Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

WATUMISHI WAPYA WIZARA YA ELIMU PEMBA WAPEWA NENO

NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WATUMISHI  wapya wa   wizara ya elimu na mafunzo ya Amali Pemba, wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni za utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji katika utendaji wao. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu Idara ya uratibu na Utumishi kutoka wizra ya elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar Harith Bakari Ali, wakati akifungua mafunzo ya kuthibitishwa kazi kwa waajiriwa wapya yaliofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Michakaini Chake chake Pemba. Alisema ufanisi wa kazi hutokana na kufuatwa ipasavyo kwa Sheria, miiko na maadili ya kazi ambayo humtengeneza mtumishi kua muawajibikaji katika utendaji wake wa kila siku ndani na nje ya eneo la kazi. "Sheria,   maadili,   kanuni na miiko ya kazi ndio kichocheo muhimu cha uwajibikaji kwa mtumishi wa Umma, hivyo ni muhimu kuyazingatia yote haya ili kufanya kazi zenu vizuri na si katikamaeneoyakazi tu bali hata nje ya kazi, alieleza. Alisema kua   kipengele chengine muhimu ...
Recent posts

Mkurugenzi TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia

  Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio nguzo kuu ya TAMWA...

MIAKA 62 YA MAGEUZI MAKUBWA YA SEKTA YA AFYA KUTOKA UHABA, MARADHI NA VIFO VINAVYOZUILIKA HADI HUDUMA ZA KISASA KISIWANI PEMBA.

  HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ Mapinduzi ya 12 Januari 1964 ni tukio la kihistoria lililobadili mwelekeo wa maisha ya Mzanzibari katika nyanja zote za kijamii.   Mapinduzi ya mwaka 1964 yalikuwa ni Mapinduzi ya uhai yakitambua kuwa bila afya bora, hakuna maendeleo, hakuna elimu, wala hakuna uchumi.   Miaka 62 ya mapinduzi hayo, sekta ya afya Zanzibar nzima inasimama kama ushahidi usiopingika kwamba Mapinduzi yamelinda  maisha ya wananchi kwa vitendo.   KABLA YA MAPINDUZI Kiuhalisia kwa upande wa kisiwa cha Pemba  kabla ya Mapinduzi matukufu ya 1964, huduma za afya zilikuwa katika hali ya kusikitisha. Kwa vile Zanzibar nzima ilikuwa na hospitali kuu moja tu ya  Mnazi Mmoja ni wazi kuwa kwa upande wa Pemba ilikuwa na huduma finyu sana za afya. Hakukuwa na hospitali kuu badala yake kulikuwa na hospitali 2 ya Chake chake na Wete, kwa upande wa vituo vya afya vilikuwa ni 14 tu huku vikiwa  havina dawa wala wataalamu wa kutosha. ...