Skip to main content

MATTAR AAHIDI KUZITATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI HATUA KWA HATUA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KATIBU Mkuu wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar Mattar Zahor Massoud, alisema changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa wizara hiyo Pemba, zitatatuliwa hatua kwa hatua, ili wafanye kazi kwenye mazingira rafiki.

Alisema, anayaelewa vyema mazingira wa tumishi walioko Pemba kwa kule kukaa kwa muda mrefu, akiwa kwenye nyadhifa tofauti, hivyo wizara itahakikisha inazitatua changamoto hizo.

Katibu Mkuu huyo, aliyasema hayo hivi karibuni, wakati akijitambulisha kwake na kuzungumza na watumishi hao, na kusema anachoomba ni umoja na mshikamano miongoni mwao.

Alieleza kuwa, baada ya kukutana na waratibu alielezwa changamoto kadhaa, ikiwemo suala la usafiri, kutoshirikishwa baadhi ya waratibu hasa uandaaji wa bajeti kuu, na kuahidi kuyafanyia kazi.

Alisema, suala la usafiri wa vyombo vya maringi mawili, wizara yenyewe itanunua kwa aina ya vipaumbele vyake, ili kuhakikisha zile Idara zinazohitaji, zinafanikiwa.

‘’Kwa upande wa vyombo vya maringi mawili hivi, wizara yetu itajitutumua na kununua taratibu, kila bajeti inapokuwepo, maana naelewa changamoto hizo,’’alifafanua.

Akizungumzia usafiri wa vyombo vya maringi manne, alisema tayari yapo mazungumzo na wenzao wa wizara ya Fedha, ili kuona wanawapatia usafiri huo.

‘’Unajua wenzetu wa wizara wa Fedha ni wasikivu, ikiwa utawaendea na maelezo mazuri yenye mchanganuo, twarajia kufanikiwa katika hili,’’alifafanua.

Kuhusu umoja na mshikamano, aliwakumbusha watumishi hao kujenga tabia ya kushirikiana katika kazi zao, ili kuwapa nafasi pana wananchi, wanapohitaji huduma.

‘’Isiwezekane ndani ya wizara moja, kunataasisi inahitaji vifaa ili kufanikisha, lakini isiazimwe na idara nyingine, jambo hilo ni baya na lisiwepo,’’alieleza.

Akizungumzia namna ya watendaji hao kuongeza elimu, aliitaka Idara ya Utumishi, kuwa na mpango madhubuti na endelevu, ambao utawahakikisha wafanyakazi wanasoma.

Alifafanua kuwa, kwenye kutafuta elimu hakuna kikomo wa umri, bali ikiwa kunamfanyakazi anataka kujisomea, ashauriane na Idara ya Utumishi na kukamilisha, ndoto yake.

‘’Niwahimize watendaji wa wizara hii, kujiandalia mazingira rafiki ya kuongeza elimu, tena sio tu kwa ajili ya kuongeza mshahara, bali kuongeza ujuzi wa kazi,’’alisema.

Mapema Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba, Mfamau Lali Mfamau, aliwasisitiza wafanyakazi, kufika na kurudi kazi kwa wakati, ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Alieleza kuwa, wapo baadhi ya wafanyakazi wamekuwa na tabia ya kuchelewa kazini na kuondoka kabla ya wakati, jambo linalotoa tafsiri mbaya, kwa jamii.

Wakati huo huo Ofisa Mdhamini huyo, aliwakumbusha wafanyakazi hao, wanapokuwa na changamoto za kiofisi kufuata ngazi moja baada ya nyingine, ili kulalamika.

Wafanyakazi hao, wameahidi kuyafanyiakazi, walioelezwa, kwani yanatoa viashirio vya utendaji kazi bora kwao.   

                       Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...