Skip to main content

SHARON ROBERT: KIONGOZI ALIYEVUNJA UKIMNYA KUWASTIRI WANAFUNZI SKULINI ZANZIBAR

 


 NA NIHIFADHI ISSA, UNGUJA@@@@

NI kawaida kwa watoto wa kike wakifikia umri kuanzia miaka 10, kubaleghe na kutokanana na maumbile siku hizo huanzia  tatu (3) hadi saba (7).

Kiutaratribu watoto hutakiwa kwenda skuli kuanzia siku 20 hadi 22 kwa mwezi mmoja  lakini watoto wa kike hususan walioko vijijini, huenda skuli siku 15 hii hutokana na kuingia kwenye kawaida yaao na kukosa taulo za kujisitiri.

Zanzibar yenye watu wapatao milioni 1.8 huku idadi ya vijana ikiwa ni Zaidi ya 600,000  inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa elimu ya afya na hedhi salama kwa wanawake

Sharon Robert akiwa Mkurugenzi wa taasisi ya 'holding  hands foundation' alifanya utafiti mwaka 2019 na kugundua kuwa, watoto wakike wanaoishi nje ya mji wanakosa kwenda skuli siku 84 kwa mwaka, katika ya siku 180 wanazotakiwa.

Akiwa mwanamke na kiongozi kwenye taasisi yake Hii ilimfanya Sharon kuanzisha kampeni ya kukusanya taulo za kike na kuwapa wasichana bure maskulini.

Sharon alianza ugawaji wa taulo za kike  mwaka 2020 ambazo anazipata taulo hizo kupitia watatii wanaokuja visiwani Zanzibar pamoja na wadau wengine.

Licha ya kuwa mama, mke yeye pia ni Meneja  wa hoteli ya Shangani kupitia nafasi hiyo humkutanisha na wageni kupata taulo za kike ambazo huzisambaza katika skuli za msingi na sekondari mjini na vijijini lengo kumsaidia mtoto wa kike kupata haki yake ya elimu bila ya ikwazo chochote.

Sharon anasema kuwa mwanamke ni   kiongozi, mzazi na mlezi  na ni  vyema kuwasaidia wanawake wengine na  anaamini ikiwa wasichana watapata taulo za kike watahudhuria masomo yao kwa siku 230 ndani ya mwaka.

''Nafanya hivi nikiwa chini ya taasisi lakini pia nikiwa mwanamke kwasababu utafiti tulioufanya wasichana wengi hawana uwezo wa kupata taulo, kwa kila mwezi kwa hiyo natumia nafasi yangu wakija watalii nawaeleza hali iliyopo na wao hutoa mchango wao,”alisema Sharon.

Hadi kufikia Disemba 2023 mwanamke huyu ameshawafikia wasichana 8,000 kwa Unguja huku mlengo ni kuwafikia wasichana 23,000 hadi kufikia mwaka 2025 kwa miaka minne.



''Iili msichana afikie ndoto zake za kuwa kiongozi bora ni lazima aandaliwe mazingira mazuri ya kujifunza na ili ajifunze vyema ni lazima ahudhurie skuli kama ambavyo wavulana wanahudhuria,''anasema. 

Utafiti kutoka taasisi ya haki ya elimu nchini Tanzania unaonesha wasichana hukosa siku nne hadi saba za masomo  kutokana na kuwa kwenye siku zao za hedhi

Hali hii inapelekea wanafunzi wanawake kukosa fursa ya kufanya  baadhi ya mitihani na hivyo ufaulu wao kushuka kutokana na kukosa cha kujihifadhia wakati wa kupata siku zao

Mradi huo wa kugawa taulo za kike kwa wasichana kwa skuli za msingi na sekondari umewafikia  wanafunzi wa skuli ya Machui, Jendele, Eden kwa  upande wa Unguja  

Tatu Shaban ni Mwalimu mkuu skuli ya msingi Jendele, Mkoa wa kusini Unguja wilaya kati, amesema bado kuna changamoto ya wasichana kutokuhudhuria masomoni wakiwa na sababu mbalimbali ikiwemo ya kukosa taulo zao.

''Wasichana hulazimika kubaki nyumbani mpaka siku zake za hedhi zimalizike, ndio arudi skuli kutokana na kukosa cha kujihifadhia, hivyo hukosa masomo kwa kipindi karibia siku saba, lakini wakipatiwa misaada hiyo ya taulo hawana sababu ya kubaki nyumbani,’’amesema.

Anaeleza kuwa, hii ni mara  ya pili kupata msaada wa  taulo za kike, kwa wasichana wa skuli ya Jendele, ambapo mara kwanza walipata kwa mwaka mzima na mara pili kwa miezi sita.

Ashura Said ni mwanafunzi wa darasa la saba katika skuli hiyo, amesema hii ni mara ya pili kupata taulo za kike, japo kuwa  alikuwa hakosi vipindi vya masomo, lakini hakuwa na amani wala haimpi uhuru akiwepo darasani.

’’Nashukuru kwa msaada huu mara hii, nakaa kambi kwa ajili mya mitihani zitanisaidia sana kujihifadhi, kwani nimefahamishwa pia jinsi ya kuzitumia,’’amesema Ashura.



Wanafunzi wengine waliofikiwa na huduma ambayo imetokana na jitihada za kiongozi mwanamke  ni   skuli ya Machui msaada wa taulo hizo za kike imekuwa ni mkombozi kwao, kwani awali wakipata siku zao, wakiwa mazingira ya skuli huona aibu kwa vile hutokea ghafla na hulazimika kuazima nguo za kujihifadhia kwa majirani.

‘‘Tumefurahi mno  kupata taulo hizi, ilikuwa tukipata siku zangu tukiwa skuli tunachafuka na kupata aibu sasa inatubidi tuwagongee majirani watusaidie tujisitiri ndio hapo tunarudi nyumbani masomo yanatupita,’’anakumbuka Mwanafunzi huyo wa skuli ya Machui. 

Suala la uongozi kwa mwanamke sio tu la kuteuliwa au kuchaguliwa kiuchaguzi bali hata kujitoa katika jamii na kuonesha uwezo wa kusaidia wengine kwa kutatua changamoto zilizopo.

Kwa mujibu wa waliofikiwa na msaada huo maono ya mwanamke kiongozi Sharon  kuwasadia watoto wa kike taulo  kumewajenga kujiamini  wakiwa skuli pamoja na uhakika wa kutokukusa vipindi vya masomo tofauti na awali.

                                             MWISHO 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch