Skip to main content

Posts

Showing posts from 2025

DISEMBA 17, 2025 MIMI 'NA ZU' TUNAJAMBO MUHIMI SANAAAAAA HILI HAPAAAA

UONGOZI WA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) UNAYOFURAHA KUWAALIKA WAHITIMU WOTE WA MWAKA WA MASOMO 2024/2025, PAMOJA NA WAZAZI, WALEZI, NDUGU, JAMAA, MARAFIKI, NA WADAU WOTE WA MAENDELEO YA ELIMU, KUSHIRIKI KATIKA MAHAFALI YA 23 YA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU). MAHAFALI HAYO YANATARAJIWA KUFANYIKA SIKU YA JUMATANO YA DISEMBA 17, MWAKA 2025, KATIKA KIWANJA CHA CHUO KIKUU TUNGUU KIBELE UNGUJA, KUANZIA SAA 2: 00 ASUBUHI. AMBAPO KATIKA MAHAFALI HAYO PAMBE, MGENI RASMI ANATARAJIWA KUWA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK. HUSSEIN ALI MWINYI. UONGOZI WA CHUO UNAWASHAURI WAHITIMU WOTE, KUKAMILISHA TARATIBU ZOTE IKIWA NI PAMOJA NA KUCHUKUWA MAJOHO KUANZIA SIKU YA ALHAMISI YA TAREHE 11 HADI TAREHE 15. MAZOEZI YA MAHAFALI 'REHASAL' ITAFANYIKA TAREHE 16 DISEMBA, 2025 SAA 2:00 ASUBUHI. HIVYI BASIII......WATU WOTE WANAKARIBISHWA KUSHEREHEKEA MAHAFALI HAYO. KUMBUKA KUWA......CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) NI CHEM CHEM YA MAADILI NA TAALUMA. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA SIMU...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA MCT, TAMWA, ZPC, WAHAMAZA, THRDC

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI SIKU YA HAKI ZA BINADAMU DUNIANI 2025   Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaungana na wanaharakati, wanahabari, na watetezi wa haki za binadamu duniani kote,  kuadhimisha siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka.   Kaulimbiu ya mwaka huu, haki za binadamu kama “Mahitaji ya Kila Siku”, inasisitiza kuwa haki hizi lazima zilindwe bila kusuasua kila siku, kwa kila mtu, na katika kila mazingira.  Katika maadhimisho ya mwaka 2025, ZAMECO inasisitiza kwamba uhuru wa kupata na kutoa taarifa ni nguzo muhimu ya utawala bora na msingi wa kulinda haki nyingine zote za binadamu.  Haki hii haipaswi kutazamwa kama ridhaa ya mamlaka bali kama wajibu wa kikatiba na kimataifa unaopaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekelezwa.  Tunawakumbusha wadau wote kuwa tangu kupitishwa kwa Tamko la Ulimwengu la Haki za Binadamu (UDHR) mwaka 1948 uhuru wa kujiele...

WATU WENYE ULEMAVU PEMBA WAKASIRISHWA KUBANDIKWA MAJINA 'FEK'

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ S HERIA ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari   8 ya 2022 kifungu cha 45 kinakemea udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu. Kwa kueleza mtu yeyote atakae mdhalilisha au kumkandamiza mtu mwenye ulemavu, kwa kumuita jina lisilofaa kutokana na aina ya ulemavu wake, atakua ametenda kosa. “Atakae tiwahatiahi kwa kufanya kosa hilo, atalipa faini isiyopungua shillingi 100,000 na isiozidi shillingi million 1, au kifungo kwa kipindi kisichopungua mienzi miwili au vyote wiwili”, kimefafanua. Mkataba wa kimataifa wa watu wenye ulemavu wa mwaka 2006 ibara yake ya 17, inazungumzia kuhusu kuheshimu tofauti za kimaumbile. “Kila mtu mwenye ulemavu anayo haki ya kuheshimiwa kwa ukamilifu wake kimwili na kiakili kwa misingi ya usawa na watu wengine,” imeeleza ibara hiyo. Ieleweke kua katika jamii, lugha ina nguvu kubwa katika kuunda mitazamo na hisia kuhusu makundi mbali mbali ya watu.   Hata hivyo, matumizi ya majina na lugha zisizofaa, yanawez...

ELIMU MJUMUISHO KEKI YA TAIFA INAYOLIWA NA WANAFUNZI WASIOONA, WAIPA TANO SMZ

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ TUPO katika ulimwengu ambao mara nyingi mafanikio ya mtu kimaisha huhusishwa na elimu. Sio tu ya utambuzi wa mazingira, bali na ile ipatikanayo   darasani. Kupata elimu hiyo kwa Zanzibar si changamoto hasa baada ya kufanya mapinduzi yake mwaka 1964, na kuanza kujitawala. Kwani katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 10 (f), kinasisitiza kuwa Serikali inawajibu wa kutoa   fursa   za kielimu kwa watu wote katika madaraja yote. Katika hili, hakuna aliebaguliwa   kwa   sababu yeyote ile, lengo likiwa ni kumjumuisha kila mtu wakiwemo wenye ulemavu. Kwani baadhi ya watu, walidhani kwa watu wenye ulemavu   kusoma   ni anasa na sio muhimu. Ndipo mikataba ya kimataifa na kikanda, sheria, pamoja sera mbali mbali zikazungumzia haki ya elimu kwa watu hawa. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa mwaka 2006, katika ibara ya 24 imezitaka nchi wanachama kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata elimu. "...

CFP, CFI, TAMWA-ZANZIBAR: ‘MRADI WA ZANADAPT WAMALIZA KIU WANAWAKE, WAANDISHI WA HABARI’

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ SERIKALI kwa kushirikirikiana na wadau wa ndani na nje, wanayo mikakati ya kweli ya kuhakikisha, kilimo mseto kinawanufaisha wanawake Pemba. Kwa sasa mradi wa kuwawezesha wanawake kukabiliana na mabadiliko tabia nchi, na kukidhi maisha yao, unaendeshwa na taasisi kadhaa na TAMWA ukiwemo upo shehia nne kwa Pemba. Kati hizo ni za Mchanga mdogo, Kambini zote zikiwa mkoa wa kaskazini Pemba, ndani ya wilaya ya Wete. Hili lilikuja baada ya tafiti kadhaa, kuonesha maeneo hayo ndio makuu yalioathiriwa na mabadiliko tabia nchi, yawe yale ya asili au yaliosababishwa na harakati za mwanadamu. Kilimo mseto kilitajwa na wataalamu kuwa, ndio mwarubaini wa kukabiliana na mabadiliko tabia nchi, kwa kule kuhifadhi mazingira na kujipatia kipato. KWANI KILIMO MSETO NI KIPI? Mitandao inaelekeza kuwa, ni m fumo wa kilimo cha mseto hujumuisha mambao kadhaa, yakiwemo, ukuzaji wa mimea na miti ya aina fulani kwa pamoja kwenye shamba. Mfumo huu waweza kuan...

ZANADAPT MKOMBOZI KWA WANAWAKE, SASA WAINUKA KIUCHUMI WAZISAIDIA JAMII ZAO

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MATUMAIANI huonekana sehemu zenye bahari kwa kuwepo aina ya miti ya mikoko, pembezoni wa bahari. Zanzibar, kwa sasa kuna uhutaji wa elimu juu ya uwoto wa asili, kwani hupoteza twasira ya mazingira na uharibifu ya bahari. Matumaini ya wanawake wa kisiwa cha Pemba shehia ya Mchangamdogo ni kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi, kwa kujikita katika kilimo msitu cha upandaji wa miti ya mikoko. Mikoko ni  misitu inayopatikana katika nchi za joto sana na la kiasi, ambayo inaweza kuota na kumea katika maeneo ya maji chumvi, ambayo yapo katika ukanda unaofikiwa na maji kujaa na kutoka na kupwa. Mikoko inaweza kuishi kwa kufunikwa na maji kujaa na kutoka, imejiweka maumbile maalum inayowezesha kustawi katika mazingira yenye changamoto. Zanzibar inayo karibu hekari 18,000 za msitu wa mikoko hekari 6,000 zipo katika kisiwa cha Unguja na hakari 12,000 katika kisiwa cha Pemba....