'Anasema mwaka huu ndio aliopangiwa na Mungu kuingia jimboni kugombea, ...awaomba wananchi kumchagua' IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ "Alienipita kwa kura moja 2020, nimempita kwa kura 62 kwenye kura za maoni mwaka huu 2025, hivyo nimeshinda kwa kishindo," Maneno hayo ya furaha yalimtoka mgombea uwakilishi Jimbo la Tumbe kupitia chama cha Mapinduzi CCM Salma Khamis Tumu wakati akizungumza na mwandishi wa makala hii huko kijiji kwao. Salma mwenye umri wa miaka 53 mkaazi wa shehia ya Tumbe Magharibi anasema, ameamini kwamba riziki ya mtu haiendi kwa mwengine bali siku ikifika, itamfika tu mwenyewe. Pamoja na kushindwa kwenye kura za maoni kwenye uchaguzi uliopita wa mwaka 2020, lakini hakukata tamaa bali ajijipanga kugombea tena 2025, ambapo alipitishwa kwa kura 134 huku mpinzani wake ambae ni mwanamme akijipatia kura 72. Mgombea huyo anasema, hizo ni baraka za Mungu kumjaalia kupita kwenye nafasi hiy...