Skip to main content

DK. MWINYI AKIWA PEMBA AWAPA FUTARI WANANCHI

 

        

NA HANIFA SALIM, PEMBA 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kila mwenye uwezo anawajibu wa kutoa sadaka kwa kuwasaidia ambao hawana uwezo hususani katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Alisema katika mwezi huu mtukufu wafadhili wengi wamejitoa katika kuwasaidia watu ambao wana hali duni za kimaisha, hivyo aliwataka wananchi wenye uwezo kujitolea kutoa sadaka kwa wenzao ambao wako katika mazingira magumu.

Aliyasema hayo kwa nyakati tofauti, katika hafla ya kukabidhi msaada wa futari kwa wazee, mayatima, wajane na watu wenye ulemavu kwa Mkoa wa Kusini Pemba, iliyofanyika ofisi ya Mkuu wa wilaya Mkoani na Tibirinzi Chake chake.

"Ni kweli wanaopata ni wachache na wanaohitaji ni wengi, lakini hii ni taasisi moja tu zipo na taasisi nyengine ambazo zimesaidia, ikiwemo kampuni ya Olympic na mashirika mengi yamesaidia kwa Wilaya ya Micheweni na Wete", alisema.

Dk. Mwinyi alisema, kwa niaba ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amewashukuru watoaji wa sadaka hiyo kutoka nchini Quwait na nchi nyengine ambazo zilijitokeza kuisaidia Zanzibar.

Aidha, aliwataka ambao wamepatiwa sadaka hiyo kuwaombea dua wafadhili hao ambao wamejitolea kuwasaidia ili Mwenyezi Mungu awaongezee kipato kitakachopelekea kuwasaidia tena kwa mara nyengine zaidi.

Mapema Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud amesifu utaratibu unaofanywa na wenzao wa nchi mbali mbali wa kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia sadaka kila ifikapo mwezi mtukufu wa Ramadhani.



Alisema, utaratibu huo unaofanyika umekua ukiwafikia makundi yote yenye hali ngumu ya kimaisha ikiwemo yatima, wazee wasiojiweza, wajane na watu wenye mahitaji maalumu.

Alisema kuwa, misaada kama hiyo imekua ikijenga mahusiano mema baina ya Serikali taasisi za watu binafsi na wananchi na serikali yao.

Baadhi ya wanufaika wa msaada huo kutoka Vitongoji Chake chake Shuwekha Abdalla Saleh alisema, amemshukuru Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi kwa kuwapatia msaada huo ambao ni msaada wa mwanzo kwa upande wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Nae Mohamed Omar Mohamed mwenye ulemavu wa viungo mkaazi wa Machomane Chake chake alisema, utaratibu huo ni vyema ukawa endelevu, kwa kila mwaka kwani umekua ukiwasaidia katika maisha yao ya kila siku kutokana na hali zao duni za kimaisha.

 


Zaidi ya wananchi 800 wa makundi ya watu wenye ulemavu, wazee, wajane na mayatima wamepatiwa msaada wa vyakula mbali mbali ikiwemo unga, sukari, tende na mafuta uliotolewa na Dk. Sughad Al-Swabah na Mubarrak Al-Swabah kutoka nchini Quwait kupitia kwa Suheil Muzammil.

                               MWISHO.

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch