Skip to main content

WANASIASA PEMBA WAZIPA KONGOLE PEGAO, ZAFELA, TAMWA-ZANZIBAR

 


 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANASIASA Kisiwani Pemba, wamesema kazi iliyofanywa na PEGAO, ZAFELA na TAMWA ya kuibua kero za wananchi na kuzifikisha eneo husika, na kisha kuchukuliwa hatua, hakuna mwanasiasa yeyote engeweza kuifanya kazi hiyo.

Walisema, taasisi hizo zilifika katika wilaya zote nne za Pemba, na kukutana wananchi, wakiwemo wanawake na kuzisikiliza changamoto zao, na kisha kuzifika tasisi husika kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.

Wakizungumza kwenye mkutano maalum wa kuwasilisha utendaji kazi kwa wahamasishaji jamii hao, kupitia mradi wa kuiwezesha jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia, na kufanyika ofisi ya KUKHAWA, walisema kazi iliyofanywa ni kubwa.

Mwenyekiti wa Chama cha wakulima cha AAFP, taifa Said Soud Said, alisema kazi hiyo anaona kusingekuwa na mwanasiasa yeyote, engeweza kuwafikia wananchi na kuchukua kero kwa lengo la kuzipatia sulhu.

Alieleza kuwa, kazi hiyo inafaa kuthaminiwa na kuungwa mkono na serikali kuu, kwa kuziwezesha tasisi hizo tatu, ili kuendelea kuisaidia serikali.

‘’Kama ingekuwa taasisi zote hapa Zanzibar, zinafanyakazi kubwa kama iliyofanywa na PEGAO, ZAFELA na TAMWA- Zanzibar wananchi wengekuwa wanaishi bila ya changamoto kubwa,’’alisema.

Nae mwanasiasa kutoka CHADEMA mkoa wa kusini Pemba, Time Ali Mohamed, alisema kwa kiasi kikubwa taasisi hizo zimesaidia sana, na kusababisha wananchi kupatiwa huduma za kijamii.

Alieleza kuwa, hata wanawake wamekuwa wahanga wakubwa wa kukosa nyaraka za lazima, mfano vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho, kufuata hudua za afya masafa marefu, lakini sasa juhudi za ZAFELA, PEGAO na TAMWA-Zanzibar zimesaidia,’’alifafanua.

Nae mwanachama wa CUF Mohamed Haji Kombo na mwenzake wa ACT-Wazalendo Juma Khamis Ali, walizitaka tasisi hizo, kuendelea kuwaelimisha wanawake juu ya haki zao za uongozi, siasa na demokrasia.





Mwakilishi wa Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Dk. Massoud Suleiman Abdalla, alisema bado suala la uzalendo limekuwa changamoto kwa wananchi, na kupelekea huduma nyingi kukwama.

‘’Inawezekana dawa zipo hospitali, au wakati mwengine mfanyakazi anakabidhiwa vitendea kazi, lakini kwa kule kukosa uzalendo, jamii hukosa huduma hiyo,’’alieleza.



Nae mwakilishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Harith Bakar Waziri, alisema changamoto ya makaazi kwa wanafunzi, uhaba wa waalimu karibu litatuka historia jambo hilo.

‘’Awamu hiyo ya serikali ya nane, imedhamiria kuajiri waalimu karibu 1000 kwa Pemba, ujenzi ya vyumba vya madarasa 1000, ili kuhakikisha hakuna, skuli yenye mikondo miwili ya wanafunzi,’’alieleza.



Akifungua mkutano huo, Mratibu wa TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema wamegundua kuwa, katiba za vyama, sheria za ajira zimekuwa changamoto kwa wanawake wanaogombea nafasi za kisiasa.

Alieleza kuwa, suala la kurejeshwa ama kutorejeshwa tena kazini baada ya kukosa nafasi kwenye uchaguzi mkuu, limekuwa likiwatia woga wanawake.




Mratibu wa mradi wa kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia ‘SWIL’ kutoka PEGAO Dina Juma, alisema kama huduma za kijamii haziko sawa, mwanamke hafikirii kugombea.

‘’Mwanamke ni mtu anayeishi kwenye dimbwi la changamoto za kifamilia, sasa kama na huduma za kijamii hazijaimarishwa, wazo la kudai haki yake ya uongozi, huwa mbali naye,’’alieleza.



 Akifunga mkutano huo, Mkurugenzi wa PEGAO Hafidh Abdi Said alisema, bado katiba za vyama vya siasa na viongozi wakuu wa vyama, hawajaona umuhimu wa wanawake kushika uongozi.

‘’Wanawake hata kwa takwimu ya sensa ni wengi kuliko wanaume, lakini kwanini kwenye nafasi za uongozi hawaonekani, bado wanakabiliwa na changamoto kadhaa,’’alieleza.



Tayari wahamasishaji jamii kisiwani Pemba ambao wanatekeleza mradi wa ‘SWIL’ unaoendeshwa na PEGAO, ZAFELA na TAMWA-Zanzibar wameshazifikia shehia 56, kwa wastani wa wananchi 3,000 kuwapa elimu ya umuhimu wa wanawake kuwa viongozi.

                   Mwisho    





Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...