Skip to main content

WEMA YAWAANDAA WATOTO WA KIKE KUWA VIONGOZI BORA WA BAADAE

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ 

 

'DUNIA imebadilika...kwani ya jana sio ya leo'

 

Katika miaka ya sasa, wanaonekana wanawake wengi wanaojihusisha na masuala ya uongozi, katika sekta mbali mbali.

 

Ikiwa ni katika vikundi vya ushirika, uongozi kwenye jamii, shehia, majimbo na hata kwenye taasisi za umma na binafsi.

 

Hii ni kutokana na elimu inayotolewa kupitia vyombo vya habari na kwenye jamii, kuhusu ushirikishwaji wa wanawake kwenye masuala ya uongozi.

 

Na ndio maana hata mfumo wa elimu uliopo sasa, unatambua kwamba watoto wa kike wanapaswa kujengwa mapema kiongozi, ili kila hatua anayopitia aweze kujiamini na kuwa jasiri.

 

Tangu wakiwa skuli, wanafunzi wanajengewa uwezo wa kuwa viongozi bora na huwashirikisha wakike na kiume bila ubaguzi, lengo ni kutengeneza taifa lenye viongozi bora wa baadae.

 

Mwanafunzi Aisha Khamis Ayoub ambae ni Waziri wa Fedha skuli ya sekondari ya Idrissa Abdulwakil Kizimbani Wete anasema, mwanzo alikuwa anaogopa kugombea nafasi za uongozi, kwani alikuwa hawezi kuzungumza.

 

Baadae alijiamulia mwenyewe na kuona kwamba ni bora agombee nafasi hiyo, ambapo sasa anajiamini na anatekeleza majukumu yake vizuri aliyopangiwa.

 

Aisha malengo yake ni kugombea ubunge atakapomaliza masomo, ili aweze kutetea wananchi hasa wanawake kwenye mambo yanayowahusu, kwa ajili ya kujenga jamii iliyobora.

 


"Kwenye serikali ya wanafunzi tuna jukumu la kusimamia wanafunzi wote, tunawasaidia waalimu wetu majukumu, ingawa wanafunzi ni wakaidi lakini tunasuluhisha wenyewe linapotokezea tatizo," anaeleza.

 

Mwanafunzi Salum Khamis Salim wa skuli hiyo, anasema kitu chochote unatotaka kukianza unatakiwa uombe Mungu na baada ya kukipata basi ukifanyie kazi ipasavyo huku ukiwa na nidhamu.

 

Anasema, wao wamejengeka kinidhamu na wanafunzi wanaowaongoza wanawajengea mazingira bora ya kuwa na nidhamu, ambapo hukaa nao na kuwaelimisha.

 

"Serikali ya wanafunzi inawasaidia sana waalimu kwenye paredi, usafi na kusimamia wanafunzi wenzao, ili walimu wafanye shughuli nyingine, ingawa changamoto zinazotukabili ni uhaba wa vifaa vya kufanyia usafi,’’anafafanua.

 

Rais wa skuli hiyo Juma Said Mohamed anasema, wanawake wanapewa fursa za kugombea, ingawa hawataki kwani wanaogopa.

 

"Nawashawishi sana kwa sababu utendaji wao ni mzuri na wanawajibika ipasavyo, hivyo nimekuwa nikiwashari mpaka wengine wanakubali," anasema.

 

Anasema serikali yao inaviongozi 25 wanawake watano na wanaume 20, ingawa wanawake wanahitaji kuongezeka, ili kazi niende vizuri.

 

Mwanafunzi wa skuli ya sekondari Limbani Shuwekha Khamis Mohamed anaeleza kuwa, wanawake wanapokuwa viongozi wanasaidia, upatikanaji wa haki kwa wote na kupata kujiamini.

 

Ingawa nafasi yake ni ya kuteuliwa, lakini anafanya kazi kwa ushirikiano mzuri na waalimu pamoja na wanafunzi, huku akiendelea kujifunza mambo ya uongozi.

 

"Nimepata mafanikio makubwa, kwani wanafunzi wananiheshimu, nimejenga upendo na waalimu pamoja na wanafunzi, sasa najiamini kwenye kazi zangu,"anasema.

 

Rais wa skuli hiyo Ahmed Hamad Mabwana anaeleza, ipo haja kwa wanawake kujengewa uwezo mapema, kuhusu uongozi ili kuwe na hali ya usawa.

 

"Ni vyema washirikishwe ili wasidharauliwe kwani kwa sasa uwezo wao sio mkubwa, ingawa kupitia Serikali ya wanafunzi naamini watakuwa vizuri," anasema.

 

Changamoto inayowakabili ni tabia ya wanafunzi kuwa wajeuri na kiburi, jambo ambalo linarudisha nyuma juhudi zao, ingawa ndizo zinazowajenga ujasiri na kujua aina ya watu wanaowaongoza.

 

Wamekuwa wakipewa elimu mara kwa mara, ambayo yanawajenga kuwa viongozi bora wa sasa na baadae, watakapokwenda kwa jamii.

 

Mwalimu Mlezi wa serikali ya wanafunzi skuli ya sekondari Limbani Maryam Omar Mohamed anasema, Serikali ya wanafunzi inawaandaa watoto kuwa viongozi kwa asilimia 75, kwani wanawapa majukumu mazito, ambayo wanayatekeleza kwa ufanisi.

 

"Wana uwezo wa kusimamia na kujieleza, tunaamini watakuwa viongozi bora kwa sababu, wanawasaidia waalimu majukumu yao, pia wanawaelewesha wanafunzi wenzao mara kwa mara," anasema.

 

Anafafanua, wanashughulikia paredi, usafi, inategemea na nafasi yake aliyopangiwa, hivyo wanawajibika vizuri.

 

"Umuhimu ni mkubwa wa serikali ya wanafunzi kwa sababu wanatupunguzia baadhi ya majukumu, uzoefu wa wanafunzi, kuwasaidia wanafunzi wenzao, ‘’anasema.

 

Serikali ya wanafunzi katika skuli hiyo ina jumla ya viongozi 14, wanawake tisa (9) na wanaume watano (5).

 

Mwalimu anaesimamia serikali ya wanafunzi skuli ya sekondari ya Idrissa Abdulwakil Kizimbani, Ghalib Said Mohamed, anasema lengo lao ni kumfanya mwanafunzi, aweze kujiamini kwani wanamfuatilia jinsi anavyoweza kuwajibika.

 

"Uongozi huo hauwakwazi wanafunzi bali unawajenga vizuri kiakili kwa sababu hawatolewi kwenye vipindi vya masomo, muda wa kusoma wanasoma na muda wa kuwajibika kiuongozi wanawajibika," anasema.

 

Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim anasema, mtaala wao kuanzia maandalizi mpaka sekondari ya juu, kuna masomo maalumu yanayoongeza vipaji na maarifa.

 

Mtaala wao umekuja na somo la historia na maadili, linalosaidia kutengeneza viongozi, kwani mada hio inaimarisha uzalendo, historia na maadili, ambavyo ni vitu muhimu katika uongozi wa baadae.

 

Wanawasaidia zaidi watoto wa kike kwa kuimarisha dakhalia, ambapo wamekubaliana wizara, kwamba wanafunzi watakaofaulu vizuri masomo yao na kupata daraja la A na B, wataweka skuli maalumu za michepuo, hivyo mabinti wanafaidika zaidi.

 

Mdhamini anafafanua, hiyo ni kwa sababu katika skuli za kawaida za kwenda na kurudi, watoto wa kike wanapata vikwazo vingi zaidi, ambavyo vinawanyima nafasi ya kufanya vizuri kwenye masomo.

 

"Kwa mfano wanalazimika kutembea masafa marefu na mazingira mengine ni hatarishi, pia baadhi ya familia tamaduni zao haziwapi nafasi ya kusoma, wanapofika nyumbani wanakuwa ni mama wa nyumba," anaeleza.

 

Mdhamini huyo alitaja jambo jingine linalowaandaa watoto wa kike kwamba, ni namna ya uchawanyaji wa skuli katika visiwa vidogo vidogo na maeneo tengefu, kwani wasichana walikuwa wakipata shida kuvuuka ingawa baada ya kujenga skuli hizo, kikwazo hicho kimewaondokea.

 

"Tumeimarisha utaratibu wa ushauri nasaha kwa kuwapa mafunzo walimu na skuli zilizojengwa tumeweka vyumba maalumu kwa ajili ya walimu wa ushauri nasaha," anafafanua.

 

Kumbe uwepo wa vyumba maalumu vya kubadilishia nguo, wakiwa katika mizunguko yao ya heidhi, ili wapate fursa ya kusoma kwani kufanya hivyo ni kutengeneza mama na kiongozi bora wa baadae.

 

Anaeleza, wamekuwa wakishirikiana na taasisi mbali mbali za serikali na binafsi ikiwemo chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar (TAMWA),  na chama cha Wanasheria Zanzibar (ZAFELA) katika kuimarisha uongozi kwa wanafunzi.

 

Mdhamini huyo anafafanua, kwa sasa mabadiliko yapo kwani watoto wa kike wa miaka hii wana uwezo mkubwa ukilingalisha na mwanafunzi msichana wa miaka ya 70 na 80.

 

"Kwanza ufaulu katika masomo ya sayansi umeimarika kwa wanafunzi wa kike, na kilichosaidia ni kujiamini kwao kutokana na walivyojengwa kuwa na uwezo wa kuzungumza popote bila ya woga," anasema.

 

 

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia Pemba ‘PEGAO’ Hafidh Abdi Said, ni jambo jema lililofanywa na wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kwa kuwaandaa watoto mapema kuujua uongozi kupitia klabu mbali mbali skulini.

 

 

Anasema, wanaamini kwamba lengo lao la kufikia 50 kwa 50 katika safu ya uongozi yatafanikiwa, kwani elimu wanayoipata watoto wakiwa skuli, itawasaidia kuwajengea ukakamavu na kujiamini.

 

"Wasichana wataanza kujiamini mapema kwani nafasi wanazopewa skuli ni kubwa na zinawajengea ujasiri wa kuzungumza mbele ya  jamii, na kupata uzoefu wa kuongoza akiwa mdogo.

 

 

                              MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...