Skip to main content

DC MKOANI MGENI RASMI MASHINDANI TAHAFIDH QUR-AN WAMBAA


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@

MKUU wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakari, kesho  anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika mashindani ya tano ya tahafidhil-quran, ya kanda ya Wambaa wilayani humo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa Jumuiya ya tahafidhil qur-an kanda ya Wambaa, Mwalimu Abdalla Haji Ali, alisema tayari maandalizi ya shughuli hiyo, yameshakamilika.

Alisema, mkuu huyo wa wilaya, atawashuhudia wanafunzi wakishindana kwa juzuu ya kwanza, pili, tatu, tano, saba, 10 na 15 wakiwemo wanafunzi wa kike na kiume.

Alieleza kuwa, mashindani hayo ya aina yake kwa mwaka huu, yanatarajiwa kufanyika msikiti wa Ijumaa, uliopo kijiji cha Chumbageni Wambaa wilaya ya Mkoani Pemba.

Alisema, baada ya majaji kukamilisha kazi yao hiyo na kutoa matokeo, mgeni rasmi huyo atatoa zawadi ikiwemo fedha taslimu, kwa washindi na washiriki wote 42.

ā€˜ā€™Ni kweli asubuhi hii, ndani ya msikiti wa Ijumaa Chumbageni, mkuu wetu wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakari, atayashuhudia mashindani ya tano ya tahafidhi qur-an, yanayoandaliwa na jumuia yetu,ā€™ā€™alifafanua.

Akizitaja madrassa saba zitakazoshiriki kwa mwaka huu, Katibu huyo, alisema ni pamoja na almadrassatul- raufu rrahim ya kijiji cha Andikoni, allah kadiri ya kijiji cha Wambaa.

Madrassa nyingine zilizothibitisha kushiriki ni minatu rrahman ya Kwazani, nur-ddin ya Ndongoni, hidayatul- islamiya ya Andikoni, kaafur ya Tumbi na imaniya ya Chumbageni.

Katika hatua nyingine, Katib huyo aliwaomba waumini wa dini ya kiislamu wa shehia za Wambaa na Chumbageni na shehia jirani, kuhudhuria katika mashindani hayo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Hassan Othman Khamis, aliwashukuru waumini wa dini ya kiislamu na mashinrika mingine, kwa kutoa michango yao, iliyofanikisha kufanyika kwa mashindani hayo.

Alisema, michango ya wazazi, walezi, viongozi wa jimbo la Chambani, ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Mkoani, waalimu wa skuli za Tumbi, Kunguni, Wambaa na baadhi ya wawekezaji, imesaidia kwa kiwango kikubwa.

Mwalimu mkuu wa almadrassatui Allah kadiri ya Wambaa Awesi Abdalla Ali, alisema maandalizi kwa upande wake, yameshakamilika ikiwemo wale wanafunzi wa juzuu ya kwanza hadi ya 10.

Mshika fedha wa Jumuiya hiyo, Ali Juma Khamis, alisema walipanga kukusanya shilingi milioni 1.6 kwa ajili ya zawadi za washindi na sadaka kwa washiriki, ingawa wamefanikiwa kukukusanya shilingi milioni 1.34.

ā€˜ā€™Kwa fedha tulizokusanya mwaka huu, zimesaidia kwa kiwango kikubwa kufanikisha shughuli yetu, ikilinganishwa na mwaka jana, jambo ambalo tunaona tumepiga hatua,ā€™ā€™alifafanua.

Baadhi ya wananchi wa shehia za Chumbageni na Wambaa walisema, wamefurahishwa kwa kukamilika kwa maandalizi hayo, na kuwaomba wenzao kuhudhuria.

Fatma Abuu Fakih, alisema ni vyema kwa wazazi na walezi, kushiriki ili kuwanga mkono watoto wao, kuzidi kukihifadhi kitabu cha Muumba.

Raya Juma Khamis na Asha Haji Ali, walisema ni wakati wao wazazi, kuwashajiisha watoto namna bora ya kukihifadhi kitabu cha Allah, ili kikawe muombezi kwao.

Hii ni mara ya tano, kwa Jumuia hiyo tahafidhi qur-an kanda ya Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, kuendesha mashindani hayo, ambapo kwa mwaka jana ilihusisha madrassa sita pakee.

Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...