Skip to main content

WAANDISHI KUWENI WAKALI HADI SHERIA MPYA YA HABARI IPATIKANE ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, UNGUJA

WAAANDISHI wa habari wameshauriwa kutoa maoni yao katika kupata sheria mpya ya habari,. ambayo itapelekea kufanya kazi zao kwa ufanisi bila kukandamiza uhuru wao.

Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Shifaa Said Hassan, alieleza hayo Febuari 8, 2023 wakati akifungua mkutano wa majadiliano kuhusu sheria zinazokandamiza uhuru wa habari Zanzibar kwa vyombo vya habari uliofanyika katika ukumbi wa Mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar ZSSF Kariakoo mjini Unguja.

Alisema kupatikana kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini ni fursa ya kuwa na sheria na muundo huo utakaoendana na wakati uliopo.

Alibainisha kuwa tasnia ya bahari ni muhimu katika nchi kwani inachochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla kiuchumi, kisiasa na kijamii.



Aidha alisema wanabari ndio wanaojua changamoto wanazokabiliana nazo katika utelelezaji wa majukumu yao ikiwemo kukosa taarifa katika wizara na tasisi za serikali hali ambayo inakandamiza uhuru wao hasa wa kikatiba hivyo vyema kutoa maoni yao ambayo yatasaidia kupata sheria nzuri.

Mjumbe Shifaa alibainisha kuwa Zanzibar kuna sheria kuu mbili za habari ikiwemo ile ya magazeti na vitabu ya mwaka 1988, sheria ya vyombo vya utangazaji ya mwaka 97 na sheria nyengine kadhaa ambazo zinakandamiza na kukinzana na uhuru wa habari.

Hivyo alisema ni imani yake kwamba baada ya mafunzo hayo watapata matokeo mazuri ya kuwa na sheria mpya ya habari ambayo itawafanya wanabari kufanya kazi zao kwa ufanisi na umahiri mkubwa.

“Zipo sheria ambazo zinakinzana katika masuala ya habari mtoe maoni yenu na michango ambayo itasaidia na pale itakapopelekwa Baraza la Wawakilishi basi iwe nzuri na kuwapa uhuru wanahabari katika utoaji wa taarifa,” alisema.

Mbali na hayo aliwataka wanahabari kupaza sauti zao kupitia vyombo vyao vya habari katika kuhakikisha wanapata sheria nzuri ambayo itaendana na wakati wa sasa.

Aliiwapongeza Intervews na Shirika la USAID kushirikiana pamoja kutoa mafunzo hayo ambayo ambayo anaamini sheria mpya ya habari itakayokuwa nzuri na itatoa uhuru kwa vyombo vya habari vilivyokuwepo nchini. 

Mkuu wa Chuo cha Uandishi wa Habari wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Iman Duwe alisema katiba ya Zanzibar kifungu cha 18 (1) kimetoa haki ya wananchi kupata taarifa na habari katika nchi yao.



Alisema vipo vifungu vingi katika sheria ya habari vinatakiwa kubadilishwa kwani baadhi yake vinanyima uhuru wa habari kwani sheria nzuri ni ile inayoainisha kila kitu.

Alibainisha kuwa vipo baadhi ya vifungu katika sheria ya usajili wa wakala wa habari, magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988 licha ya kufanyiwa marekebisho kadhaa.

Mkuu Duwe alivitaja vifungu hivyo kuwa ni cha 27 (1) cha sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu nambari 5 ya mwaka 1988  kinachotoa mamlaka kwa ofisa yoyote wa Polisi kufanya ukaguzi na kumamata gazeti lolote limechapishwa iwapo atashuku kuwa limechapishwa kinyume na sheria.

Alisema kupitia kifungu hicho Polisi amepewa mamlaka ya kushikilia mali za gazeti jambo linalonyanganya haki ya kutoa habari iliyoainishwa na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Kwa upande wa Sheria ya Tume ya  Utangazaji ya Zanzibar namba 7 ya mwaka 1997, alisema  kifungu cha 7 (2) hakijakaa sawa kwani kinampa uwezo tume kufanya kazi nyengine yoyote atakayopangiwa hivyo ni vyema sheria hiyo ikaeleza au kutaja kazi hizo ili kuepusha kutumika vibaya kifungu hicho.      

Juma Khamis Juma ni Mwandishi wa Habari ambae pia ni Mwanasheria wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar, sheria ya kufuta sheria ya Baraza la Wawakishi (Kinga, Uwezo na Fursa) namba 4 ya 2007 na kutunga sheria mpya ya Baraza la Wawakilishi (Kinga, Uwezo na Fursa) kutekeleza kazi na mambo mengine yanayohusiana na hayo namba 6 ya mwaka 2022 ina vifungu vinavyominya uhuru wa habari.

Alisema katika kifungu cha 27 cha sheria hiyo kinaeleza kwamba utaratibu wowote Baraza au Kamati ambapo mtu yoyote atatakiwa kutoa ushahidi au kuwasilisha nyaraka, utahesabiwa kama amekiuka utaratibu wa kimahakama.

Mwanasheria Juma alisema hali hiyo inaathiri uandishi wa habari za uchunguzi na ni kinyume na kanuni ya uwazi na uwajibikaji.

Hata hivyo akizungumzia sheria ya kufuta sheria ya uchaguzi namba 11 ya mwaka 1984 na kutunga sheria ya uchgazi ya mwaka 2017 na masuala mengine yanayohusiana na hayo kuna vifungu vinavyokataza mtu kutangaza matokeo ya uchaguzi ambayo hayathibitishwa na tume licha kuwa yametolewa na maofisa wa tume katika ngazi za vituo au jimbo.



Alibainisha kuwa vifungu hivyo vinatoa adhabu kubwa ambazo kimsingi vinawapa hofu waandishi wa habari kufanya kazi vizuri.

“Vifungu hivi vinakiuka utu wa mtu na umuhimu wa waandishi wa habari hivyo ni vyema nyinyi wadau kuendelea kupaza sauti zenu ili tasisi zinazohusika na  sheria kuzipatia upya ili ziendane na wakati,” alisisitiza.

Mbali na hayo alisisitiza umuhimu kwa wanahabari kuwa na sheria na kanuni mbalimbali kwa ajili ya kuzisoma ili ziweze kusaidia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.   

Aliwataka wanahabari kuacha mihemko ya kubeba wagombea na kufanya kazi kwa mujibu wa taaluma yao inavyowaelekeza.

Nao waandishi wa bahari wakichangia katika mkutano huo walisema sheria nyingi zilizokuwepo Zanzibar zimeshapitwa na wakati na zinahitaji kuwangaliwa.

Hivyo walisema ipo haja ya kuangaliwa kwa makini vifungu vinavyokwaza uhuru wa habari katika baadhi ya sheria ili kuongeza ufanisi wa kazi zao za kila siku.



Mkutano huo wa siku mbili, mada mbalimbali ziliwasilishwa  ikiwemo ya sheria ya usajili wa wakala wa habari magazeti na vitabu namba 8 ya mwaka 1997, sheria ya  Tume ya Utangazaji Zanzibar namba 7 ya mwaka 1997 kama ilivyorekebishwa na sheria namba 1 ya mwaka 2010 na sheria ya makosa ya mtandao 2015.




Mkutano huo umeandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake(TAMWA)  Zanzibar na kuwashirisha waandishi wa habari wa Unguja na Pemba chini ya ufadhiliwa mradi wa boresha habari INTERNEWS  na Shirika la Marekani USAID.

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch