Skip to main content

WATAALAMU WA SHERIA WAIPA KAZI IDARA YA KATIBA NA MSAADA WA KISHERIA

 

           


 
                  

NA HAJI NASSOR, PEMBA

WATAALAMU wa sheria Zanzibar, wameitaka Idara ya Katiba na Msaada wa sheria Zanzibar, kuongeza jitihada za elimu ili kusaidia kubadili mawazo, mitazamo na uwelewa wa watu maskini, ili kuongeza matumizi ya huduma za msaada wa kisheria.

 Walisema, Idara inapaswa kuweka kipaumbele cha pekee cha kutoa mafunzo hayo, ili kuona walengwa wa mfumo wa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria ambao ni watu maskini wanafaidika nao.

Kwa mujibu wa tafsiri ya ripoti ya tathmini ya awali ya hali halisi ya msaada wa kisheria Zanzibar ya mwaka 2020, iliyotolewa na wizara ya Katiba na sheria, walisema azma ya uwepo wa msaada wa kisheria ni kwa watu wasio na uwezo.

Wataalamu hao kwenye ripoti hiyo walisema, suala la utoaji wa msaada wa kisheria linazingatiwa kuwa ni miongoni mwa viashiria vya msingi ya upatikanaji haki.

Walieleza kuwa, taifa lolote lile duniani haliwezi kufurahia uwepo wa baadhi ya haki za binadamu bila ya kunawiri mfumo wa utoaji wa msaada wa kisheria.

Aliyekuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, kwenye ripoti hiyo alisema wasaidizi wa sheria na watoa msaada wa sheria wanafanyakazi kubwa ya kuisaidia jamii kuwapa ufahamu wa sheria.

Wakili wa serikali Mwandamizi Afisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Ali Rajab, alisema bado watoa msaada wa kisheria hawajawafikia ipasavyo watu katika maeneo hasa ya vijijini, ambao wengi wao hawana uwezo wa kulipia gharama za mawakili.

“Jengine ambalo ni kasoro inaonekana watoa msaada wa kisheria wengi wao ni waajiriwa wa serikalini au sekta binafsi, hivyo hawana muda mwafaka wa kutoa huduma,’’alieleza.




Rais mstaafu wa chama cha mawakili Zanzibar Omar Said Shaaban, alisema sasa mawakili hawana tena mtazamo mbaya kwa watoa msaada wa kisheria, kama ilivyokuwa hapo mwanzo.

Wakili wa mahakama kuu Pemba Khalfan Amour Mohamed, alisema wananchi walio wengi waliopo Pemba, hawajafurahia utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kutokana na jiografia ya kisiwa chenyewe.

Aidha Mkurugenzi wa Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’ Jamila Mahamoud, alisema wasaidizi wa sheria hawana muda wa kutosha wa kuwahudumia watu katika maeneo yao.

“ZAFELA imegundua kuwa, wasaidi wa sheria waliopata mafunzo na ZLSC hawakai katika maeneo ambayo walipojisajili wakati wanaomba mafunzo hayo,’’alifafanua.

Katika ripoti hiyo, wataalamu hao wa sheria walipendekeza kuwa, wakati umefika sasa kuongeza ufahamu wa watoaji wa masaada wa kisheria ili kutambuliwa rasmi.

Hata hivyo walipendekeza kuwa, ni vyema watoa msaada wa kisheria kushirikiana kwa karibu na mawakili katika ofisi zao, ili kutoa huduma za kujitolea kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza hivi karibuni Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na msaada wa kisheria Zanzibar, Hanifa Ramadhn Said, alisema licha ya uchanga wa idara, wameshafanya makubwa, ikiwa ni pamoja na elimu kwa jamii.

“Hivi sasa karibu kila shehia tumeshaifikia, nab ado tunaendelea kukutana na jamii, ili kuwapa elimu na ushauri wa kisheria tena bila ya malipo,’’alieleza.

Ripoti hiyo ya tathmini ya awali ya hali halisi ya msaada wa kisheria Zanzibar, inaangalia taarifa za awali kuhusiana na historia, hadhi, asili ya shughuli za masaada wa kisheria hapa Zanzibar.

Ambapo ripoti hiyo, itasaidia kubainisha mambo yatakayoimarisha huduma za utoaji msaada wa kisheria pamoja na kupendekeza mfumo mzuri, utakaopelekea kupatika kwa urahisi kwa watu wote.

                      Mwisho

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch