NA MWANDISHI MAALUM@@@@ WANAWAKE Jijini Dar es salaam wameomba elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora izidi kutolewa kwenye mikusanyiko ya wanawake kwani wao mara nyingi wamekuwa wakikosa fursa ya kupata elimu hiyo hasa katika mikutano inayoandaliwa na viongozi wa Serikali kutokana na majukumu waliyo nayo. Rai hiyo imetolewa na wanawake waliotembelea banda la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kwenye maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam. ''Tumejifunza mengi leo kuhusu haki zetu kama wanawake, tunaomba elimu hii itufikie hadi kwenye vikundi vyetu vya kina mama, kwani mara nyingi tunashindwa kuifikia mikutano inayoandaliwa vijijini ama mitaani kutokana na shughuli nyingi za jamii majumbani, lakini elimu ya haki ikitukuta kwenye vyama vyetu huwa tunalazimika kwenda kwasababu huwa haviwahusu wanaume”. alisema mama mmoja aliyetembelea banda ya THBUB, viwanja vya sabasaba. Kwa upand...