NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Pandani kwa tiketi ya Chama cha wananchi ‘CUF’ Maryam Omar Said, amsema kuaniza Juni 29, mwaka huu ametangaaza, kujiengua kwenye chama hicho na kujiunga na CCM, akidai amevutiwa na utekelezaji wa Ilani ya chama hicho, kwa miaka mitano iliyopita. Alisema, ameamua kurudi nyumbani, baada ya kuona yale yote aliyota ndani ya jimbo lake la Pandani, yamekelezwa ikiwemo miradi ya elimu, afya na maji safi na salama kwa miaka mitano iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba alisema, hana sababu ya kubakia ndani ya CUF, na ameamua kuhamia CCM, ili kuungana na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Alieleza kuwa, akiwa ndani ya CUF, hatakuwa na nafasi nzuri ya kushika bango la CCM na ndio maana, ameamua kwa hiari yake na bila ya kulazimishwa, kurudi ndani ya chama hicho. Mbunge huyo mstaafu wa CUF, alisema awali alikuwa mwana CCM, ingawa alitok...
NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA ZOEZI la uchukuwaji wa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum linaendelea kupamba moto, kwa wanawake,wakiwemo wanahabari kupishana ofisi za CCM wilaya za kisiwani Pemba . Zanzibar leo kisiwani Pemba, ambalo limepiga kambi katika ofisi hizo, limeshuhudia wandishi wabahari wanawake, wajasirimali, watendaji wa serikali na waachama wingine, wakitekeleza haki yao ya kidemokrasia. Akizungumza na gazeti hili, mmoja kati ya watia nia hao kwa nafasi ya ubunge Jimbo la Chake chake, Ashura Abdalla Simai 'mabodo', alisema moja ya sababu iliyomsukuma ni kutekeleza haki yake ya kikatiba ya kisiasa. Alieleza kuwa, pindi vikao vya chama vikiridhia jina lake na kurudi, atakwenda bungeni kuwatetea wanawake wenzake na wingine, kwani walio wingi hawajafanya hivyo. “Wanawake wamekuwa wakikosa matetezi kwa kina, wa mambo yanayotuhusu, hivyo nimechukuwa fomu hii kujaribu bahati yangu kwa mara ya tano,”alisema. Afisa hab...