Skip to main content

WATAALAMU WA AFYA PEMBA WAPIGIA CHAPUO MAZIWA YA MAMA KWA WATOTO


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::::

WATAALAMU wa afya ya mama na mtoto kisiwani Pemba, wamewakumbusha wanawake, kuhakikisha hawawalishi chakula au aina yoyote ya kimiminika, watoto wao wachanga, kama bado hawajatimiza miezi miezi sita, kwani kufanya hivyo, huwapa ukuaji bora na wenye afya.

Walisema ukuaji bora na wenye afya kwa mtoto, na hasa baada ya kuzaliwa, huchangiwa na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na wazazi kuacha kuwalisha watoto wao chakula au aina ya yoyote ya maji.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wataalamu hao walisema, kumlisha chakula hata laini au aina yoyote ya maji mtoto ambae hajatimiza miezi sita, ni kuilazimisha mishipa na mashine ya kusagia kufanya kazi isiyoimudu.

Mmoja kati ya wataalamu ambae ni muuguzi wa mama na mtoto wa Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, Rabia Mohamed Ussi, alisema hali hiyo, hupelekea kuzuka kwa magonjwa ikiwa ni pamoja na utampia mlo.

‘’Hata kama mtoto analia kwa ishara ya njaa, lakini hakuna namna ya kumpa chakula au aina yoyote ya maji, na likifanyika hilo ni kumpelekea kupata athari, na kubwa zaidi ni kudunisha ukuajia wake,’’amesema.



Kwa upande wake Msimamizi wa kitengo cha lishe Wilaya ya Chake Chake, Harusi Masoud Ali, anasema kufuata utaratibu wa kumnyonyesha kwa akina mama, huwapa ukuaji mzuri mtoto.

Alisema ndani ya miezi sita ya kwanza, mwili wa mtoto hujitayarisha kwa ajiali ya chakula, au maji maji na ikifanyika vyenginevyo, ni kulazimisha na kupelekea athari.

Alisema wapo baadhi ya akinamama, wamekuwa wakijishiriki kwenye kazi za muda mrefu, na kucha utamaduni wa kuwanyonyesha watoto na kisha kuwalisha kabla ya wakati.

‘’Tunasisitiza kuwa, ili mtoto apate makuzi mazuri, afya njema na kujiepusha na utapia mlo ni vyema wazazi wachunge miezi sita ya mwanzo wasiwalishe aina yoyote ya chakula,’’alieleza.

Nae mtaalamu wa malezi ya kisayansi na makuzi ya awali ya mtoto ‘SECD’ Omar Mohamed Ali, alisema upo uwezekano mkubwa wa mtoto kuwa na ufahamu wa kina, ikiwa wazazi watafuata maelekezo ya wataalamu.

‘’Bado jamii wamekuwa wakiona kama utani, wanapoambiwa wasiwalishe watoto wao chakula au maji, maana maziwa ya mama yanavirutubisho na madini ya kutosha kwa ajili ya maisha ya mtoto,’’alifafanua.

Akizungumza hivi karibuni, kwenye mafunzo ya siku sita kwa waandishi wa habari, maafisa ustawi na maendeleo wa baadhi ya mikoa, na kufanyika Dodoma, mkufunzi wa mafunzo ya ‘ECD’ Davis Gisuka wa tasisi ya Children in Crossfire Tanzania, alisema jamii inapaswa kushirikina katika malezi.



‘’Tukizungumzia makuzi na maendeleo ya awali ya watoto, wanaume wamekuwa wakijitenga, jambo ambalo sio sahihi, kwani mama peke yake, hawezi kuwa na mtoto bora,’’alieleza.

Meneja ‘ECD’ tasisi ya Maendeleo ya Binadamu kutoka Chuo Kikuu cha Aga Khan, Mombasa Joyce Marangu, alisema upatikanaji wa chakula bora kwa mama mzazi, humpa ari ya kunyonyesha mtoto wake.

‘’Moja ya faida kubwa ya malezi ya ‘ECD’ kwa wazazi na walezi ni kugundua ufahamu na umahiri wa mtoto, tokea mapema, lakini hata juu ya uwezo wake wa kutambua mambo kadhaa,’’alifafanua.

WAZAZI

Wazazi Asha Hilali Nassor na mwenzake Aisha Othman Dadi wakaazi wa Mizingani Mkoani, wanasema wamekuwa wakiwanyonyesha watoto kabla ya miezi sita ya mwanzo kumalizika, kutokana na wao kukosa mlo kamili hapo awali.

Wanasema, bado jamii inaona suala la makuzi na malezi bora ya mtoto ni jukumu la mama peke yake, wakisahau wanayonafasi ya kuwapatia chakula na lishe bora wakati wote.



Omar Khamis Haji na Mohamed Issa Omar wa Chake chake, wanasema elimu ya kuanzisha bustani ya mboga mboga, bado iko chini na ndio maana waliowengi wanapoelezea lishe kwa mama, hufikiria mayai na samaki mkubwa.

Khadija Hamza Shehe, mwenye watoto wawili, anasema mtoto wake wa kwanza mwenye miaka sita, anaufahama duni, ikilinganishwa na mwenye miaka minne.

‘’Wa kwanza alikuwa analia mno, alipofika miezi mitatu, nilianza kumpa maji, na chakula laini, na huyu wa pili alianza kula akiwa ni miezi saba, lakini wanatofautiana hata kiafya,’’anasema.  

RIPOTI INASEMAJE YA UNICEF

Ripoti mpya ya ulimwengu iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’ iitwayo siku za mwanzo za maisha ya kila mtoto ni muhimu ‘Early Moments Matters for Every child’ inasema kipindi tokea kutunga kwa mimba, ni mihimu.

Ripoti hiyo inasema ni kipindi mwafaka na adimu kwa wazazi, katika kuandaa vyema na kuujenga ubongo wa mtoto wao mchanga, na takuwa na wapesi wa ufahamu wa mambo kadhaa katika maisha yake.

Ripoti inafafanua kuwa, watoto hata wakiwa tumboni wanahitaji huduma bora mfano afya, lishe, kuchangamshwa, fursa za kujifunza na kuyaelewa mazingira yao kwa haraka.

‘’Watoto milioni 55, wameripotiwa kudumaa duniani kote, na wengine milioni 230 wanaishi katika mazingira yaliyoathiriwa na machafuko na wanakabiliwa na msongo wa mawazo, huku watoto wengine milioni 300 wakiishi katika maeneo yalioathiriwa na uchafuzi na uharibifu wa mazingira,’’aimefafanua.

Tanzania imetajwa kwenye ripoti hiyo kuwa, inao maelfu ya watoto wanaokosa vichochezi vya ukuaji vinavyolea ubongo wao, ikiwemo lishe duni sawa na asilimia 34 ya watoto waliochini ya miaka mitano.

                                        Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch