao au pale vitendo vinapotokea vinazidisha sana suala la udhalilishaji kwa watoto” Amesema Talhiya. 

Viongozi wa dini wanasababu lukuki za kuielemisha jamii kuhusu kupingana na masuala ya udhalilishaji kwa jamii hususan kuwasaidia wazazi kutambua athari za teknolojia kwa watoto. 

Mchungaji wa Kanisa la KKKT Lidya Isaya amesema suala la udhalilishaji limechukua sura mpya kwa sababu ya ukuaji wa teknolojia kwenye ulimwengu hivyo kila mmoja aawajibu wa kuwaelimisha watoto juu ya matumizi sahihi ya simu. 

“Tunaona picha za utupu zinatumwa kwenye mitano na nyengine ni za watoto wadogo,kisha zinasambwaza huo pia ni udhalilishaji maana ikitokea hio itamuathiri zaidi mtoto hivyo jukumu la kuwalinda watoto ni la jamii mzima” Amesema Lidya wakati wa majadiliano hayo. 

Sophia Ngalaphi ni Afisa Mawasiliano kutoka TAMWA,amesema suala la udhalilishaji kwa watoto ni kilio kikubwa kwa jamii ila sasa linajihusisha moja kwa moja na matumizi mabaya ya mtandao.”Wadau ambao wamekuja hapo wanakaa na jamii hivyo jukumu la kuwalinda watoto na matumizi mabaya ya teknolojia ni la mzazi,mtoto mwenyewe na jamii kwa ujumla” Amesema Sophia. 

Zaidi ya wenyeviti wa mabaraza ya watoto 50 ,viongozi wa dini,wawakilishi wa taasisi mbalimbali walikutana kwa pamoja kujadiliana kwa pamoja  njia nzuri ya matumizi ya teknolojia kwa watoto ikiwa kama ni maadhimisho ya mtoto wa Afrika yaliyobebe kaulimbiu ya “Matumizi sahihi ya kidigitali kwa ustawi bora wa mtoto”. 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch