Skip to main content

Posts

Showing posts from 2025

ZURA YAWATAKA WAANDISHI KUTOA ELIMU MATUMIZI SAHIHI YA UMEME KWA WANANCHI

NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@  KAIMU Mkuu kitengo cha uhusiano  Mamlaka ya udhibiti wa huduma ya maji na nishati Zanzibar (ZURA)  Shara Chande Omar amesema mamlaka itaendelea kuandaa utaratibu pindi tu inapotokea mabadiliko ya bei  elekezi kwa matumizi za huduma ya maji,  nishati ili Kuwaondoshea usumbufu wananchi.  Ameyasema hayo  akitoa ufafanuzi wa bei mpya ya umeme katika kikao na  wandishi wa habari mbali mbali huko kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi za ZURA Kibirinzi chake chake Pemba Amesema lengo la kikao hicho na wadau wa habari ni  kuwafikishia wananchi tarifa hiyo ya mabadiliko ya bei ya umeme ambayo imeanza kutumika kwa sasa.  " Wandishi wa habari ndio Wenye jukumu la kuwafikishia wananchi tarifa  sahihi pindi tu itapotokea mabadiliko ili kuepuka malalamiko na kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya umeme. "alisema kaimu huyo.  Aidha amesema kuwa mamlaka imeanda utaratibu wa kuwasajili mafundi wa umeme kwa kuwapatia vib...

IDARA YA KATIBA: ‘’KUJITOLEA KWA WASAIDIZI WA SHERIA NI TAKWA LA KISHERIA’'

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa Divisheni ya Katiba na Sheria Pemba Bakari Omar Ali, amewasisitiza wasaidizi wa sheria, kukumbuka kuwa ,   bado dhana ya kujitolea kwa aina ya kazi yao hiyo, itabakia pale pale licha ya changamoto walizonazo. Alisema, kwa mujibu wa sheria inayowaongoza, ni kosa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria na kisha kuomba malipo kwa m wananchi husika. Mkuu huyo wa Divisheni, aliyasema hayo leo Febuari 09, 2025  ukumbi wa mikutano wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ wakati akitoa maoni yake, baada ya kuwasilisha matokeo ya awali ya utafiti kwa wasaidizi wa sheria ,   kisiwani humo. Alisema, ijapokuwa sasa wapo wanaodai malipo kama baraka ya kufanyakazi zao, lakini bado sheria haitambuwi uwepo wa posho kama motisha wa kufanya kazi zao. Alieleza kuwa, msingi mkuu wakati wa lipo omba kazi hiyo na sasa ikiingizwa ndani ya sheria yao, ni kufanyakazi kwa njia ya kutolea, na hasa kwa wananchi wanyonge na makundi maa...

WADAU WALIA NA SHERIA TUME YA UTAANGAZAJI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SASA ni miaka 26 tokea kuasisiwa kwa sheria ya Tume ya Utangaazaji Zanzibar nambari 7 ya mwaka 1997, licha ya kujumuisha na marekebisho yake. Sheria hii, imekuja kusimamia, kuangalia mwenendo wa vyombo vya habari Zanzibar hasa redio, televisheni na vile vya kisasa vyenye kurusha maudhui yao mtandaoni. Sheria hii yenye vifungu 30, vilivyobebwa na sehemu sita kuu, inavyovifungu kwa hakika sio rafiki, kuelekea uhuru kamili wa habari hapa Zanzibar. SHERIA KWA UJUMLA Kama ilivyo sheria nyingine zote, kwenye sehemu ya kwanza imeundwa na vifungu vitatu, maana kile cha nne, kimefutwa na kati ya hivyo kimoja kinatoa jina la sheria na maana ya maneno. Kwa mfano,  mtangaazaji ni mtu ambaye amepewa leseni chini ya sheria hii ya kutoa huduma za utangaazaji katika vyombo vya habari. Kwenye sehemu ya pili ya sheria hii, yenyewe imeundwa na vifungu kuanzia cha tano (5) hadi cha 10, na kubwa zaidi lililopo ni pamoja na uanzishwaji wa Tume ya Utangaazaji Zanzibar. Je...

T.O.T WAPEWA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA TABIANCHI

  Wanawake  wameombwa kuvitumia vyombo vya habari ipasavyo kwa lengo la kutangaza kazi wanazozifanya katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Akifungua mafunzo ya siku moja ya kuwajengea uwezo wanawake viongozi  kupitia mradi wa ZanzAdapt Mkurugenzi wa TAMWA ZNZ Dkt Mzuri Issa Ali amesema wanawake wanafanya mambo mengi katika jamii ila bado mchango wao haujatambulika kama ilivyo kwa wanaume hivyo kuvitumia vyombo vya habari kutawezesha kutambulika na kujitangaza kwa haraka hasa kupitia mitandao ya kijamii. Amesema historia ya Tanzania na Zanzibar kwa ujumla haioneshi mchango ama juhudi za wanawake kwa sababu wanawake bado hawajawa na ujasiri na uthubutu wa kutumia vyombo vya habari kwa usahihi. “Wanawake wanafanya mambo mengi katika jamii na kujitoa zaidi, sasa wakati umefika kueleza changamoto na mambo yanayowahusu kupitia vyombo vya habari ili kupatiwa ufumbuzi,” Dkt Mzuri. Mkufunzi katika mafunzo hayo Sophia Ngalapi amesema vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya ...

KATIBU MKUU ABEDA ASAINI AGENDA YA MASUALA YA WANAWAKE KUHUSU AMANI, USALAMA

  NA MWANDISHI WETU, UNGUJA KATIBU Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Abeida Rashid Abdallah amesaini Mpango wa Taifa wa kushughulikia Utekelezaji wa Agenda ya masuala ya Wanawake, kuhusu Amani na Usalama ulioandaliwa mahsusi kwa ajili ya kutekeleza Azimio Na:1325 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Hafla ya utiaji saini imefanyika jana ofisini kwake Kinazini Unguja, amesema Mpango huo ni heshima kwa Tanzania kwani imeonesha wazi kukubali na kutekeleza Azimio hilo la Umoja wa Mataifa la kuhakikisha Wanawake wanakua  katika amani na usalama wakati wote. Amefahamisha kwamba Azimio hilo lilipitishwa tarehe 31 mwezi Oktoba mwaka 2000, kwa lengo la kuhimiza umuhimu wa nafasi ya wanawake katika kuzuia na kutatua mizozo, mashauriano ya amani, ujenzi wa amani, ulinzi wa amani, hatua za usaidizi wa kibinadamu na ujenzi baada ya mizozo na kusisitiza umuhimu wa ushiriki sawa katika uendelezaji wa amani na usalama duniani. Ameeleza Wizara ya Maendeleo ya Jam...

MWAMBE MKOANI IN PEMBA ISLAND: CHILDREN FORCED TO A LIFE OF STONE CRUSHING

By HAJI NAASSOR, PEMBA@@@@   It is about an hour-and-a-quarter drive from Chake Chake town to Mwambe village in Mkoani District in the Southern Region of Pemba Island within Zanzibar country.   The village of Mwambe is located in a rocky area but is more fertile than the surrounding villages. It has three shehias, known here as Jombwe, Mwambe and Mchakwe.   The village has a population of 19,525,(2022 census) half of them children. Its people survive on agriculture growing beans for local consumption, and citrus and bananas to sell.   It has its own primary and secondary schools and a health centre that provides various medical services.   Besides, agriculture, the villagers are also engaged in fishing, stone crashing and mining. Since Mwambe is rocky, most people, especially the elderly and children, are involved in quarrying stone for sale.   The stone crashing business has forced many children to abandon school to earn money but this is taking its toll o...