Skip to main content

Posts

Showing posts from 2025

WANAWAKE DAR -ES SALAAM WAOMBA ELIMU ZAIDI KUHUSU HAKI

NA MWANDISHI MAALUM@@@@ WANAWAKE Jijini Dar es salaam wameomba elimu ya haki za binadamu na misingi  ya utawala bora izidi kutolewa kwenye mikusanyiko ya wanawake kwani wao mara nyingi wamekuwa wakikosa fursa ya kupata elimu hiyo hasa katika mikutano inayoandaliwa na viongozi wa Serikali kutokana na majukumu waliyo nayo. Rai hiyo imetolewa na wanawake waliotembelea banda la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kwenye maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.   ''Tumejifunza mengi leo kuhusu haki zetu kama wanawake, tunaomba elimu hii itufikie hadi kwenye vikundi vyetu vya kina mama, kwani mara nyingi tunashindwa kuifikia mikutano inayoandaliwa vijijini ama mitaani kutokana na shughuli nyingi za jamii majumbani, lakini elimu ya haki ikitukuta kwenye vyama vyetu huwa tunalazimika kwenda kwasababu huwa haviwahusu wanaume”. alisema mama mmoja aliyetembelea banda ya THBUB, viwanja vya sabasaba. Kwa upand...

MKAGUZI WA POLISI SHEHIA YA PANDANI, AWAASA VIJANA KUJITENGA NA JINAI

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MSAIDIZI shehia ya Pandani wilaya ya Wete, Inspekta wa Polisi Khalfan Ali Ussi, amesema, ushirikishwaji wa jamii katika dhana ya ulinzi shirikishi, kutasaidia vijana kujitambua na kuishi kwa kuzingatia madili katika jamii.   Aliyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa bonanza la michezo, lilifanyika katika uwanja wa mpira katika kambi ya ‘FFU’ Finya wilaya Wete.   Alisema vijana ndio wahanga wakubwa katika jamii kwenye matokeo mbali mbali ya uhalifu, hivyo wanapaswa kupewa elimu itakayowawezesha kujitambua na kuacha matendo yaliyokinyume na maadili ya jamii.   Alieleza kuwa, kundi hilo nalo ni muhimu mno katika jamii ya leo na kesho, hivyo lazimalitazamwe kwa jicho pan ana kukua wakiwa na maadili mema.   "Mabonanza kama haya yakiendelea kufanyika yatawasaidia wao, kuhamisha akili yao katika matendo ya kihalifu na kushiriki katika michezo, ambayo tija yake ni kubwa,’’alifafanua.   Aidha aliwasisitiza vij...

SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR BADO NI KIZUNGUZUNGU

NA SITI ALI, ZANZIBAR@@@@ “Sheria ni msingi wa haki amani na maendeleo kwa kila nchi “Hayo si maneno yangu bali yalikuwa ni  maneno ya Raisi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alipokuwa akizindua toleo jipya la juzuu za sheria mwezi  Aprili ,2025 jijini Dar es salaam. Anasema, bila ya sheria kuwa wazi uhakika wa ulinzi wa haki za raia unatoweka au unakuwa hauna uhakika na kusababisha uvunyifu wa amani.    Wandishi wa Habari Zanzibar wamekuwa wakidai sheria nzuri na rafiki ya habari bila ya mafanikio yoyote.Kutokana na kutumia sheria ya zamaani na iliyopitwa na wakati  iliyotungwa tokea miaka ya 1988 ambayo kwa sasa ni kikwazo kwa wandishi wa habari. Akizungumzia kuhusu sheria hiyo, mwandishi nguli wa habari visiwani Zanzibar, Salma Lusangi anasema ni muhimu kwa sasa sheria hiyo ibadilishwe ili iendane na wakati na kukidhi matakwa ya wakati husika. “Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukifanya uchechemuzi wa sheria mbili kuu yaani sheria ya Wakala wa...

KUKUU KANGANI WAASWA KUJIEPUSHA NA WIZI WA KARAFUU

    BAKAR KHAMIS, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wameaswa kuacha tabia ya wizi wa zao la karafuu, kwani kufanya hivyo pia wanaweza kuingizwa kwenye vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Hayo yameelezwa na Mkaguzi wa Polisi Inspekta Hamad Ali Faki, kwenye kikao cha kuimarisha maadili ndani ya jamii, wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Kukuu Kangani wilaya ya Mkoani.   Alisema wapo baadhi wanajamii, wamekuwa na tabia ya kukwapua karafuu za wenzao wanapokuwa shambani, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara zaidi, ikiwemo udhalilishaji.   Alieleza kuwa, zipo kesi kadhaa kila unapofika msimu wa uchumaji wa zao karafuu, hujitokeza zikiambatana na wizi wa karafuu.   "Ndugu zangu wanajamii, niwasihi sana kujiepusha na dhulma ya wizi wa karafuu, maana ndio chanzo cha udhalilishaji, ikiwemo watoto kupewa mimba, kulawitiwa na wengine kuhujumiwa kwa kipgo,"alifafanua.   Katika hatua nyingine, aliwakumbusha wazazi na walezi, kutowaac...

‘WEPO’ YAWAFIKIA WANANCHI 473 KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 473, kati yao wanawake 295 na wanaume 178, wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minungwini, wamefikiwa na elimu, ushauri na msaada wa kisheria, ikiwemo utaratibu wa upatikanaji cheti cha kuzaliwa, kwenye kambi ya msaada wa kisheria, iliyowekwa na Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’. Kambi hiyo ya siku moja, iliyofanyika leo Julai 7, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:30 jioni, wengi wa wananchi waliofika, walikuwa na malalamiko ya kukosa vyeti vya kuzaliwa. Ilifhamika kuwa, wingine ni wanaolalamikia kukosa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi pamoja na vile ya taifa. Akizungumza na waandishi wa habari, Msaidizi wa sheria kutoka ‘WEPO’, Siti Faki Ali, alisema kambi hiyo imewasaidia kuwapa mwanga, wa aina ya changamoto iliomo ndani ya jamii. Alisema, kambi hiyo imewaamsha kwamba, kazi ya kuwaelimisha wananchi kupitia wasaidizi wa sheria, inahitaji kuongezwa nguvu, kwani wapo ambao hawajui hata utaratibu wa kupata nyaraka hizo ...

WATIA NIA CCM : 'MSIJIPITISHE PITISHE KWA WAJUMBE TULIENI MAJUMBANI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHAMA cha Mapinduzi CCM mkoa wa kusini Pemba, kimepiga marufuku kwa watia wa nafasi mbali mbali, kuacha kujipotisha pitisha kwa wajumbe, na kuanza kampeni za chini kwa chini, kwani wakati wake haujafika.   Akizungumza na mwandishi wa habari katibu wa CCM mkoani humo, Kajoro Vyohoroka, alisema huu sio wakati kwa watia nia kujipitisha karibu na makaazi ya wajumbe na kuanza kampeni.   Alisema, CCM inaomfumo mzuri wa kidemokrasia wa kuwapata wajumbe watatu, ambao ndio watashushwa chini kwa ajili ya kupigiwa kura, na sio sasa kuanza kufanya jambo lolote.   Alieleza kuwa, ni marufuku kwa sasa kwa watia nia hao, kufanya jambo lolote linaloashiria kampeni ama kuingilia utaratibu wa vikao vya chama, na badala yake wawe watulivu majumbani mwao.   ‘’Ni kweli kuwa, hatua ya kwanza ya kuwapata wagombea wetu kwenye uchaguzi mkuu, umeshakamilika hivyo, watia wastahamili waanze kishindo cha kuwasilimu wajumbe, huu wakati wake bado,’...

'WEPO' KUENDESHA KAMBI YA MSAADA WA KISHERIA KIGONGONI, KIUYU MINUNGWINI ASUBUHI HII

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’ asubuhi hii, inatarajia kuendesha kambi ya siku moja, ya msaada wa kisheria kwa wananchi wa shehia za Kigongoni na Kiuyu Minunwgini wilayani humo, bila ya malipo. Kambi hiyo, ambayo inatarajiwa kuwakusanya zaidi ya wananchi 500 wa shehia hizo, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa kupambana na ukatili na udhalilishaji, chini ya ufadhili wa shirika la UNDP. Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mratibu wa mradi huo, Rashid Hassan Mshamata, alisema kambi hiyo itawahusisha wataalamu wa masuala ya ardhi, mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka, ofisi ya Mwanasheria mkuu. Alieleza kuwa, wataalam wingine watakaokuwepo kwenye kambi hiyo ni Jeshi la Polisi, dawati pamoja na wasaidizi wa sheria, kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’. Aliwataka wananchi wa shehia hizo na nyingine, kufika kwenye kambi hiyo ya siku moja, ili kuwasilisha matatizo yao ya kisheria...

'TUZ': TUNAWASHIRIKISHA WADAU ILI KUFIKIA MALENGO'

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MKURUGENZI Rasilimali watu utawala na mipango wa Tume ya Utangazaji Zanzibar ‘TUZ’ Zainab Sheha Khamis amesema, kushirikishwa kwa wadau mbali mbali katika kuchangia kanuni ya maudhui na udhibiti wa vituo vya utangazaji, kutasaidia kufikia malengo yaliyokusudiwa na  tume hiyo.   Aliyasema katika mkutano wa mafisa wa Jeshi la Polisi wa kitengo cha kupambana na uhalifu wa mtandaoni, kuhusu udhibiti wa maudhui kwa vituo vya utangazaji, kuelekea uchaguzi mkuu 2025 uliyofanyika ukumbi wa mikutano ZBC Mkoroshoni Chake Chake Pemba.   Alieleza kuwa, kwa kushirikiana na wadau hao kutasaidia kufikia malengo husika, ya kupambana na uhalifu wa kimitandao, kuhusu maudhui kwa vituo vya utangazaji, ili kuepusha migogoro inayoweza kutokezea.   "Tumeona wadau hawa ni muhimu, katika kushirikiana nao kwani wao ni sehemu moja wapo ya kuhakikisha wanadhibiti maudhui yaliyokua siyo na kupambana na uhalifu katika mitandao,"alifafanua. ...

'WEPO' 'JAMII IKIAMUA, LEO UDHALILISHAJI KWISHA KAZI WETE'

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ MRATIB wa mradi wa uwezeshaji na upatikanaji wa haki, Rashid Mshamata, kutoka Jumiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete ‘WEPO’ amesema bado jamii, ina muamko mdogo katika vita vya ukatili na udhalilishaji.   Alieleza hayo kwa wanafunzi na walimu wa skuli na madarsa, za Wete ukumbi wa skuli ya Chasasa, ikiwa ni muendelezo wa kampeni ya kupiga udhalilishaji katika jamii.   Alisema jamii bado ina mila na desturi kandamizi ambazo zinawafanya wasichana na wanawake waishi kwa hofu, na kukosa usawa na haki zao stahiki, jambo linalowapa mwenye wa kufanya maovu.   ‘’Kupitia kampeni hii, tunawaleta vijana kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, ambapo tunawafundisha sio tu kujitambua, bali kushiriki katika kulinda haki za wenzao na kuripoti vitendo,"alieleza.   Mshamata alifafanua kuwa, mafanikio ya kampeni hizo skuli na madrassa, inadhihirisha kwamba vijana wakiwa na maarifa sahihi, wanaw...