Skip to main content

JAJI RABIA AWATAKA WANANCHI KUWALALAMIKIA WATUMISHI VISHOKA WA MAHKAMA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuitumia Kamati ya maadili ya watumishi wa mahakama, kwa kufikisha malalamiko yao pale wanapoona wamekwazwa kwa njia moja ama nyingine, na mtumishi yeyote wa mahakama.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Jaji wa mahakama kuu Zanzibar, Rabia Hussein Mohamed, wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, juu ya uwepo wa kamati hiyo.

Alisema kwa wananchi waliopo Pemba, wanaweza kufikisha malalamiko yao kwa njia ya maandishi kwenye jengo la mahakama kuu Chake chake, na kisha kamati hiyo kuyasikiliza kwa kina.

Alisema, kamati hiyo baada ya kusikiliza hupeleka mapendekezo kwa Jaji mkuu kwa ajili ya hatua nyingine za kinidhamu, kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Jaji Rabia alieleza kuwa, kamati hiyo ambayo inaundwa na wajumbe watano, inalengo la kuona watumishi wa mahakama wanafanyakazi zao kama sheria na kanuni za utumishi zinavyoelekeza.

Aidh Mwenyekiti alisisitiza kuwa, huu sio wakati tena kwa wananchi kulalamika chini ya meza, pale wanapoona wamefanyiwa ukiukwaji wa kimaadili ya kazi.

“Kamati yangu, moja ya jukumu lake kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa mahakama ya mwaka 2018, ni kuchunguuza na kutoa mapendekezo kwa Jaji mkuu na tume ya utumishi wa mahakama, kwa kuchukua hatua,’’alieleza.




Kuhusu uwepo wa kamati hiyo, alisema ni kuweka kwa ufanisi nzuri kwa watendaji wa mahakama, ili kuwapa nafasi wananchi kuendelea kukitumia chombo hicho, kwa uwazi.

Katibu wa kamati hiyo, Hussein Makame Hussein alisema, baada ya kupokea malalamiko hayo na kuyachunguuza, huwafikisha mapendekezo kwa ngazi husika.

‘Sisi kamati yetu haina uwezo kisheria kutoa adhabu, bali ngazi ya Jaji mkuu na mamlaka ya kinidhamu ndio wanaoweza kumuwajibisha mtumishi husika,’’alieleza.

Hata hivyo Katibu huyo alisema, mwananchi anaweza kumlalamikia Jaji mkuu, Jaji wa mahakama kuu, mtendaji mkuu, kadhi au naibu kadhi mkuu, ingawa sio kupitia kamati hiyo.

“Kamati hii imefungwa miguu na mikono kupokea malalamiko ya viongozi hao, maana wanangazi nyingine kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984,’’alieleza.

Nao wajumbe wa kamati hiyo Mohamed Bakar Shamata na kadhi wa mahakama ya wilaya  Mwanakwerekwe sheikh Idi Said Khamis, walisema ni fursa kwa wananchi, kuitumia kamati hiyo.

Walisema, wananchi wasiwe na sababu ya kulalamika pembeni, bali sasa serikali, imewaletea chombo huru kwa ajili ya kupokea malalamiko au kero wanazofanyiwa na watumishi wa Mahkama.



Kadhi huyo alieleza kuwa, wananchi hata wanapoona kuna tuhuma za rushwa au uvunji mwengine wa maadili, wasisite kufikisha malalamiko yao mahakama kuu Chake chake wa Pemba na Vuga kwa Unguja.

Baadhi ya wananchi kisiwani Pemba, wamesema kamati hiyo ni nzuri, ikiwa itakuwa huru na kufanyakazi zake bila ya kuingiliwa kama ilivyo kwa vitengo vyengine.

Hadia Khamis Chumu alisema, wataitumia kamati hiyo, hasa kwa vile wapo baadhi ya watendaji wamekuwa wakishindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo.

Jokha Mnubi Iddi alisema, anachoomba kwa wajumbe wa kamati hiyo, kuendelea kutekeleza wajibu wao kama sheria inavyoongoza.

Kamati hiyo yenye wajumbe watano wakiwemo wanawake wawili, ambayo imeasisiwa April 15 mwaka jana, wajumbe watadumu kwa miaka mitatu, na tayari imeshapokea malalamiko manne, kutoka kwa wananchi wakiwalalamikia watumishi wa mahkama.

Miongoni mwa majukumu yake ni kushughulikia kesi, tuhuma za rushwa, tabia isiyoendana na kanuni na maadili ya mahkama au kushindwa kutekeleza wajibu wake.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch