Skip to main content

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA: MIFUMO YA SHERIA IWE JUMUISHI KWA WATU WOTE'

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

TUME ya Kurekebisha sheria Zanzibar, imesema itaangalia kwa kina, juu ya mifumo ya sheria, ili isiwaweke nje ya utaratibu watu wenye ulemavu, katika mapambano dhidi ya udhalilishaji wa wanawake na watoto.

Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa Tume hiyo, Mussa Kombo, wakati akikikfungua kikao kazi, cha kupokea maoni ya wadau wa haki jinai, kuelekea marekebisho ya Sheria ya Adhabu nambari nambari 6 ya mwaka 2018 na ile ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai nambari 7 ya mwaka 2018, kilichofanyika ukumbi wa wizara ya Fedha Gombani.

Alisema, ni kweli watu wenye ulemavu wanaonekana kuwekwa nyuma kwenye mifumo ya haki jinai, kuanzia kuchukuliwa maelezo vituo vya Polisi, ushahidi mahakamani, kujitetea jambo ambalo, linaweza kuwa chanzo cha kuwakosesha haki zao.

Alieleza kuwa, kupitia marekebisho hayo na kwa kuzingatia maoni yaliotolewa, watahakikisha kundi hilo sasa linawekewa kifungu maalum ndani ya sheria hizo, ili iwe sababu ya kuunga mkono mapambano hayo.

‘’Ni kweli kama kuwepo mkalimani wa lugha ya alama katika mahakama zetu halipo moja kwa moja kisheria, ni changamoto, ambayo inahitajika kuangaliwa upya,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Katibu huyo wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, alisema wakati umefika sasa, kwa taasisi zinazoshughulikia kesi za udhalilishaji kujenga umoja wa kikazi, ili kukomesha matendo hayo.

‘’Kwa mfano, ikiwa hakimu mmoja aliyemtia hatiani mshitakiwa wa kosa la ubakaji, anamfunga miaka 20 na hakim mwingine kwa kosa kama hilo anamfunga miaka 15, hapa ipo shida,’’alifafanua.

Aidha Katib huyo, aliitaka jamii kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali, katika kupambana na kudhibiti matendo ya ukatili na udhalilishaji.

‘’Moja ya wajibu wa jamii, kwanza ni kufika Polisi na mahakamani kutoa ushahidi kwa kile walichokiona, kusikia, kushuhudia katika mtiririko wa kosa ambalo, limeshafikishwa mahakamani,’’alieleza.

Baadhi ya washiriki hao, wakitoa maoni yao kwenye kikao hicho kazi, walisema moja ya eneo ambalo linatakiwa kutiliwa mkazo, ni usimamizi wa sheria, ambazo zimekubaliwa kutumika.

Mratib wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania ‘TAMWA’ Ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema ni mapema mno, kuurejesha umri wa mtoto, kutoka miaka 17 ya sasa na kuweka miaka15.

Nae mjumbe wa Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, alisema lazima mifumo ya haki jinai, iwe jumuishi kwa makundi kadhaa ya watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake, Maryam Mohamed Muhene, alisema ni vyema sheria ikaweka kifungu kinachozuia mtu kumtumia mtoto kama mfanyakazi wa ndani.

Nae mshiriki Rashid Abdalla Mshamata, alisema bado elimu inahitajika kwa jamii, juu ya athari ya kuendelea kufanya matendo ya ukatili na udhalilishaji.

Hata hivyo mwakilishi wa Dawati la jinsia na watoto la Wete Said Mohamed Ali, alisema uwepo wa mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji, imesaidia kupunguza, kwa matendo hayo ndani ya jamii.

‘’Lakini changamoto ambayo inajitokeza na huenda ikaathiri kama haikufanyiwa kazi, ni baadhi ya mahakimu kuchelewa kusoma hukumu na wakati mwingine hadi kufikia mieizi miwili,’’alieleza.

Nae Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba ‘PPC’ Bakar Mussa Juma, alisema yapo mazingira ya mtoto anayafanya na kisha kubakwa, ingawa wazazi na walezi huwa chanzo.

Kikao hicho kazi, ni muendelezo wa mikutano inayofanywa na Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, ya kukusanya maoni ya kiutafiti juu ya sheria za Adhabu na ile ya Mwenendo wa Makosa ya jinai, zote za mwaka 2018.

Tume ya Kurekebisha sheria, imeanzishwa kwa sheria ya Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, nambariu 16 ya mwaka 1986, na kupewa jukumu la kufanya mapitio ya sheria zote za Zanzibar au eneo fulani la sheria husika.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch