Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

SERIKALI YAAHIDI KUZISIMAMIA HAKI, FURSA ZA WATU WENYE ULEMAVU

NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amesema serikali itaendelea kulijali kundi la   watu wenye ulemavu, ili kuhakikisha wanapatiwa haki zao msingi, ikiwemo za uongozi na uchumi.   Hayo aliyasema leo Septemba 16, 2025 kwenye hutuba yake, iliyosomwa kwa niaba yake na Katib tawala wilaya ya Micheweni Sheha Mpemba Faki, alipokuwa akifungua kongamano la wadau wa maendeleo jumuishi katika jamii, lililofanyika skuli ya Utaani Pemba. Mkuu huyo mkoa alisema, serikali imewapa haki na fursa na kuwathamini pamoja na kuwaunga mkono, watu wenye ulemavu kama walivyo watu wingine.   Alieleza kuwa, watu wenye ulemavu wamepewa fursa kubwa ya kushiriki katika kupiga kura na kuchagua viongozi, wawatakao, kama msingi wa sheria mama katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilivyoekeleza kifungu cha 7 na ch 12.   "Niwatoe hofu nyinyi watu wenye ulemavu, mnayo fursa kubwa ya kushiriki kikamilifu katika harakati mbali mbali zikiwemo za kisi...
Recent posts

'KIST' CHAFUNGUA TAWI PEMBA, VIJANA WAITA KUJIUNGA

NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ MAKAMU wa Pili wa Rais wa  Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla  amesema, kufunguliwa kwa Tawi la Taasisis ya Sayansi na Teknolojia ya  Karume Pemba kutasogeza kwa karibu huduma za masomo ya sayansi na teknolojia kwa wananchi na kutoa fursa kwa vijana kujiendeleza kielimu wakiwa kisiwani Pemba badala ya kufuata masomo nje ya kisiwa hicho. Ameyasema hayo leo Septemba 16, 2025 wakati akifungua Tawi la  chuo cha Sayansi na Teknolojia ya Karume Pemba katika viwanja vya Mnazimmoja Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.    Amesema, Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume inatoa mchango mkubwa katika kukuza taaluma ya Sayansi na Teknolojia ndani na nje ya nchi sambamba na kupata mafanikio mengi ikiwemo kuongezeka kwa wataalamu wa fani ya Sayansi na Teknolojia nchini na Barani Afrika kwa ujumla.   Alieleza kuwa, uwepo wa Tawi hilo kutafungua milango ya kuitangaza Pemba kielimu katika nyanja za sayansi na Teknolojia na kuwavutia watu we...

‘AAFP’ CHAWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

  NA MARYAM SALUM, PEMBA @@@@   MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wakulima, ‘AAFP’ Said Soud Said amewataka wananchi, kutokubali kushawishiwa na mtu au chama, kuchafua amani, na badala yake kuilinda na kuitunza kwa maslahi ya umma.   Alitoa wito huo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, wa kampeni kwa chama hicho, uliofanyika Kiuyu wilaya ya Wete Pemba.   Alisema kuwa, suala la uwepo wa uchaguzi wa vyama vingi, hakuna uhusiano wowote na uvunjifu wa amani, hivyo ni vyema kila mmoja kuliheshimu hilo.   Alieleza kuwa, siasa, mikutano ya kampeni na hatimae uchaguzi wa kuwachagua viongozi mbali mbali, ni jambo la kupita, ingawa kuichafua amani na kuirejesha ni jambio zito.   Mgombea huyo wa urais, aliwaasa wananchi hao na hasa vijana, kujitenga mbali na chama ama kundi la watu, lenye dhamira ya kutaka kuchafua amani ya nchi. ‘’Mimi nikiwa mgombea urais wa Zanzibar, niwaeleze kuwa, kwanza tuichaguweni amani na kisha ndi...

WATU WENYE ULEMAVU WA UZIWI, WATAKA WAKALIMANI TAASISI ZA UMMA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ Watu wenye ulemavu wa Uziwi wameziomba taasisi Serikali na binafsi   zinazotoa huduma mbali mbali za kijamii, kuweka wa kalimani wa alama katika taasisi hizo ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watu wote. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti   watu wenye ulemavu wa uziwi walisema, wamekua wakichelewa   kupata huduma bora na stahili katika baadhi ya taasisi   kutokana na kutokuwepo mawasiliano mazuri kati yao na watoa huduma, hali inayosababishwa na upungufu wa wakalimani wa   lugha za alama katika taasisi hizo. Mmoja kati ya watu wenye ulemavu wa uziwi Zuhura   Kombo Omar kutoka Mjimbini Mkoani Pemba alisema, katika taasisi nyingi za utoaji huduma za kijamii   kumekua na uhaba wa wakalimani wa lugha ya alama hali inayosababisha kutopata huduma bora na kwamuda sahihi. Alisema kukosekana kwa wataalamu hao unasababisha kutokuwepo kwa mawasiliano mazuri jambo linalosababisha ...

UZINDUZI KAMPENI CCM PEMBA, WAANZA KWA NEEMA YA USHINDI, 453 KUTOKA ACT WAMFUATA DK. MWINYI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema akipata ridhaa ya kuongoza nchi, miaka mitano ijayo, anakusudia kuwapa hatimiliki wakulima wa zao la karafuu, wanaomiliki mashaba ya eka.     Dk. Mwinyi aliyasema hayo jana Septemba 15, 2025 katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM katika kiwanja cha Gombani ya Kale, wilaya ya Chake chake kisiwani Pemba.   Alisema hatua hiyo itawezesha wamiliki hao kuzalisha kwa wingi na hata pale watakapofariki basi, warithi wao wanaweza kuyarithi, kisheria kwa ajili ya kuyaendeleza.   Mgombea huyo alisema CCM ikiendelea kushika dola basi hayo yote yatatimia kwa asilimia 100, kama ilivyofanya kwa awamu iliyopita.   Alifahamisha kuwa, wamiliki wa mashamba hayo ya eka, wamekuwa wakipata changamoto kwa kule kuyatunza, kisha kukosa hata kukodishwa wao.   ‘’Naomba mnipe ridhaa ya kuiongoza tena Zanzibar, n...