Skip to main content

RUZUKU YA TASAF KWA WALENGWA PEMBA YAGEUKA KAA LA MOTO , TASAF YATOA UFAFANUZI

 




NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@

MFUKO wa Maendeleo ya Jamii Tanzania ‘TASAF’ kupiti mpango wa kunusuru kaya maskini, umekua ni kama kivuli, wakati wa kiangazi eneo la jangwani.

Mpango huu wa kunusuru kaya masikini, toka kuanza kwake nchini umeweza kusaidia wananchi wengi, waliokuwa kwenye jua kali la kimaisha, na sasa wamepata kuvuli.

TASAF kupitia miradi yake mbali mbali ya maendeleo, imeweza kuwakomboa wananchi wengi kiuchumi, ambapo wengi wao wamekomboka kimaisha.

Wananchi wa shehi ya Ving’ambwa kijiji cha Vikunguni ni moja kati ya wanufaika wa mpango huo, ambapo baadhi ya wanufaika hao wameanza kupata mafanikio makubwa kupitia miradi hiyo.

Iko misemo mingi ya kiswahili ukiwemo mtaka cha mvunguni sharti ainame’, wengine wakasema ‘abebwae hujikaza’ mgagaa na upwa hali wali mkavu ikiwa na maana pana kwa mujibu wa jambo lenyewe.

WALENGWA VIKUNGUNI CHAKE CHAKE

Fatma Khamis Mbarouk mkaazi wa Vikunguni shehia ya Ng’ambwa Chake Chake, ni miongoni mwa wanufaika, anasema kwa sasa maisha yake yako juu ikilinganishwa na hapo kabla.

Anasema mpango huo uliofanywa na TASAF wa kunusuru kaya masikini  tokea kuanza kwake, umesaidia na kuwakomboa wananchi wengi, akiwemo yeye.

Yeye kila baada ya mwezi hupata ruzuku ikiwemo ya watoto wanaokwenda skuli kuanzia msingi hadi sekondari na Klinik, ingawa kwa upande wa hutofautiana kati ya mlengwa mmoja na mwengine.

“Wapo wanaopata ruzuku ya shilingi 30,000 hadi shilingi 40,000 na zipo fedha nyengine ambazo kila mlengwa hupatiwa na mfuko huo ambazo ni shilingi 20,000 anaeleza mlengwa huyo.

Fatma, anasema kinachompa uhakika wa maisha na hasa baada ya ujio wa TASAF, ambapo pamoja na ruzuku ya msingi anayoipata, lakini anafurahishwa na kuwepo kwa ajira za muda.

‘’Hata uchimbaji wa mitaro, misingi ya barabara au ujenzi wa matuta ya kinga ya maji, tukiyafanya kwa ajili ya wananchi wote, tunalipwa ujira wetu,’’anasema.

Aisha Maliki anasema kwake TASAF ni kama mkombozi wa wanyonge nchini, ambapo wengi wao wameweza kuona njia kiuchumi, kutokana na fedha za ruzuku wanazopewa.



‘’Kwa hakikia TASAF kwangu imekuwa kama mtoto wangu wa kumzaa, jinsi na namna inavyonienzi hasa katika eneo kukuza pato na uchumi wangu,’’anaeleza.

Anaona TASAF kuandaa mpango huo kwa makusudi, umechangia kwa kiasi kikubwa kuwatoa wananchi walio wengi kwenye unyonge na umaskini hasa wa kipato.

‘’Kwa hakikia TASAF imetusaidia mno, maana tumekuwa tukipata ruzuku ambazo sasa tumeshazihamishia kwenye vikundi vya ushirika na sasa tumeshauaga umaskini,’’anaeleza.

CHANGAMOTO KWA WALENGWA

Aisha Massoud Mohaamed, anasema moja ni fedha zao kuingizwa kwenye mfumo wa kielektroniki, ambapo upatikanaji wa ruzuku hiyo moja kwa moja, huwa mgumu.

Anainisha kuwa, TASAF awali walikuwa wakikabidhwa fedha mkononi, na sasa baada ya kuwepo kwa ulazima wa rukuzu yao kupita benki ama njia za kisasa, wamekuwa wakipata changamoto.

‘Mara unakumbana na mkato usiootegemea, mara unakwenda kwa wakala hana salio na wakati mwengine mfumo unakuacha hupati kabisa, na hapo ndio unarudi kwenye umaskini,’’analalamika.

Bimkubwa Issa anasema, hata mfumo wa wao kwenda benki kutoa fedha zao, ni changamoto inayowaumiza, hasa kutokana na hali zao za kipato kuwa kidogo kisha kukumbana na mikato ya benki.

“Chakushangaza tunapokwenda benki au kwa mawakala kutoa fedha katika akaunti zetu, fedha hazitoki kamili kama tulivyoambiwa hapo mwanzo, hivyo tunaomba kama kunamakato yoyote,” anafahamisha.

Hata Salma Ali Mohamed na wenzake Fatma Khamis Mbarouk, na Mtumwa Ali Omar wakaazi wa shehia ya Vikunguni, wanaoma kero kubwa kwao ruzuku waliokusudiwa wao kisha kuingia kwenye mfumo wa mikato.

Waliiomba Tasaf kuendeleza mfumo huo kuwaangalia wananchi wenye hali duni kiuchumi, hasa kwa wale ambao hawajabahatika kufikiwa kwa fursa hiyo kuwasaidia kwa njia moja ama nyengine ili nao waondokane na utegemezi.

Asha Rashid Khamis mkaazi wa Vikunguni ameishukuru Tasaf kwa kuwaona wananchi wenye hali duni kiuchumi, kwa kuwapatia fedha za kuwasaidia watoto wao kwa matumizi ya Skuli, Afya na mahitaji mengine ya lazima.



SHEHA

Sheha wa shehia ya Vikunguni Issa Rihani Abass, anasema kuwa katika shehia yake wapo wananchi 2, 500 kati yao wananchi 226 ndio wanufaika wa mradi wa kunusuru kaya masikini kupitia TASAF.

Anasema TASAF imewakomboa wananchi wa shehia yake kwa kuwepo kwa vikundi kwa njia moja ama nyengine, wanachama wake wameondokana na umasikini.

“Nashukuru katika shehia yangu TASAF imewakombowa wananchi wengi waliokatika umaskini baada ya kuwapatia miradi kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini”, anasema.

Kuhusu changamoto za fedha za ruzuku kupitia kwenye mfumo wa kielektroniki na benki, anasema limekuwa changamoto kwa wananchi hao waliotarajiwa kuondolewa na umaskini.

‘’Kwa hakika tunazo taarifa kuwa mfumo huo umezaa changamoto, na TASAF tumeshawapelekea, kwa hivyo wanazifanyia kazi ili kuona walengwa wetu wanakuwa huru kupata fedha hizo. 

TASAF

Mratibu wa TASAF Pemba Mussa Said, anasema kumekuwa na malalamiko mengi kwa walengwa wao, aingawa anaona inatokana na uwelewa kuwa chini juu ya mifumo.

“Wengi wao hutoa pesa kwa mawakala bila kujua kima cha fedha kilichomo na kilichobaki kwenye akaunti, hivyo kupelekea kuwepo kwa changamoto hiyo kwa walengwa,” anaeleza.

Ndio maana akashauri kuwa, kutokana na changamoto hiyo, ni vyema kwa walengwa husika kutoa fedha zao benki, ili kuondokana na malalamiko yasiyokuwa ya lazima.

Anafahamisha kuwa kwa sasa suala hilo haliwezi kuepukika kirahisi rahisi kutokana na mfumo wa malipo ya Serikali kufanyika kwa mfumo huo wa kutoa benki.

Ingawa anaeleza kuwa, TASAF kwa sasa imo kwenye mazungumzo na Benki, ili walengwa wa kaya maskini wasiweze kukatwa fedha zao pale wanapokwenda kutowa fedha zao.

Aidha anawashauri walengwa ambao uelewa wao ni mdogo katika kujua salio lao wanapotaka kwenda kutoa fedha zao kwenye akaunti, kuhakikisha wanachukua ndugu zao wenye uelewa.  

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Tanzania, Mkurugenzi Uratibu TASAF Haika Shayo, alisema baada ya kuzuka malalamiko, walikaa na viongozi wa serikali za mitaa, kuwapa mafunzo ya ufafanuz ambayo anaamini yamesaidia kufanikisha lengo la mpango, na kupunguza malalamiko.

 “Sote tunafahamu lengo ni kuwa na uwelewa wa pamoja na kuweza kuwahudumia walengwa, mutakuwa mabalozi wa mpango kwa kuwafahamisha wananchi wetu pale wanapokuja katika shehia zenu,” alisema.

Naye Ofisa ufuatiliaji na tathmini wa TASAF Pemba Abrahman Khamis, anasema changamoto zilizomo kwenye mfumo, anatarajia sasa masheha na madiwani wawaelimishe walengwa wao.

Hata hivyo kwa upande wa masheha waliahidi kwenda kusimamia kikamilifu, shuhuli zote za TASAF zinazofika katika shehia zao, kwani wao ndio viongozi wa Serikali kwenye shehia husika.

Mpango wa kunusuru TASAF ambao ulianza mwaka 2014, upo kwenye shehia 78, na tayari hadi kufikia mwaka 2019, zaidi ya shilingi bilioni 14.4 zimeshawafikia walengwa kwa Pemba pekee.

Kwa hilo sasa walengwa hao 14,280 wamefanikiwa kuanzisha vikundi 942 kati ya hivyo 700 vimeshasajiliwa, kwa ajili ya kuendeleza miradi kama ya ufugaji, kilimo, kuweka na kukopa, wakitokea shehi za Ng’ambwa, Kinyasini, Chimba, Kiwani, Konde, Makangale, Ndagoni pamoja na Tumbe.

                      MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch