Skip to main content

KIKUNDI CHA 'KHERI LIWE" KENGEJA WAANZA KUONA MWANGA, WAIPA TANO TAMWA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

KIKUNDI cha ‘Kheri liwe’ kilichopo Likoni shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, kimesema mafunzo, mawazo na fikra walizopewa na TAMWA-Zanzibar, sasa zimezaa matunda baada ya kujipatia zaidi ya shilingi milioni 2.8 ikiwa ni faida kwa miaka mitatu iliyopita.

Wanakikundi hao, walisema baada ya kuanzisha mpango wa kuweka fedha na kukopa ‘hisa’ ambao walishawishiwa na TAMWA, na kufanya biashara ndogo ndogo, utengenezaji sabuni na kilimo cha mboga, sasa wameona matunda yake.

Wakizunguma na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, wanakikundi hao, walisema kumbe walichelewa kujikusanya na kama wengeanza miaka ya nyuma zaidi, kwa sasa wengeshapiga hatua kubwa zaidi.

Walieleza kumbe zipo fursa kadhaa endapo jamii itazifanyiakazi kupitia vikundi hivyo, na kisha kuwezeshwa kimafunzo na fikra za jinsi ya kukusanya fedha na kisha kujikopesha wenyewe.

Mwenyekiti wa kikundi hicho Fatma Nahoza Juma, alisema sasa kila mwanachama ameshapata faida, iwe wakati wanapogawana faida au kukopa fedha anapokuwa na shida.

“Kikundi hichi tulikianzisha kama utani, wakaja watendaji wa TAMWA Pemba, wakataka tujiwekee akiba na huku tutafute biashara ambayo wanunuzi ni sisi wenyewe tulifanya hivyo, na sasa tuko vizuri,’’alieleza.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema waliendesha biashara ya bidhaa ya sukari, na hapo walilazimishana kuikopa wanakikundi na kujiingizia faida.

Aliongeza kuwa, pia wanapolima kama mchicha, bilingani na tungule wateja wa kwanza ni wao, na kupata faida ambayo sasa wanajivunia kupitia kikundi chao.

Mshika fedha wa kikundi hicho cha ‘Kheri liwe’ Maimuna Ngwali Ali, alisema paketi moja ya kilo 50 ya sukari walikuwa wananunua kwa shilingi 72,000/= pamoja na gharama za usafiri na kisha wanajipatia faida ya shilingi kati ya 25,000/= hadi shilingi 30,000/=.

Alisema wamekuwa wakifanya hivyo kwa miaka miwili sasa ambapo hujipatia faidi ya shilingi 360,000/= kwa mwaka na kwa miaka miwili pekee wameshavuna faida ya shilingi 720,000/= kwenye bidhaa ya sukari.

“Utaratibu wetu katika kuhakikisha tunaingiza faida, basi lazima kila mwanachama wetu anunue bidhaa ama atupe faida ambayo tumepanga tuiingize, mfano kila kilo moja ya sukuri, ipo faidi ya shilingi 500/=,’’anafafanua.

Kwa upande wa kilimo cha mboga, ambacho nacho walishauriwa na TAMWA Pemba, wameshajipatia wastani wa shilingi 180,000/= ndani ya miezi sita.

“Kilimo  cha mboga nacho, tunakiendesha na mavuno ya kwanza tulipata shilingi 50,000/= mavuno ya pili 130,00/= na sasa baada ya kuvuna tunatarajia kujipatia wastani wa shilingi 300,000/=,’’alifafanua.

Mshika fedha huyo, ameipongeza TAMWA kwa mpango wao ambao unaelekea kupunguza umaskini, pindi wanaoelekezwa wako tayari kujiletea maendeleo.

Mwanachama wa kikundi hicho, Khalfan Salim Khalfan na mwenzake Rukia Vuai Khamis walisema, vikundi hivyo ni vizuri maana vinatoa heshima ya mwanamke katika jamii.

“Heshima ya mtu ni kazi, ndio maana TAMWA imetupa heshima kwa kutupa mafunzo ya kilimo, sabuni na uwekaji hisa, sasa hatuna wasiwasi,’’alieleza Rukia.

Kwa upande wake, Katibu wa kikundi hicho cha kheri liwe cha Kengeja, Mwajuma Shaban Khamis, alisema sasa wanaangalia kubuni mradi mwengine, wa ufugaji kwa siku zijazo.

Aidha Katibu huyo, aliwataka wafadhili wengine kujitokeza ili kuwawezesha katika ziara za kimafunzo, kwa vikundi vilivyopiga hatua zaidi, ili wazidi kunufaika macho.

“Kwa maendeleo tuliyonayo, lazima tuwapongeze wenzetu wa TAMWA kwa ushauri, elimu, maelekezo na fikra zao na sasa tunajivunia,’’alieleza.

Ofisa Uwezeshaji wa TAMWA- Pemba Asha Mussa Omar, alisema huo ni mpango maalum, ulioandaliwa kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Alisema, ni kweli vipo vikundi kadhaa kisiwani Pemba ambavyo wamekuwa wakiviwezesha, lakini baadhi yao vimekuwa havifanyi vizuri kwa kutokuwa tayari.

“Vikundi vyengine kama kilichopo Mkanyageni, Mavungwa, Mbuzini, Chake chake na hicho cha Kengeja vimekuwa vikijiongeza na kubuni miradi ambayo huzaa tija,’’alifafanua.

Kikundi hicho cha ‘kheri liwe’ cha Kengeja wilaya ya Mkoani ambacho kinajishughulisha na kuweka wa hisa, kilimo cha mboga, utengenezaji sabuni na biashara, kina wanachama zaidi ya 25 na kimeanzishwa mwaka 2008.

                               MWISHO.  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch