Skip to main content

SHAHIDI DAKTARI: ''NILIGUNDUA MAREHEMU ALISHAMBULIWA KWA MARUNGU''

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SHAHIDI nambari 14 kwenye kesi ya mauwaji, ambae ni Daktari wa hospitali ya Vitongoji Chake chake Pemba Ali Juma Ali, amedai mahakamani kuwa, baada ya uchunguzi alibaini kuwa, mjeruhiwa alishambuliwa kwa vitu vyenye cha kali na silaha mfano wa marungu.

Alidai kuwa, wakati akiwa kazini kwake hospitalini hapo, Septemba 21, mwaka 2021, alimpokea mjeruhumiwa Suleiman Said Saleh (55) akiwa katika hali mbaya.

Shahidi huyo akiongozwa na Wakili wa serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Ali Amour Makame, mbele ya Jaji wa mahakama kuu Zanzibar Ibrahim Mzee Ibrahimu, alidai kuwa uchunguuzi ukabini kuwa kina cha jeraha la kichwani ni nchi nne kwa upana na urefu nchi mbili.

Alidai kuwa, jeraha jingine ambalo lilikuwa bega la mkono wa kushoto, lilikuwa na nchi tatu kwa urefu na kina cha kwenda chini likuwa nchi mbili.



Akiendelea kuongozwa na Wakili wake, shahidi huyo alidai kuwa, wakati anamfanyia uchunguuzi, alibaini pia mkoja wake wakati ukitoka ulikuwa umechanganyika na damu na huku mjeruhiwa kabla ya kufariki alikuwa akililia maumivu.

‘’Kwa kushirikiana na wataalamu wenzangu, pamoja na majeraha ambayo marehemu yalikuwa yakionekana wazi wazi, pia uchunguuzi tukabaini alikuwa na mititigiko ambayo yanaashirikia alishambuliwa na vitu bapa,’’alidai.

Aidha shahidi huyo nambari 14, alidai vitu kitaalamu vinaweza kuwa mithili ya marungu ya miti, ambayo yalionesha dhahiri alipigwa na watu.

‘’Hata wakati tunamuhoji mjeruhiwa huyo, pamoja na ndugu na jamaa zake waliomleta, walidai kuwa alishambuliwa na watu kadhaa na kusababisha kuvuja damu na kulia maumivu,’’alidai.

Katika hatua nyingine shahidi huyo ambae ni daktari, aliimbia mahakama hiyo kuu kuwa, baada ya siku mbili na kumuona mgojwa wao hali imezidi kuwa mbaya, walimpatia rufaa kwenda hospitali nyingine kwa matibabu.

‘’Ni kweli tulimpokea mjeruhiwa akiwa katika hali mbaya mno, na siku mbili baadae kutokana na ukosfu wa baadhi vya vifaa, tulilazimika kumpa rufaa,’’alidai.

Mara baada ya shahidi huyo kumaliza kutoa ushahidi wake na kuiwasilisha fomu maalum ya matibabu kutoka kituo cha Polisi ‘PF3’mahakamani, Jaji Ibrahim Mzee Ibrahimu, aliupa nafasi upande wa utetezi, ili kuulizwa maswali.

Wakili msomi wa watuhumiwa hao wanne, akiwemo mwanamke mmoja, Zahran Mohamed Yussf, alitaka kujua ikiwa mgonjwa aliyempokea alikua na jalada ‘file’ lake na kujua alikuwa nambari ngapi.

Aidha wakili huyo alitaka kujua ikiwa Daktari huyo hakumfanyia uchunguuzi yeye peke yake, ingawa alidai kuwa alifanya na wenzake kwa amri yake.

Wakili huyo pia alitaka kujua, ikiwa bado hadi sasa Daktari huyo anawakumbuka ndugu na jamaa waliomlete mjeruhiwa huyo, siku alipokuwa kazini na kudai hawakumbuki tena.

‘’Nini nani aliyekwambia kuwa, majeraha aliyokuwa nayo mgonjwa uliyempokea, yalitokana na ugomvi wa ndugu na jamaa zake, kama ambavyo uliieleza mahakama,’’alihoji Wakili huyo.

Mara baada ya kumalizika kwa ushahidi huo na maswali ya kinzani kwa pande zote, Mwanasheria wa serikali Ali Amour Makame, aliimbia mahakama kuu kuwa, wamebakisha na mashahidi wawili.

‘Mheshimiwa Jaji, kwa sasa bado mashahidi wawili akiwemo Askari mpelelezi, na hivyo tukimaliziana na hao wawili, itakuwa tumekamilisha mashahidi wetu 16, na tunaweza kufunga ushahidi,’’alidai.

Hivyo aliiomba mahakama hiyo, kuliahirisha shauri hilo na kulipangia tarehe nyingine, kwa ajili ya kujakuendelea kuwasikiliza mashahidi waliobakia.

Jaji Ibrahim, aliuuliza upande wa utetezi, ikiwa umekubaliana na ombi la upande wa mashataka, na kupitia wakili wa watuhumiwa hao Zahran Mohamed Yussuf, ulikubali.

Hivyo Jaji huyo nae, alikubaliana na mawazo ya pande zote mbili, na kulipangia shauri hilo, kurudi tena Febuari 20, mwakani, huku watuhumiwa wakiendelea na dhamana zao.

Watuhumiwa wanaodai kuumua Suleiman Said Saleh (55) wa Vitongoji ni Said Nassor Khalfan (60), Khadija Said Saleh (52), Nassor Said Nassor (29) na Mohamed Said Nassor (23) wote wakaazi wa Vitongoji.

Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch