Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

BARAZA LIJALO LA MAWAZIRI WANAHARAKATI WATAMANI 50 KWA 50 IANZIE HAPO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ NOVEMBA 1, mwaka huu Rais mteule wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alikula kiapo cha uaminifu cha kushika madaraka ya urais kwa awamu ya pili. Sherehe hizo zilifanyika uwanja wa New Amani Complex, kuanzia majira ya saa 12: 00 asubuhi, huku umati wa wananchi wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, wakijitokeza. Sherehe hizo, ni ishara ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, uliopigwa Oktoba 29, mwaka huu na wazanzibari laki 448, 832 kumpa kura za ushindi, ambayo ni sawa na asilimia 74.8. Kisha, Rais huyo wa Zanzibar, alimteua Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Mwinyi Talib Haji, hapo ni sawa na kusema, anaanza kupanga safu yake ya awamu ya pili. Pamoja na kumtea Makamu wa Pili wa rais akiwa ndie mtendaji mkuu wa serikali, bila shaka sasa zamu ya baraza la mawaziri linafuata. WANAHARAKATI WANASEMAJE Dk. Mzuri Issa Ali, ambae ni Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, anampa heko Dk...
Recent posts

HAKI YA ELIMU KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU, SERA, SHERIA, MIKATABA HAINA CHANGAMOTO LAKINI.....

    NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ SERA ya Elimu ya Zanzibar, imetaja elimu mjumuisho, ili kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki sawa kama ilivyo wingine. Sera hiyo ya mwaka 1991 ya Zanzibar, kipengele cha elimu ya watu wenye ulemavu, ibara 4.9 kimeainisha kuwa hakutokuwa na kikwazo wala sababu ya kumnyima haki yake hiyo. Imezungumzia Wizara ya Elimu na tasisi husika, itashirikiana ili kuhakikisha elimu inatolewa kwa misingi bora kwa watu wote. Hapa nayo Sheria ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (1), kimesisitiza haja kwa watu wenye ulemavu, kupewa haki zote za msingi za kibinaadamu sawa na watu wingine. ‘’Watoto wenye ulemavu na wasio na ulemavu wote watachanganywa, ili tu kupatiwa elimu bora,’’ilifafanua shehemu ya sheria hiyo. Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa wenye ulemavu nambari 19 ya mwaka 2024, inaelezea waraka wa Baraza la               ...

MADC: WANAWAKE PEMBA, WAWAONESHA NJIA WANAWAKE NAMNA YA KUONGOZA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’HESHIMA, bidii ya kazi, upole, ustahamilivu na kufanya uamuzi sahihi, ndio njia moja wapo za kuwatumikia watu,’’anasema Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki. Anasema inawezekana waliowengi, wandhani ili uwe kiongozi mzuri, lazima uchupe mipaka, kimavazi, heshima, uondoe upole, ukiuke sheria, jambo ambalo ni tofauti. Anahadithia wakati wakiwa mtendaji wa Tume ya Uchaguzi, miaka 15 iliyopita, alichunga sana nidhamu na heshima yake, huku akihakikisha halazi kazi. Alizingatia mno kivazi cha heshima, kujenga mapenzi ya kazi kwa kila mmoja, na kuhakikisha kitengo chake hakifeli kwa jukumu, walilopewa. ''Kuna wakai tunasafirisha vifaa tena siku ya mvua, ilipofika majira ya saa 5:50 usiku, wapo walionitaka nirudi nyumbani kumpunzika na wao wataendelea na kazi, niligoma,''anakumbushia. Aliwaambia kama ni wakati wa kazi wanafanya kwa pamoja na wakati wa kumpunzika, wanapumzika kwa pamoja, maana kazi ndio kazi. ‘’Siku hiyo kila mmoj...

MCHAKATO WA KISIASA KWA WATU WENYE ULEMAVU BADO KITENDAWILI

   NA SAMIRA ABDALLA, ZANZIBAR UCHAGUZI mkuu wa mwaka 2025 unafanyika kesho, na suala la ushirikishwaji kamili wa watu wenye ulemavu, linazidi kuwa muhimu.   Zanzibar, kama sehemu nyingine ya dunia, imejitolea kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu, zinalindwa na kutekelezwa, ikiwemo haki yao ya kupiga kura na kugombea uongozi. Makala haya yatafanya uchambuzi wa kina kuhusu ushirikishwaji wao, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025. Licha ya kuwa wengi wetu walikuwa wakifikiria kwamba watu wenye ulemavu, hawana haki na wala hawafai kushiriki katika uchaguzi, jambo ambalo sio sahihi. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kama sheria mama, inatoa msingi wa ulinzi wa haki za binadamu kwa raia wote kuanzia kifungu ch 11 hadi 25A. Ingawa haitaji moja kwa moja watu wenye ulemavu, inasisitiza usawa mbele ya sheria na kutobaguliwa kwa misingi yoyote. Hata hivyo, sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, inatoa mwelekeo mpana na wa kina zaidi kuhusu haki ...