NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@ KAIMU Mkuu kitengo cha uhusiano Mamlaka ya udhibiti wa huduma ya maji na nishati Zanzibar (ZURA) Shara Chande Omar amesema mamlaka itaendelea kuandaa utaratibu pindi tu inapotokea mabadiliko ya bei elekezi kwa matumizi za huduma ya maji, nishati ili Kuwaondoshea usumbufu wananchi. Ameyasema hayo akitoa ufafanuzi wa bei mpya ya umeme katika kikao na wandishi wa habari mbali mbali huko kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi za ZURA Kibirinzi chake chake Pemba Amesema lengo la kikao hicho na wadau wa habari ni kuwafikishia wananchi tarifa hiyo ya mabadiliko ya bei ya umeme ambayo imeanza kutumika kwa sasa. " Wandishi wa habari ndio Wenye jukumu la kuwafikishia wananchi tarifa sahihi pindi tu itapotokea mabadiliko ili kuepuka malalamiko na kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya umeme. "alisema kaimu huyo. Aidha amesema kuwa mamlaka imeanda utaratibu wa kuwasajili mafundi wa umeme kwa kuwapatia vib...