Skip to main content

VIKUNDI 16 VYA KUWEKA NA KUKOPA VYA UNGUJA, VYAPEWA MAFUNZO YA USIMAMIZI BIASHARA

 



NA MWANDISHI WETU, PEMBA @@@@

WANACHAMA 25 kutoka vikundi 16 vya kuweka na kukopa katika Wilaya ya Kusini Unguja wamepatiwa mafunzo ya siku mbili ya kuchagua, kupanga na kusimamia biashara.

Mafunzo hayo yalitolewa chini ya Programu ya Mashirikiano ya pamoja kwa ajili ya haki za Watu wenye Ulemavu (CADiR) inayotekelezwa na Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ), Shirikisho la Jumuiya za Watu wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) na Jumuiya ya wasioona Zanzibar (ZANAB) kwa ushirikiano mkubwa na Shirika la Watu Wenye Ulemavu la Norway (NAD).

Amapo jumla ya washiriki 16 wa mafunzo hayo ni watu wenyeulemavu na 9 ni walezi na wasimamizi wa Watoto wenyeulemavu, ambapi wanatarajiwa kuyafikisha maarifa haya kwa wanachama wenzao, ili kila kikundi kinufaike pamoja na kuimarisha biashara zake.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo,Aziza Ismail ambae ni Mratibu wa program ya CADiR kutoka NAD, alisema taasisi zinazoshirikiana katika programu hii zina matumaini makubwa kuwa mafunzo haya yatawawezesha wawakilishi wa vikundi kupeleka elimu waliyoipata kwa wenzao,ili kusaidia wanachama wote kuchagua biashara bora na zenye tija.

“Kwa vile miongoni mwa malengo makuu ya program hini kuwawezesha watu wenyeulemavu kuinuka kiuchumi na kupata kipato rasmi, tunaamini mafunzo haya yatasaidia kikamilifu kulifikialengo hili”, alisisitiza Mratibuhuyo.

Mkufunzi wamafunzo hayo, Muhidini Ramadhan kutoka TAMWA ZNZ alisema, hali ya umasikini inaweza kupungua kwa watu wenye ulemavu iwapo wataelimishwa juu ya ujuzi na miradi ya kiuchumi yenye tija.

Nae Meneja wa Programu kutoka TAMWA ZNZ Nairat Ali, aliongeza kua mafunzo haya ni muhimu kwa ajili ya kuwasaidia wanachama kupanga na kuchagua biashara zenye tija ili vikundi viwe endelevu na viweze kujitegemea kiuchumi.

Kwa upande wake ndugu Khamis Ali, Afisa Program kutoka ZANAB, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kujifunza kwa umakini mafunzo hayo ili waweze kuchagua biashara sahihi zitakazowawezesha kupata mikopo na kuweza kurudisha kwa wakati.



Washiriki walijadili na kuandika mipango ya biashara, baadhi wakieleza ndoto zao za kukuza biashara ndogo ndogo walizo nazo, ikiwemo kilimo, ufugaji, kufungua maduka na ushonaji.

Akizungumza kwaniaba ya washiriki wenzake, Yusra Ali Hassan ambaye ni Msaidizi Katibu wa kikundi cha "Mtu ni Utu"cha Kajengwa, ame wapongeza waandaaji wamafunzo hayo na kusema kwamba, yamewapa muongozo mzuri wa namna ya kupanga biashara na kutumia vizuri fedha katika kukuza biashara zao.

Kupitia mafunzo haya tumejifunza kupanga matumizi kwa uangalifu na kuweka mipango thabiti ya biashara, binafsi nimeona namna biashara ya ushonaji inavyoweza kukua zaidi nikiwa na maarifa haya mapya,” amesema Yusra.

Mafunzo hayo ya siku mbili yamefanyika katika ukumbi wa walimu Kitogani, ikiwa  ni sehemu ya utekelezajiwa program ya CADiR katika eneo la uwezeshaji kiuchumi, ambalo linalenga kuanzisha na kuimarisha vikundi vya watu wenye ulemavu vya kuweka na kukopa katika wilaya 11 za Unguja na Pemba.

                                                                    MWISHO

 

Comments