Skip to main content

WAZEE WATAKA UZEE UTAMBULIWE KWA MIAKA 60 NA SI0 70

 


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Abeida  Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo imepokea maoni yaliyotolewa na Wazee kuhusu kuifanyia marekebisho sheria ya Masuala ya Wazee, sheria namba mbili (2) ya mwaka 2020 katika kifungu kinachozungumzia umri wa mzee.

Akizungumza baada ya kikao cha pamoja baina ya watendaji wa wizara hiyo ,Kamati ya Kanuni na Sheria ndogo ndogo ya Baraza la Wawakilishi, wazee kutoka Jumuiya ya wazee (JUWAZA) pamoja na wazee wanaoishi katika makao ya wazee, kilichofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa Makao ya Wazee Sebleni, Unguja.

Alisema wazee wametaka kifungu cha sheria hiyo kifanyiwe marekebisho umri wa mzee uwe miaka 60 badala ya miaka 70. Hivyo watendaji wa wizara hiyo watakaa chini na kutafakari.



“Kamati imekuja kututembelea katika makao ya wazee, pamoja kupata maoni ya kanuni, ya masuala ya wazee iliyotungwa hivi karibuni lakini majadala mkubwa umejitokeza, baada ya kanuni hiyo kuonesha umri wa mzee ni miaka 70, na umri huo umewekwa kwa mujibu wa sheria ya masuala ya Wazee, hivyo wazee wametaka turudi kwenye sheria tuifanyie marekebisho ” Alisema katibu Mkuu huyo.

Aidha alisema kwamba Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussuin Ali Mwinyi amewaagiza watendaji wake kwamba endapo sheria ikionekana inaleta changamoto basi ifanyiwe marekebisho ili iendane na wakati uliyopo.

Alisema zaidi wajumbe wa kamati hiyo katika kikao cha majumuisho watatoa maelekezo kuhusiana na hilo, pamoja na wadau wengine ambao wanafanya kazi katika jumuiya za wazee katika kusimami masuala ya wazee.



Alieleza muda sio mrefu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto itatoa elimu dhidi ya kanuni ya Masuala ya Wazee (Utowaji Huduma za Makaazi ) kupitia makundi mbali mbali ndani ya jamii ili kila mtu aifahamu kanuni hiyo. kwani kanuni hiyo imetoa fursa mtu yeyote anaweza kuanzisha Makao ya Wazee.

Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Mwera Mhe. Mihayo Juma N’Hunga amesema wako katika utaratibu wa kuchua maoni kwa wadau na kuangalia kama Kanuni hiyo inafanya kazi na kama kuna mapungufu basi ifanyiwe marekebisho



Alisema kanuni hiyo imetungwa mwezi April mwaka huu, hivyo kamati inafuatilia utekelezaji wake na ndio maana walianza na ziara ya kuwatembelewa wazee katika makao ya Wazee, Limbani Pemba, na kwa upande wa Unguja Welezo na Sebleni na kuwauliza masuala mbali mbali kuhusiana na kanuni.

 Kwa upande wa Wazee akizungumza Bi Salama Kombo Ahmed kwa niaba ya wazee wa Jumuiya wa Wazee Zanzibar (JUWAZA) alisema Serikali ya Zanzibar inamuachisha mtu kazi anapofikia umri wa miaka 60 na sio 70, hivyo sheria ifanyiwe marekebisho.


Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch