Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

ALIEPITWA KWA KURA MOJA 2020 AIBUKA MSHIDI 2025 KURA ZA MAONI

    'Anasema mwaka huu ndio aliopangiwa na Mungu kuingia jimboni kugombea, ...awaomba wananchi kumchagua'   IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   "Alienipita kwa kura moja 2020, nimempita kwa kura 62 kwenye kura za maoni mwaka huu 2025, hivyo nimeshinda kwa kishindo,"   Maneno hayo ya furaha yalimtoka mgombea uwakilishi Jimbo la Tumbe kupitia chama cha Mapinduzi CCM Salma Khamis Tumu wakati akizungumza na mwandishi wa makala hii huko kijiji kwao.   Salma mwenye umri wa miaka 53 mkaazi wa shehia ya Tumbe Magharibi anasema, ameamini kwamba riziki ya mtu haiendi kwa mwengine bali siku ikifika, itamfika tu mwenyewe.   Pamoja na kushindwa kwenye kura za maoni kwenye uchaguzi uliopita wa mwaka 2020, lakini hakukata tamaa bali ajijipanga kugombea tena 2025, ambapo alipitishwa kwa kura 134 huku mpinzani wake ambae ni mwanamme akijipatia kura 72.   Mgombea huyo anasema, hizo ni baraka za Mungu kumjaalia kupita kwenye nafasi hiy...
Recent posts

UJENZI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA PEMBA, BARABARA CHAKE CHAKE -MKOANI NJIA SAHIHI KUKUZA UCHUMI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ILE dhamira ya Dk. Hussein Ali Mwinyi kuifungua Pemba kiuchumi kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa, sasa imefana. Kwani uzinduzi wa ujenzi wa uwanja huo na barabara ya Chake Chake- Mkoani, umezinduliwa rasmi Septemba25, mwaka huu, katika uwanja wa ndege uliopo Furaha Pemba. Ni furaha kubwa kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, kuona kwamba kitu ambacho wamekisubiri kwa muda mrefu, sasa kinakwenda kufungua uchumi wao. Maana serikali ya awamu ya nane, imedhamiria kufanya mageuzi ya makubwa katika sekta ya usafiri wa anga Zanzibar, kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma katika uwanja wa ndege wa Pemba.   Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amezindua ujenzi huo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, jemedari wa uchumi.   Makamu huyo anasema, ujenzi wa miradi hiyo ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ambapo malengo ya se...

TUME YA HAKI ZA BINAADAMU, YANGONGOMELEA MSUMARI KAMPENI JUMUISHI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ TUME ya haki za binaadamu na utawala bora, ofisi ya Pemba, imetoa wito kwa vyama vya siasa   kuzingatia na kuhakikisha ushiriki wa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni zinazoendelea, kwa kuwawekea mazingira rafiki kwa kuzingatia aina zao za ulemavu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Ofisini kwake Chake Chake Pemba, Afisa Mfawidhi wa tume hiyo Pemba Suleiman Salim Ahmad alisema, katika kuhakikisha ushiriki nzuri wa watu wenye ulemavu katika   upigaji kura, ni vyema ni vyema vyama vya siasa   kuhakikisha ujumuishi wao katika kampeni zinazoendelea. Alisema kwamba, mazingira mazuri kwa watu wenye ulemavu katika mikutano ya kampeni itasaidia kufuatilia sera zinazotolewa na wagombea wa vyama vya siasa katika nafasi za Urais, Uwakilishi, Ubunge na Udiwani, jambo litakalopelekea kuchagua viongozi wanaowataka kwa usahihi. Alisema kua, pamoja na jitihada mbali mbali zinazofanya na wadau   na watetezi wa haki za binaada...

NCHIMBI AONA MBALI MIAKA 5 IJAYO CCM IKIRUDI MADARAKANI

MGOMBEA MWENZA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dk. Emanuel John Nchimbi amesema, katika miaka mitano inayokuja wamedhamiria kuongeza kasi ya zoezi la utafiti wa rasilimali za bahari, ili wananchi wapate maisha bora, kwani uchumi wa buluu umeleta mafanikio makubwa katika nchi. Dk. Nchimbi ameyasema hayo wakati wa mkutano wa mkuu wa kampeni uliyofanyika katika viwanja vya Kinyasini Jimbo la Gando Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema,  wanayo imani na matumaini makubwa kwamba ndani ya bahari kwa upande wa Pemba kuna rasilimali nyingi ambazo zitawasaidia wananchi kuwa na maisha bora, hivyo ilani ya CCM ya mwaka 2025/2023 imeweka wazi suala la kuongeza kasi ya zoezi la utafiti, ili kuimarisha zaidi uchumi wa wananchi. "Pia tutaimarisha ufungaji wa samaki, vizimba vya samaki na ukulima wa zao la mwani ili kuinua kipato cha wananchi na kuwaletea manufaa katika familia zao," alisema Dk. Nchimbi. Dk. Nchimbi alisema kuwa, anaamini kwamba chama kitap...

MTUMWA SULEIMAN: MGOMBEA UDIWANI ANAEPANIA KUMALIZA CHANGAMOTO

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@  "WANANCHI wa Wadi yangu wana upendo na mimi, nilipochaguliwa walinifurahia sana, hivyo sina wasiwasi na ushindi,"  Hayo si maneno ya mtu mwengine bali ni ya Mtumwa Suleiman Salum mwenye umri wa miaka 41 mkaazi wa Ole Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Mtumwa ambae ni mgombea udiwani Wadi ya Ole kupitia chama cha Mapinduzi CCM, anasema atakapofanikiwa kuchaguliwa atahakikisha wananchi wake wanafurahi zaidi, kwani atawashirikisha kila hatua ili kuona wanafanikiwa kwa haraka. Anaeleza, Wadi yake ni tofauti na nyengine kwani hata wananchi wa vyama vya upinzani wanampenda na kumuunga mkono, kutokana na kuwajali bila kuwabagua, hivyo anaimani atachaguliwa kuwa diwani wa Wadi hiyo. Wananchi wa Wadi yake walifurahi sana kuona kiongozi huyo mwanamke amepitishwa na wajumbe ili aweze kushika nafasi hiyo, kwani wanaamini kwamba, changamoto zao nyingi zitapatiwa ufumbuzi kipindi kitakachokuja. "Kwa kweli sina wasiwasi na nafasi hii na ...

JAMII YATAKIWA KUDHIBITI MABADILIKO YA TABIANCHI

   IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Mwamvuli wa Asasi za Kiaraia Zanzibar (ANGOZA) Hassan Khamis Juma amesema, kutokana na maeneo mengi kuathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi kisiwani Pemba, kuna haja kwa wadau kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanadhibiti hali hiyo katika jamii. Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa masuala ya mabadiliko ya tabia nchi katika Ukumbi wa Wizara ya Kilimo Pemba, Mkurugenzi huyo aliwataka kuyafanyia kazi mafunzo hayo kwa ajili ya kujenga mazingira bora ya sasa na baadae. Alisema kuwa, wamejikita kutoa mafunzo hayo hasa kwa wananchi wanaoishi maeneo ya ukanda wa bahari, ili kuelimisha jamii katika udhibiti wa mabadiliko ya tabia nchi ambayo yameathiri sehemu mbali mbali kisiwani hapa. "Tunaamini kwamba elimu hii tutaitumia ipasavyo katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ili mulete mabadiliko chanya katika jamii," alisema Mkurugenzi huyo. Aidha aliwataka kufanya kazi vizuri ili wanajamii waelewe, ...