Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

MBUNGE CUF PEMBA AJIUNGA CCM, AAZIMIA KUCHUKUA FOMU YA UBUNGE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Pandani kwa tiketi ya Chama cha wananchi ‘CUF’ Maryam Omar Said, amsema kuaniza Juni 29, mwaka huu ametangaaza, kujiengua kwenye chama hicho na kujiunga na CCM, akidai amevutiwa na utekelezaji wa Ilani ya chama hicho, kwa miaka mitano iliyopita. Alisema, ameamua kurudi nyumbani, baada ya kuona yale yote aliyota ndani ya jimbo lake la Pandani, yamekelezwa ikiwemo miradi ya elimu, afya na maji safi na salama kwa miaka mitano iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba alisema, hana sababu ya kubakia ndani ya CUF, na ameamua kuhamia CCM, ili kuungana na Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Alieleza kuwa, akiwa ndani ya CUF, hatakuwa na nafasi nzuri ya kushika bango la CCM na ndio maana, ameamua kwa hiari yake na bila ya kulazimishwa, kurudi ndani ya chama hicho. Mbunge huyo mstaafu wa CUF, alisema awali alikuwa mwana CCM, ingawa alitok...
Recent posts

WANAWAKE PEMBA WAKIWEMO WAANDISHI WA HABARI NAO MGUU SAWA UCHUKUAJI FOMU

  NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA ZOEZI la uchukuwaji wa fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum linaendelea kupamba moto, kwa wanawake,wakiwemo wanahabari kupishana ofisi za CCM wilaya za kisiwani Pemba . Zanzibar leo kisiwani Pemba, ambalo limepiga kambi katika ofisi hizo, limeshuhudia wandishi wabahari wanawake, wajasirimali, watendaji wa serikali na waachama wingine, wakitekeleza haki yao ya kidemokrasia. Akizungumza na gazeti hili, mmoja kati ya watia nia hao kwa nafasi ya ubunge Jimbo la Chake chake, Ashura Abdalla Simai 'mabodo', alisema moja ya sababu iliyomsukuma ni kutekeleza haki yake ya kikatiba ya kisiasa. Alieleza kuwa, pindi vikao vya chama vikiridhia jina lake na kurudi, atakwenda bungeni kuwatetea wanawake wenzake na wingine, kwani walio wingi hawajafanya hivyo. “Wanawake wamekuwa wakikosa matetezi kwa kina, wa mambo yanayotuhusu, hivyo nimechukuwa fomu hii kujaribu bahati yangu kwa mara ya tano,”alisema. Afisa hab...

WAISLAMU: ADHIMISHENI MWAKA MPYA WA KIISLAM KAMA ILIVYO ASILI

NA BAKAR KHAMIS, PEMBA@@@@   Waumini wa dini ya kiislamu,wametakiwa kuazimisha mwaka mpya kwa kulinganisha na historia ya uislamu. Hayo yameelezwa na imamu mkuu wa msikiti wa ng'ambwa wilaya ya chake chake mkoa wa kusini pemba sheikh Abdallah said mara baada ya khutba ya ijumaa Amesema waumini wa kweli hawana budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita iwapo kuna mema waliyoyafanya waendeleze na mabaya wajikataze  "Kwa kweli hatuna budi kujitathmini katika kipindi cha mwaka uliopita wa 1446 kama kuna mema tuliyokua tukiyafanya tujitahidi kuyaendeleza na kuzidisha katika mwaka huu wa 1447 hijria kama shukran zetu kwa mola wetu" "Na pia maovu yote ya siri na ya dhahiri tujitahidi kuyaepuka ili tupate neema na salama". Kwa upande wake khatibu wa zamu Zahor Yahya Muhdhari, amesema maadhimisho mema ya mwaka mpya ni kusimamia malezi ya watoto na usimamizi wa familia. "Hakika watoto na wake zetu ni mtihani mkubwa kama ambavyo Allah s.w amesema kwa hivyo tu...

UWT YAWAALIKA WANAWAKE KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA

  BAKARI KHAMIS NA MOZA SHAABAN, PEMBA MAKAMu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainab Khamis Shomari, amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi mbali mbali za uongozi majimboni. Aliyasema hayo ofisi ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya Mkoa iliyopo Chake chake kisiwani Pemba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea zoezi la uchukuaji wa fomu za lililoanza janaJuni 28. Alisema ni vyema wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo, kutokana na kuwepo kwa mazingira rafiki yanayowawezesha, kushiriki zoezi hilo bila kikwazo chochote. Alisema ushiriki wa wanawake katika kugombea nafasi za uongozi ni miongoni mwa matakwa ya ilani ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’, ambacho kipo madarakani, ambayo imeeleza kipaumbelechake cha uwepo wa wawakilishi wanawake kwa asilimia 50 katika vyombo vya kutunga sheria. Alieleza kwamba Umoja wa Wanawake Tanzania, umekua ukifanya jitihada mbali mbali katika kulitimiza takwa hilo,...

AHMED ABUBAKR AWA WA KWANZA KUCHUKUA FOMU CCM

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ZOEZI la uchukuaji wa fomu za kuomba ya kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum kupitia chama cha Mapinduzi ‘CCM ‘wilaya ya Chake chake, linaendelea vyema.   Zanzibar leo ambalo lilifika ofisi ya CCM wilayani humo majira ya saa 2:00 asubuhi, liliwashuhudia wanaccm wakijitokeza mfululizo kuchukua fomu hizo, kwa nafasi kadhaa zilizotangaazwa.   Mtinia wa kwanza kwa nafasi ya uwakilishi kutoka Jimbo la Chonga Ahmed Abubakar Mohamed, alifika ofisini hapo majira ya saa 2:40, na kufika chumba cha kwanza, kwa ajili ya usaili, kabla ya kukutana na Katibu wa CCM na kukabidhiwa fomu.   Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi ya CCM mjini Chake chake, mtia nia huyo alisema, ameamua kuchukua fomu hiyo, ili kuunga nguvu za Rais wa sasa wa Zanzibar, ya kuwaletea maendeleo wananchi.   Alisema, amekuwa akivutiwa mno na kasi ya Dk. Mwinyi jinsi anavyowafanyia wananchi wake maendeleo, na ndio maan...

SWAHILI COAST PROJECT: EMPOWERING WOMEN AND YOUTH AS CHAMPIONS OF PEACE IN PEMBA

  BY KHELEF NASSOR@ZANZIBAR Peace is more than the absence of conflict; it is a state of harmony where communities live with respect, understanding, and cooperation. True peace creates an environment where individuals can thrive, families grow strong, and societies progress. However, peace is fragile and must be actively nurtured by all members of society. Women and youth play a critical role in building and sustaining peace. They are not only the majority of many communities but also agents of change, innovation, and resilience. When empowered with knowledge and leadership skills, they become vital contributors to conflict prevention, social cohesion, and community development. Their involvement ensures that peace is inclusive, representative, and sustainable. Recognizing this,   Norwegian Church Aid - NCA recently organized a comprehensive three-day training program focused on leadership and peacebuilding for women and youth in Pemba Island. The training was part ...

MASHEHA CHUMBAGENI, WAMBAA WAAHIDI KUIPIGA TAFU JUMUIYA TAHAFIDHIL-QUR-AN WAMBAA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   MASHEHA wa shehia za Wambaa na Chumbageni, wilaya ya Mkoani Pemba, wameiahahidi jumuiya ya tahafidhil quran, kwamba, watashirikiana nayo, ili kuhakikisha mashindani ya sita ya mwakani yanafanyika kwa ufanisi.   Wakizungumza kwenye kikao maalum cha kamati kuu cha jumuiya hiyo, kilichofanyika Chumbageni, walisema wako tayari kuona mashindani ya mwakani yanafanikiwa.   Walisema, suala la kuwakusanya watoto katika jambo jema kama hilo, hawaa budi kuliunga mkono, kwani ndio eneo la kutafuta kheir kutoka kwa Muumba,   Shehia wa Chumbageni Mgeni Othman Shaame, alisema atazishauri taasis kadhaa na waumini wingine, ili kutoa michango yao ya hali na mali.   Alisema, kutokana na mashindani ya tano kufanikiwa, vyema binafsi ameingia tena hamu, kuona ashirikiane na Jumuiya hiyo, kwa ajili ya mwakani.   ‘’Kwa hakika, mashindani ya tano yalifanikiwa vyema, na kwa kwa mara ya kwanza, mgeni rasmi alikuwa Mkuu w...

MWENGE WAUKUBALI USHIRIKA WA UPANDAJI MIGOMBA KUKUU KANGANI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KIONGOZI wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi amesema, ameridhishwa kwa asilimia 100, na utekelezwaji wa mradi wa upandaji wa migomba uliotekelezwa na kikundi cha ‘tusitupane Cooparative’ kilichopo shehia ya Kukuu wilaya ya Mkoani Pemba. Alisema, mradi huo ni miongoni mwa jitihada za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, za kuunga mkono wananchi wake, katika kuhakikisha wanatumia fursa za kiuchumi zinazowazunguka katika maeneo yao. Aliyasema hayo jana, wakati alipotembelea shamba la migomba la kikundi hicho, shehiani humo, ikiwa ni shamra shamra za mwenge huo, kwa mwaka huu. Alieleza kua, mradi huo ni utekelezaji wa ahadi alizoziweka Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi baada ya kuingia madarakani, za kuwawezesha wananchi kuzitumia fursa za kiuchumi zilizopo nchini. Alifafanua kua, kilimo hicho kinaonyesha dhahiri kwamba, vijana wa kikundi hicho wamefanya jitihada nzuri, katika kutimiza azma na maono ya Dk. Mwinyi. "Vijana w...

MWENGE WABISHA HODI CHAKE CHAKE, UKITOKEA MKOANI

    NA MWANDISHI WETU, PEMBA MKUU wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakari, ameuhakikishia, uongozi wa mbio za mwenge kitaifa wa mwaka 2025, kwamba watayafanyia kazi maagizo, maelekezo na ushauri waliutoa, hasa suala la kutunza amani na utulivu, kuelekea uchaguzi mkuu .   Mkuu huyo wa wilaya aliysema hayo jana, eneo la skuli ya Ngwachani wilayani humo, kwenye hafla ya kumkabidhi mwenge huo, mwenzake wa wilaya ya Chake chake Mgeni Khatib Yahya.   Alisema ujumbe wa mwenge kiujumla, umekuja kuwazindua wananchi wa wilaya yake, juu ya umuhimu wa kutunza amani, kwa maslahi mapana ya taifa na watu wake.   Alieleza kuwa, wakati mwenge huo unakimbizwa wilayani mwake na kukutana na wananchi, ulisisitiza utunzaji wa amani, na hasa kuelekea mwezi Oktoba mwaka huu, kwenye uchaguzi mkuu wa vyama vingi.   Dk. Hamad alifahamisha kuwa, jingine ambalo mwenge huo wa uhuru chini ya kiongozi wake Ismail Ali Ussi, ulisisitiza, ni kupiga vita dawa za kulevya ...

WANANCHI PANDANI, MKAGUZI WAO WAJIIMARISHA KUTOKOMEZA UHALIFU

     NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Pandani wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, wamesema wataendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi, ili kudumisha amani na utulivu kwa kupambana na matendo maovu katika shehia yao.   Walieleza hayo katika kikao cha pamoja na mkaguzi wa shehia hiyo cha kujadili na kupanga mikakati ya kuzuiya uhalifu katika shehia hiyo, kilichofanyika shehiani.   Saada Hamid Ali mkazi wa shehia hiyo na Said Juma walieleza kwa niaba ya wanakijiji wenzake walipongeza jitihada za Mkaguzi huyo kwa kuona wanafikia lengo la kuondosha uhalifu.   Walieleza kuwa, kijiji kinapokuwa salama, huwapa nafasi vijana na wananchi wingine, kufanya shughuli zao mbali mbali za maendeleo kwa ufanisi   Akifafanua kikao hicho, Mkaguzi wa shehia hiyo kutoka Jeshi la Polisi mkoa wa kaskani Pemba Khalfan Ali Ussi, alieleza kuwa wanazo mbinu kadhaa za kukabiliana na uhalifu.   Hata hivyo, aliwasisitiza wananch...