NA HAJI NASSOR NIPO, jiji la Beijing linalopatikana takriban saa 12, kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar, kwa usafiri wa anga. Jiji hili ni moja kati ya majiji manne yayounda taifa la China, likiwemo pia lile la Shanghai, ingawa Beijing ndio mji mkuu. Lenyewe limezungurukwa na milima mikubwa kwa upande wa magaribi, ingawa kusini mashariki na kaskazini mwa jiji hilo, linaujirani na bahari iitwayo Bohai. Jiji hili, lina ukubwa wa skweya kilomita 16,410, ambapo hadi mwishoni mwa mwaka 2023, lilikuwa na wakaazi milioni 21.858. Kati yao hao, wanaoishi ndani ya mji husika wa kudumu ni watu milioni 19.198, sawa na asilimia 87.8, huku ambao sio wa waakzi wa kudumu ni milioni 8.204 sawa na asilimia 12.2. Mpaka mwezi April 2023, Beijing pekee inazo wilaya 16 ‘ municipal districs’ ikiwemo ya Xichenga, Chaoyang, Fengatai, Shijingshan, Hiaidian, Miyun pamoja na wilaya ya Yanging. Ukingia ndani ya jiji la Beijing, mara zote utakaribishwa na mazingira maz...