NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amesema serikali itaendelea kulijali kundi la watu wenye ulemavu, ili kuhakikisha wanapatiwa haki zao msingi, ikiwemo za uongozi na uchumi. Hayo aliyasema leo Septemba 16, 2025 kwenye hutuba yake, iliyosomwa kwa niaba yake na Katib tawala wilaya ya Micheweni Sheha Mpemba Faki, alipokuwa akifungua kongamano la wadau wa maendeleo jumuishi katika jamii, lililofanyika skuli ya Utaani Pemba. Mkuu huyo mkoa alisema, serikali imewapa haki na fursa na kuwathamini pamoja na kuwaunga mkono, watu wenye ulemavu kama walivyo watu wingine. Alieleza kuwa, watu wenye ulemavu wamepewa fursa kubwa ya kushiriki katika kupiga kura na kuchagua viongozi, wawatakao, kama msingi wa sheria mama katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilivyoekeleza kifungu cha 7 na ch 12. "Niwatoe hofu nyinyi watu wenye ulemavu, mnayo fursa kubwa ya kushiriki kikamilifu katika harakati mbali mbali zikiwemo za kisi...
NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amesema, kufunguliwa kwa Tawi la Taasisis ya Sayansi na Teknolojia ya Karume Pemba kutasogeza kwa karibu huduma za masomo ya sayansi na teknolojia kwa wananchi na kutoa fursa kwa vijana kujiendeleza kielimu wakiwa kisiwani Pemba badala ya kufuata masomo nje ya kisiwa hicho. Ameyasema hayo leo Septemba 16, 2025 wakati akifungua Tawi la chuo cha Sayansi na Teknolojia ya Karume Pemba katika viwanja vya Mnazimmoja Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba. Amesema, Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume inatoa mchango mkubwa katika kukuza taaluma ya Sayansi na Teknolojia ndani na nje ya nchi sambamba na kupata mafanikio mengi ikiwemo kuongezeka kwa wataalamu wa fani ya Sayansi na Teknolojia nchini na Barani Afrika kwa ujumla. Alieleza kuwa, uwepo wa Tawi hilo kutafungua milango ya kuitangaza Pemba kielimu katika nyanja za sayansi na Teknolojia na kuwavutia watu we...