UONGOZI WA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) UNAYOFURAHA KUWAALIKA WAHITIMU WOTE WA MWAKA WA MASOMO 2024/2025, PAMOJA NA WAZAZI, WALEZI, NDUGU, JAMAA, MARAFIKI, NA WADAU WOTE WA MAENDELEO YA ELIMU, KUSHIRIKI KATIKA MAHAFALI YA 23 YA CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU). MAHAFALI HAYO YANATARAJIWA KUFANYIKA SIKU YA JUMATANO YA DISEMBA 17, MWAKA 2025, KATIKA KIWANJA CHA CHUO KIKUU TUNGUU KIBELE UNGUJA, KUANZIA SAA 2: 00 ASUBUHI. AMBAPO KATIKA MAHAFALI HAYO PAMBE, MGENI RASMI ANATARAJIWA KUWA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK. HUSSEIN ALI MWINYI. UONGOZI WA CHUO UNAWASHAURI WAHITIMU WOTE, KUKAMILISHA TARATIBU ZOTE IKIWA NI PAMOJA NA KUCHUKUWA MAJOHO KUANZIA SIKU YA ALHAMISI YA TAREHE 11 HADI TAREHE 15. MAZOEZI YA MAHAFALI 'REHASAL' ITAFANYIKA TAREHE 16 DISEMBA, 2025 SAA 2:00 ASUBUHI. HIVYI BASIII......WATU WOTE WANAKARIBISHWA KUSHEREHEKEA MAHAFALI HAYO. KUMBUKA KUWA......CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR (ZU) NI CHEM CHEM YA MAADILI NA TAALUMA. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA SIMU...
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI SIKU YA HAKI ZA BINADAMU DUNIANI 2025 Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaungana na wanaharakati, wanahabari, na watetezi wa haki za binadamu duniani kote, kuadhimisha siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka. Kaulimbiu ya mwaka huu, haki za binadamu kama “Mahitaji ya Kila Siku”, inasisitiza kuwa haki hizi lazima zilindwe bila kusuasua kila siku, kwa kila mtu, na katika kila mazingira. Katika maadhimisho ya mwaka 2025, ZAMECO inasisitiza kwamba uhuru wa kupata na kutoa taarifa ni nguzo muhimu ya utawala bora na msingi wa kulinda haki nyingine zote za binadamu. Haki hii haipaswi kutazamwa kama ridhaa ya mamlaka bali kama wajibu wa kikatiba na kimataifa unaopaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekelezwa. Tunawakumbusha wadau wote kuwa tangu kupitishwa kwa Tamko la Ulimwengu la Haki za Binadamu (UDHR) mwaka 1948 uhuru wa kujiele...