Skip to main content

Posts

Showing posts from 2025

WAZIRI MASSOUD: MAPINDUZI YA ZANZIBAR NDIO MATOKEO YA MAENDELEO YALIOPO SASA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Uvuvi na Uchumi wa Buluu Zanzibar, Massoud Ali Mohamed, amewataka wananchi kuendelea kuyathamani Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, kwani ndio msingi wa maendeleo yaliopo. Waziri Massoud, alitoa raia hiyo jana, wakati alipomaliza shughuli za ufunguzi wa kituo cha kisasa cha ununuzi wa karafuu, eneo la Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za miaka 62 ya mapinduzi. Alisema kuwa, mapinduzi sio hadithi ya kuvutia pekee, bali ni kuwepo kwa maendeleo kila sekta, kama ilivyokuwa azma ya waasisi wa taifa hili. Alieleza kuwa, kwa mfano Kiwani iliyokuwepo kabla ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 na ya sasa ni tofauti, kwa kuwepo miundombinu ya kisasa, kwenye sekta ya afya, elimu, maji safi na salama na barabara. Alieleza kuwa, hayo ndio thamani na umuhimu wa kufanyika kwa mapinduzi hayo, na sasa ipo haja kwa wananchi na hasa wapenda maendeleo, kuyathamini na kuyaenzi kwa nguvu zao zote. ‘’Niwatake wanan...

WAZIRI PEMBE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SOKO KENGEJA, ATOA NENO

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Riziki Pembe Juma, amewataka wafanyabiashara wa Kengeja wilaya ya Mkoani, kuacha kuuza biashara zao pembezoni mwa barabara, na badala yake wayatumie masoko yanayojengwa. Waziri Pembe alitoa raia hiyo jana, wakati alipomaliza shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi la soko la kisasa, la sokoni Kengeja wilayani humo, ikiwa ni shamra shamra za miaka 62 ya mapinduzi. Alisema kuwa, mapinduzi yalifanyika kwa dhamira kadhaa, ikiwemo kuwakomboa wajasiriamali na wafanyabiashara, ikiwemo kuzipandisha hadhi bidhaa zao, na kuzihamishia sokoni kutoka pembezoni mwa barabara. Alieleza kuwa, utamaduni wa kufanyabishara katika mazingira hatarisha ikiwemo pembezoni mwa barabara, kwenye misingi ya maji taka, huu sio wakati wakati wake tena, na badala yake waingie masokoni. Waziri huyo alieleza kuwa, hasa ndani ya utawala wa serikali ya awamu ya nane, imekuwa ikifanya kila juhudi kuhakikisha wajasirimali na wafanyabiashara, wa...

MICHEWENI WATAKA UTAMADUNI WA JANDO UENDEE ILI WANAUME WAWE WAKAKAMAVU, KUEPUKA UGONJWA WA MISHIPA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   JANDO ni kumkata mtoto au kumfanyia tohara kwa kuondosha gozi la juu kwenye uume.   Jando au tohara ni kitu cha lazima kwa wanaume hasa jamii ya waislamu kwani humuweka katika hali ya usafi na usalama katika afya yake.   Pamoja na kuwa jando/ tohara ni lazima kwa vijana wa kiume na watoto wa kiume, lakini baadhi ya vijiji walifanya kama utamaduni maalumu, hasa pale walipoutekeleza kwa muda maalumu na kuwakusanya pamoja huku zikiambatana na sherehe.   Na kila sehemu walikuwa na utaratibu wao wa kuwatia watoto wao wa kiume jandoni, ambao ulikuwa ni utamaduni maalumu wanaojiwekea.   Wanajamii wa vijiji vya Micheweni Pemba, ni miongoni mwa watu ambao, jando walilifanya kama utamaduni kwa kuwakusanya watoto wa kiume na kuwaweka sehemu moja, huku kukifanyika shughuli mbali mbali za kimila zilizoambatana na sherehe baada ya kupona kidonda.   Hamad Mbwana Shaame mkaazi wa shehia ya Majenzi Wilaya ya Mic...

MATTAR AAHIDI KUZITATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI HATUA KWA HATUA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KATIBU Mkuu wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar Mattar Zahor Massoud, alisema changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa wizara hiyo Pemba, zitatatuliwa hatua kwa hatua, ili wafanye kazi kwenye mazingira rafiki. Alisema, anayaelewa vyema mazingira wa tumishi walioko Pemba kwa kule kukaa kwa muda mrefu, akiwa kwenye nyadhifa tofauti, hivyo wizara itahakikisha inazitatua changamoto hizo. Katibu Mkuu huyo, aliyasema hayo hivi karibuni, wakati akijitambulisha kwake na kuzungumza na watumishi hao, na kusema anachoomba ni umoja na mshikamano miongoni mwao. Alieleza kuwa, baada ya kukutana na waratibu alielezwa changamoto kadhaa, ikiwemo suala la usafiri, kutoshirikishwa baadhi ya waratibu hasa uandaaji wa bajeti kuu, na kuahidi kuyafanyia kazi. Alisema, suala la usafiri wa vyombo vya maringi mawili, wizara yenyewe itanunua kwa aina ya vipaumbele vyake, ili kuhakikisha zile Idara zinazohitaji, zinafanikiwa. ‘’Kwa upande wa vyombo ...

UIMARISHAJI MASLAHI NI HATUA YA KUMUANDAA MSTAAFU MTARAJIWA "GORA"

    NA  MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ NAIBU Katibu Mkuu wa Utumishi na Utawala bora Zanzibar Omar Haji Gora, amesema kupandishwa kwa mshahara   kwa   watumishi wa   Umma katika serikali ya awamu ya nane ni miongoni mwa juhudi za serikali za kuwaandalia mustakbali mzuri wa maisha watumishi baada ya kustaafu. Alisema hayo katika ufunguzi wa mafunzo ya maandalizi ya kustaafu kwa wastaafu watarajiwa watakaolipwa   mafao yao ya kustaafu kazi na mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF, yaliofanyika katika ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake Pemba. Alisema katika kuhakikisha watumishi wa umma wanakua na mustakbali nzuri wa maisha yao baada ya kustaafu serikali imechukua juhudi kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wa serikali, kupandisha pensheni, pamoja na kutoa mafunzo ya maandalizi kwa wastaafu ili kuweza kupata uelewa   wa namna bora ya kujiandalia mazingira ya kuyakabili maisha baada ya kustaafu. ...

JAMII YATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI KUKABILIANA NA HAKI YA TABIA ZA NCHI

  NA SALMA OMAR, PEMBA @@@ ANGOZA kwa kushirikiana na Mashirika ya kiraia pamoja na serikali, zimeiasa   jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na changamoto za haki ya tabia ya nchi. Hayo yamesemwa katika mkutano wa mafunzo na majadiliano yaliyoshirikisha jamii na taasisi mbalimbali zikiwemo asasi za kiraia, pamoja na wawakilishi kutoka serikalini katika ukumbi wa Samail Gombani Chake chake Pemba. Mwenyekiti wa ANGOZA Hassan Khamis Juma, amesisitiza jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na haki za tabia ya nchi, ikiwemo kujiepusha na uharibifu na uchafuzi wa mazingira. Alieleza kua kwani, kufanya hivyo kunaweza   kupelekea athari kubwa katika jamii na kusababisha maafa baadae, na jamii kuishi katika mazingira magumu. ‘’Niwaombe sana wanajamii, kwanza waziunge mkono asasi kama ANGOZA, maana zinakuwa na wajibu wa kuhakikisha wanawakinga wananchi na majanga kadhaa, yakiwemo ya athari za mazingira,’’alisema. Kwa upande wake, mwakilishi kuto...