Skip to main content

''PUNGUZENI MATUMIZI YA KARATASI KWA SHUGHULI ZA KIOFISI' MHANDISI ZENA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WATENDAJI wa taasisi kisiwani Pemba wametakiwa kuacha tabia ya kutumia makaratasi kwenye shughuli zao za kiofisi na badala yake waendelee kutumia mfumo wa kidigitali, ili kuwarahisishia katika utendaji wa kazi zao za kila siku.

Akifungua mafunzo ya mfumo wa vibali vya safari za nje ya nchi (ZanVibali), leo Machi 4, 2024 Chake chake Pemba, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandis Zena Ahmed Said alisema, mfumo wa kidigitali ni rahisi na mtumishi atapata kibali kwa haraka.

Alisema kuwa mfumo huo ni muhimu sana kwani kutakuwa na uwazi na uwajibikaji, Serikali itaona fedha zote za gharama zitakazotumika kwenye safari pamoja na kurahisisha upatikanaji wa vibali kwa watumishi hao ambapo wakitumia makaratasi huchukua mda mrefu.

"Tumeweka mfumo huu kwa ajili ya kuleta tija kwetu kwa sababu mfumo wa makaratasi una changamoto nyingi, hivyo huu utaturahisishia kila kitu na utapata kibali kwa urahisi zaidi pasi na kikwazo chochote," alisema.

Mhandis huyo alizielekeza taasisi zote kutumia mfumo wa kidigitali wa ZanVibali na ZanMalipo ili kuipatia Serikali mapato ambayo ndio yanayotumika katika kuwalipa wafanyakazi na kujenga miundombinu mbali mbali kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

"Tutumie hii mifumo, tutoe na tudai risiti ili tupate mapato mengi yatakayotusaidia kupata maendeleo katika nchi yetu," alieleza Katibu huyo.

Aidha Mhandis Zena aliwataka viongozi wa taasisi kuzisoma Sheria, kanuni na kuzisimamia, ili kuwajibika ipasavyo sambamba na kuchukua hatua za kinidhamu kwa mtendaji ambae atakwenda kinyume na maadili ya Utumishi wa umma.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar Said Seif Said aliwataka viongozi hao wa taasisi kukubali mabadiliko ya kidigitali ili yapatikane kwa urahisi.

"Mambo mengi sasa yatabadilika kutoka analogi kuja kwenye digitali, hivyo tujitahidi sana makusanyo ya mapato ya Serikali yapitie kwenye mfumo wa digitali na tushirikiane kuhakikisha tunatimiza lengo la Serikali kwa haraka na kwa ufanisi," alifahamisha Mkurugenzi huyo.

Nae Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali alieleza kuwa, kila mmoja kwa nafasi yake ana wajibu wa kusimamia na kutekeleza yale ambayo yanaleta mageuzi katika Serikali.

"Tuna mifumo tofauti, mengine imeshaanza kutumika na mengine wataendelea, zile changamoto zilizopo tuzione ni fursa, hivyo tusiwe ni miongoni mwa wanaokwamisha bali tusimamie ili kufanikiwa," alieleza.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo Awena Rajab Mohamed kutoka eGAZ alitaja miongoni mwa faida kuwa ni kuongezeka kwa uwazi wa taarifa za vibali na kufanya maamuzi sahihi kwa wakati unatakiwa.

Mafunzo hayo ya siku tatu yamewashirikisha watendaji wa kada mbali mbali kwa siku tofauti, yameandaliwa na Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar ambayo yamefanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani Chake Chake.

                MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...