Skip to main content

WANAWAKE KISIWA CHA FUNDO PEMBA WATAKA KITUO CHA POLISI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANAWAKE wa kisiwa kidogo cha Fundo wilaya ya Wete Pemba, wamesema umbali wa kilomita zaidi ya 60 kwa usafiri wa baharini kutoka kisiwani hapo, hadi kilipo kituo cha Polisi Wete, ni moja ya changamoto zainazowafanya wasiyaripoti mara kwa mara, matukio ya kihafalifu wanayofanyiwa.

Wamesema wamekuwa wakifanyiwa vitendo viovu kama vile kuharibiwa mitego yao, kilimo chao cha mwani na kisha kutukanwa, ingawa wamekuwa na uzito kukifuata kituo cha Polisi Wete.

Walisema, suluhushi la wao kuyaripoti matendo wanayofanyiwa na vijana wa kisiwa hicho, ni kujengewa kituo kidogo cha Polisi ili karibu yao.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kisiwani hapo, walisema hawaishi kwa amani na utulivu kama walivyo wanawake wengine vijiji vyengine, kutokana na kutishiwa hata usalama wao.

Mmoja kati ya wanawake hao Mwajuma Rashid Salmin, alisema wanapoharibiwa mashamba yao ya mwani na vijana kisha hurejea kuwatukana.

Alieleza kuwa, pamoja na hivyo, wamekuwa wakiwatishia matusi jambo linalowakosesha furaha katika maisha yao, jambo ambalo linawarejesha nyuma.

“Suluhisho la hili tunalofanyiwa na vijana wetu, sasa ni kuwepo kwa kituo cha Polisi, ili iwe rahisi sisi kufikisha malalamiko yetu, maana kituo cha Polisi cha wilaya yetu kiko mbali,’’alilalamika.

Nae Hidaya Omar Hassan, alisema wapo baadhi ya vijana wamekuwa wakiingia ndani kwa nia ya ubakaji na wizi, ingawa unapowakamata hukutishia kwa maneneo maovu.



“Wanatuahidi hata sisi wazazi kutubaka, na kutuharibia vipando vyetu pindi tukiwakataza, sasa wakati umefika wa serikali kuangalia uwezekano wa kutujengea kituo cha Polisi,’’alieleza.

Kwa upande wake Hadia Hassan Mkombe alisema, wanaoendesha vitendo hivyo ni watoto wao wa kuwazaa, wanaochukua mazoezi miji ya Nungwi na Wete mjini.

“Kwanza huanza kuvuta sigara kisha bangi na kisha hujiingiza kwenye vitendo vya wizi na baade kutoa matusi ya hadharani bila ya woga,’’alieleza.

Kwa upande Omar Haji Ussi, alisema kilichokosekana kwenye shehia yao ya Fundo ni kutokuwepo kwa kikundi cha ulinzi shirikishi na vijana kufanya watakavyo.

Nae Othman Hamad Pandu mwenye ulemavu wa viungo, alisema ujenzi wa kituo cha Polisi kinaweza kuwa suluhisho, iwapo watendaji wa jeshi la Polisi, watazitumia vyema sheria.

Sheha wa shehia ya Fundo Khamis Abeid, alisema kutokana na kisiwa hicho kuongezeka wa idadi ya watu, navyo vitendo vya uvunjifu wa maadili vimeongezeka.

“Ni kweli sasa wakati umefika kwa kisiwa kidogo cha Fundo kujengewa kituo cha Polisi, na huwenda ikawa suluhisho la kupunguza kasi ya vitendo viouvu,’’alieleza.

Vijana Hassan Kombo Mwadini na Hashim Ngome Is-haka walisema bado kwa kisiwa chao, hakihitaji ujenzi wa kituo cha Polisi kwa vile hakuna uhalifu wa kutisha.

“Wazazi wakae pamoja kuwashughulikia wale wachache wanaojihusisha na uvutaji bangi na wizi, hata kutumia malezi ya pamoja ili kisiwa kiwe salama,’’alieleza.

Mwinjaa Shavui Masiku ambae anaulemavu wa viungo, amesema uhalifu uliopo unaweza kudhibitiwa ikiwa kutaimarishwa kwa ulinzi shirikishi.

“Kunaweza kujengwa kituo cha Polisi lakini kisipewe ushirikiano na uhalifu pengine ukazidi, jambo linalotakiwa ni wazazi kukutana na kukubali kuwa vijana wao ndio wakosaji,’’alieleza.

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Hamad alisema kuwa, wakati umefika kujengewa kituo hicho, ili kuepukana na usumbufu wa kukifuata kisiwa cha Fundo.

Alisema tayari Kamishna wa Polisi Zanzibar ameshapata taarifa hiyo na kinachosubiriwa ni ruhusa ya kuanza kwa ujenzi huo, hasa kwa vile wananchi wenyewe wako tayari.

‘’Ni kweli wananchi hao wanaomba kujengewa kituo cha Polisi, na sisi kama wilaya kazi iliyobakia ni kukumbisha makao makuu ya Polisi, maana hili ni jambo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,’’alifafanua.

Hivi karibuni Kamishan wa Jeshi la Polisi Zanzibar Awadh Juma Haji, alinukuliwa na vyombo vya habari, akisema amekiri kupokea ombi hilo na fedha zikipatikana kitajengwa.    


     

Kisiwa cha Fundo kilichoasisiwa na wavuvi wadago miaka 80 iliyopita, kikiwa na wakaazi 50, sasa kinawakaazi zaidi ya 5000, kipo wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, kimepakana na visiwa vya Uvinje na kijiji cha Raha.

                               Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch