Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

ANNA ATAJA FAIDA LUKUKI ZA ELIMU KWA MTOTO WA KIKE

  NAIBU Waziri wa Maendeleo wa Jamii Jinsia Wazee na Watoto Anna Athanas Paul amesema iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao. Ameeleza jayo katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mtoto wa kike huko katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Kampas ya Maruhubi Unguja. Amesema   watoto wa kike wakisoma kwa bidii itasaidia kutimiza malengo yao ya baadae hali ambayo itasaidia kujiepisha na vitendo viovu ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia. “Iwapo mtoto wa kike atasoma kwa bidii ataweza kuviepuka viashiria vya unyanyasaji ambavyo ndio vikwazo vikubwa vinavyowafanya kutokufikia malengo yao ” Amesema Waziri huyo. Naibu Waziri huyo amefahamisha kuwa kwa mujibu takwimu kutoka Afisi ya Mtakwimu Mkuu mwaka 2023 matukio 1954 ya ukatili na udhalilishaji yaliripotiwa kati ya matukio hayo wasichana walikuwa 1263 sawa na aslimia 77.1 hiyo inaonesha bado watoto wa kike wanah
Recent posts

VOSHOKA WA UBAKAJI PEMBA KIKAANGONI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAMTANDAO wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji kisiwani Pemba, wamelaani kitendo cha watu wazima, kukimbilia kwa watoto wachanga, kuwadhalilishaji, kwani husababisha athari zaidi kwao. Walisema, miongoni mwa athari hizo ni kuwasababisha kukosa kizazi, kuwatishia masomo, athari za kisaikolojia jambo ambalo linatajwa kuzima ndoto zao za maisha. Wakizungumza kwenye kikao cha kuwasilisha ripoti za kazi zao, kilichofanyika ofisi ya TAMWA Pemba, walisema, sasa vitendo hivyo wadhalilishaji wameelekeza nguvu zaidi kwa watoto wadogo. Walieleza kuwa, zipo kesi kadhaa zinazowahusu watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi 10, wakifanyiwa udhalilishaji na wanaume wenye umri kuanzia miaka 40 hadi 50. Mwanamtandao kutoka wilaya ya Mkoani Haji Shoka Khamis, alisema sasa wabakaji wameelekeza nguvu kwa watoto wadogo, jambo linalokuwa gumu wanapofika mahakamani. ‘’Wadhalilishaji sasa wamehamia kwa watoto wadogo, na kisha huwapa lugha za vitisho, kwamba

TAMWA- ZANZIBAR YAKOSA USINGIZI HADI SHERIA MPYA YA HABARI IPATIKANE

      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’BILA ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi’’. ‘’Tena pia mtu huyo ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati, na raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio ya nchini na duniani kote, ambayo ni muhimi kwa maisha yake’’. Ndivyo Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inavyoelekeza kifungu cha 18, juu ya upatikanaji na utoaji wa habari kwa raia, tena bila ya kujali mipaka ya nchi. Mwanasheria wa kujitegemea Khalfan Amour Mohamed, anasema suala la kupata habari, au kutoa ni haki ya kikatiba, ambayo inatofautiana na haki nyingine. ‘’Ukitaka kuzigawa haki hizi, basi zipo haki za kikatiba na haki nyingine zilizotengenezewa sheria yake mbali mbali, mfano haki ya elimu,’’anafafanua. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajali wananchi wake, haikuishia tu ndani ya Katiba kifungu cha

POLISI ZANZIBAR HARAKISHENI KESI YA UKATILI WA MTOTO -WAZIRI PEMBE

  Na Ibrahim Mustafa, SUZA@@@@ WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Riziki Pembe Juma ameliomba Jeshi la Polisi Zanzibar kushughulikia haraka kesi ya mtoto mwemye miaka  mitatu (3) ambae amefanyiwa kitendo cha ukatili wa kupigwa hadi kuvunjwa mkono na babaake wa kambo Lukman Shaffii (27) Mkaazi wa Magomeni Unguja, Mkoa wa Mjini Magharib. Kauli hiyo ameitowa wakati alipofika kumkagua mtoto huyo huko Maungani Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, ambapo mtoto huyo anaishi na bibi yake kwa sasa baada ya kutokea tukio hilo la ukatili wa kinyama. Amesema endapo Jeshi la Polishi litashughulikia kesi hiyo kwa haraka na uadilifu basi sheria itafuata mkondo wake na itakua funzo kwa wazazi wengine wenye tabia kama hiyo, na hatua hiyo itawafunza kujua kama mtoto ni wa Serikali. “Naliomba Jeshi la Polisi kushughulikia ipasavyo kesi za ukatili na udhalilishaji wa watoto katika jamii ili kuweza kuona vitendo hivyo vinapungua kwani watoto ndio taifa bora la badaae” Amesema Waziri Riziki. Wa

TAMWA-ZANZIBAR: ''WANAWAKE JITOKEZENI 2025 MSIJALI VITISHO''

      NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR @@@@ MKURUGENZI wa Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi   kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni,   ili kuongeza ushiriki wao bila ya kuogopa vitisho. Dk. Mzuri ameyasema hayo leo Oktoba 1, 2024 ukumbi wa mikutano wa chama hicho Tunguu Unguja, katika kikao cha kueleza namna gani   wanawake   watapata ulinzi dhidi ya ukatili wa kijinsia   mitandaoni, kupitia mradi wa wakuwawezesha waandishi wa habari vijana.   Amesema kuwa, hamu yao ni kuona wanawake wengi   wanaingia majimboni kugombea nafasi mbali mbali, lakini suala la udhalilishaji mitandaoni, linawarudisha nyuma. “Jamii inaamii mtu akitaka kugombea nafasi ya uongozi ni lazima awe msafi kwa asilimia 100, lakini mwanamke ni binadamu na   hakosi mapungufu,’’alisema. Amesema kuwa, moja kati ya kikwazo kikubwa kwa wanawake katika kugombea ni vitisho kutoka wagombea wanaume. ‘’Wanawake musiogope kujitokeza k

WANANCHI WATAKIWA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA WAPIGA KURA

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA   JAJI wa Rufaa mstaafu Mbarouk Salim Mbarouk amewataka wadau wa uchaguzi kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili wapate haki yao ya msingi ya kupiga kura ifikapo Oktoba mwaka 2025.   Akizungumza na wadau hao katika mkutano wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililofanyika katika Ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Chake Chake, Jaji huyo alisema, kila mmoja alifikia vigezo ana haki ya kushiriki zoezi hilo.   Alisema kuwa, ipo haja kwa wadau hao kila mmoja kwa nafasi yake ahakikishe anawahamasisha wananchi waliokaribu yake kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili kumuwezesha kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.   "Tume inathamini sana mchango wenu na ndio maana imewaita hapa kushirikiana na nyinyi, kujadili namna ya kuifikia jamii kwenda kuwaelimisha na kuwahamasisha ili wasikose haki yao ya kujiandikisha katika daf

TULIA ACKSON MGENI RASMI LEO HAFLA UTOAJI TUNZO

  NA HAJI NASSOR, DAR-ES-SALAAM@@@@ SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, jioni ya leo Septemba 28, 2024 kwenye hafla ya 15 ya kuwakabidhi tunzo waandishi wa habari mahiri. Tunzo hizo ambazo zimekuwa zikiandaliwa na Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’, kwa mwaka wa 15, tokea zilipoanzisha mwaka 2009, zinatarajiwa kufanyika ukumbi wa AGA KHAN DIAMOND JUBILEE eneo la Upanga jijini Dar-es Salaam. Akitoa taarifa hiyo jana, Katib Mtendaji mpya wa ‘MCT’ Ernest Sungura, alisema matayarisho yote yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa mgeni rasmi huyo. Alisema, Spika huyo ndie atakaemkabidhi mshindi wa jumla kwa mwaka 2023/2024, huku washindi wingine mbali mbali wakikabidhi zawadi na tunzo zao, na wageni mashuhuri waalikwa. Alieleza kuwa, katika hafla inayofanyika jioni hii ya leo, kutakuwa na mambo kadhaa mazuri ikiwa ni pamoja na zawadi kwa mwandishi nguli aliyefanya vyema zaidi katika maisha yake ya kihabari.   Ak