Skip to main content

WANAKISOMO CHA WATU WAZIMA WAOMBA MIWANI YA KUSOMEA

 

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@


WANAKISOMO cha madarasa ya Elimu ya watu wazima kisiwani Pemba wameiomba Wizara pamoja na wafadhili kuwasaidia miwani, ili waepukane na usumbufu wakati wa kusoma na kuandika.

Walisema kuwa, madarasa hayo ambayo kwa asilimia kubwa ni wanafunzi watu wazima, wakati mwengine wanashindwa kusoma wala kuandika kutokana na kupungua kwa nuru ya macho.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi katika vijiji tofauti, ikiwemo Mjinikiuyu shehia ya Minungwini Wilaya ya Wete,wanakisomo hao walisema wana shauku ya kujifunza zaidi ingawa wakati mwengine inawapa wakati mgumu kuhudhuria darasa.

Walisema kuwa, kuna haja kwa Wizara ya Elimu pamoja na wafadhili wengine kuwasaidia kwa kuwapatia miwani, ili wahudhurie darasani wakiwa na hamasa ya kusoma na kuandika kwa bidii.

Mmoja wa wanafunzi hao Viwe Yusuf Malik mwenye miaka 70 alieleza kuwa, anahudhuria darasa siku zote walizopangiwa lakini inapofika wakati wa kuandika ama anapoambiwa asome kwenye ubao macho yanamsumbua sana.



"Kusoma nimeshajua vizuri kiasi lakini shida yangu ni kuwa na uoni hafifu, hii inaniumiza sana kwa sababu mwalimu anapoandika ubaoni nataka nisome ili nipate uzoefu zaidi, ingawa nashindwa," alisema bibi huyo.

Kwa upande wake mama wa miaka 65 ambae hakutaka jina lake litajwe alieleza kuwa, walipoanza mwanzo kusoma walikuwa wanaona vizuri, ingawa kila umri unapokwenda mbele na wao wanapungua nuru ya macho, hivyo wanahitaji kusaidiwa.

"Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali pamoja na taasisi nyengine ikiwemo TAMWA na PEGAO zinajitahidi kutusaidia vifaa vya kuandikia na kujifunzia lakini hii miwani bado hatujapatiwa na tuna uhitaji mkubwa," alieleza.

Mwanakisomo Aisha Omar Issa mwenye umri wa miaka 35 alieleza, wamekuwa wakitumia jituhada za ziada kwa kusoma na kuwataka wazee hao waitikie ili wajisikie vizuri katika darasa hilo, hivyo ipo haja ya kupewa miwani kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kusoma na kuandika mara kwa mara.

Mwalimu wa darasa hilo Maryam Juma Hamad alisema, katika darasa lake la wanafunzi 42 kuna vijana na wazee ambao kwa sasa wana uoni hafifu unaohitaji kisaidizi cha miwani.

"Ni miaka minne tangu tuanze darasa hili la watu wazima na wanafunzi wangu wa bidii sana ya kusoma na kuandika, hivyo naomba wasaidiwe miwani," alisema.

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said alisema, wakati wanahamasisha wanajamii umuhimu wa mwanawake kuwa kiongozi waligundua kuwa, wengi wanashindwa kutokana na kutokujua kusoma na kuandika na ndio maana wakaamua kuanzisha madarasa hayo kwa ajili ya kuwasaidia.

Nae Mratibu wa mradi wa SWIL Pemba Dina Juma Makota alisema, ukosefu wa miwani kwa wanakisomo cha watu wazima ni changamoto kubwa ambayo bado haijapatiwa ufumbuzi, hivyo watafanya juhudi za makusudi kuhakikisha inapatikana.



Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim alisema, wamekuwa wakiwahamasisha wanafunzi hao kuwa pale Serikali inapopata wataalamu wa kambi za macho wafike haraka ili wapimwe na kupata huduma ya miwani kwani Wizara ya Afya kila baada ya kipindi fulani hutoa huduma hiyo na bila ya malipo.

"Haya madarasa mengi yapo vijijini na hizi kambi mara nyingi huwepo mjini kwa hiyo baadhi ya wananchi hukosa taarifa jambo ambalo ni changamoto, lakini tunatumia madarasa hayo kuhamasisha na kuwapa taarifa ya ujio wa madaktari bingwa wanaokuja ili kupima na kupewa huduma ya miwani," alifafanua.

Mdhamini huyo aliwataka wanakisomo hao licha ya changamoto hiyo waliyonayo, waendelee kujifunza kwa moyo mkunjufu ili kujinufaisha na kuwasaidia watoto wao kupata elimu bora kwa maisha yao ya baadae.

                                                                    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch