NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amesema serikali itaendelea kulijali kundi la watu wenye ulemavu, ili kuhakikisha wanapatiwa haki zao msingi, ikiwemo za uongozi na uchumi. Hayo aliyasema leo Septemba 16, 2025 kwenye hutuba yake, iliyosomwa kwa niaba yake na Katib tawala wilaya ya Micheweni Sheha Mpemba Faki, alipokuwa akifungua kongamano la wadau wa maendeleo jumuishi katika jamii, lililofanyika skuli ya Utaani Pemba. Mkuu huyo mkoa alisema, serikali imewapa haki na fursa na kuwathamini pamoja na kuwaunga mkono, watu wenye ulemavu kama walivyo watu wingine. Alieleza kuwa, watu wenye ulemavu wamepewa fursa kubwa ya kushiriki katika kupiga kura na kuchagua viongozi, wawatakao, kama msingi wa sheria mama katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilivyoekeleza kifungu cha 7 na ch 12. "Niwatoe hofu nyinyi watu wenye ulemavu, mnayo fursa kubwa ya kushiriki kikamilifu katika harakati mbali mbali zikiwemo za kisi...