NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ NOVEMBA 1, mwaka huu Rais mteule wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, alikula kiapo cha uaminifu cha kushika madaraka ya urais kwa awamu ya pili. Sherehe hizo zilifanyika uwanja wa New Amani Complex, kuanzia majira ya saa 12: 00 asubuhi, huku umati wa wananchi wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, wakijitokeza. Sherehe hizo, ni ishara ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu, uliopigwa Oktoba 29, mwaka huu na wazanzibari laki 448, 832 kumpa kura za ushindi, ambayo ni sawa na asilimia 74.8. Kisha, Rais huyo wa Zanzibar, alimteua Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Mwinyi Talib Haji, hapo ni sawa na kusema, anaanza kupanga safu yake ya awamu ya pili. Pamoja na kumtea Makamu wa Pili wa rais akiwa ndie mtendaji mkuu wa serikali, bila shaka sasa zamu ya baraza la mawaziri linafuata. WANAHARAKATI WANASEMAJE Dk. Mzuri Issa Ali, ambae ni Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, anampa heko Dk...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ SERA ya Elimu ya Zanzibar, imetaja elimu mjumuisho, ili kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki sawa kama ilivyo wingine. Sera hiyo ya mwaka 1991 ya Zanzibar, kipengele cha elimu ya watu wenye ulemavu, ibara 4.9 kimeainisha kuwa hakutokuwa na kikwazo wala sababu ya kumnyima haki yake hiyo. Imezungumzia Wizara ya Elimu na tasisi husika, itashirikiana ili kuhakikisha elimu inatolewa kwa misingi bora kwa watu wote. Hapa nayo Sheria ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (1), kimesisitiza haja kwa watu wenye ulemavu, kupewa haki zote za msingi za kibinaadamu sawa na watu wingine. ‘’Watoto wenye ulemavu na wasio na ulemavu wote watachanganywa, ili tu kupatiwa elimu bora,’’ilifafanua shehemu ya sheria hiyo. Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa wenye ulemavu nambari 19 ya mwaka 2024, inaelezea waraka wa Baraza la ...