Skip to main content

Posts

TAMWA -ZNZ: 'SHERIA MPYA YA HABARI, MWANGA WA KUWATOA WOGA WAANDISHI WA HABARI'

NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@ Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania Zanzibar Dk Mzuri Issa amesema kuwepo kwa Sheria mpya ya habari inayokwenda sambamba na maendeleo ya Sayansi na teknolojia itatowa fursa kwa waandishi wahabari kufanya kazi zao kwa ufanisi. Akitowa taarifa kwa vyombo vya habari amesema pamoja na kuwepo maoni mengi yaliyotolewa na waandishi wahabari pamoja na wadau na watetezi wa haki za binadamu kuhusu mabadiliko ya sheria ya zamani iliodumu kwa takribani muongo mmoja bado kunahitajika kuwepo kwa sheria rafiki inayokwenda na wakati wa sasa. Dk Mzuri amewapongeza wadau mbali mbali walioshirikiana na vyombo vya habari ikiwemo Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya msingi ya kupata habari kama inavyosema Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 18, pamoja na Mikataba ya Kikanda inayosimamia uhuru wa vyombo vya habari nchini. “Wakati tunaingia mwaka mpya 2024 waandishi na vyombo vya habari wana matumaini makubwa ya kuzita...

HAROUN: 'KITUO CHA UTATUZI MIGOGORO ZANZIBAR KIVUTIZI KWA WAWEKEZAJI'

  NA FAKI MJAKA, AMM  -ZANZIBAR@@@@   Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Mh. Haroun Ali Suleiman amesema kuanzishwa kwa Sheria ya Usuluhishi na Kituo cha Utatuzi wa Migogoro Zanzibar kutaongeza imani ya wawekezaji kuja nchini kuwekeza miradi yao ya kimaendeleo.   Amesema kituo hicho kitakapoanzishwa kitawahudumia wenyeji na wageni na hivyo kupunguza kasi ya watu kuepelekana mahkamani hasa pale migogoro ya kibiashara na uwekezaji inapotokea.   Waziri Haroun aliyasema hayo huko katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege alipofungua Mkutano wa Wadau uliojadili Rasimu za Miswada ya Sheria ya Usuluhishi na Sheria ya kuanzisha Kituo cha Usuluhishi wa Migogoro Zanzibar uliohudhuriwa na wadau kutoka sekta mbali mbali nchini.   Alisema hali ya Zanzibar kiuchumi inaimarika sana kutokana na juhudi zinazochukuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi za kuwavutia Wawekezaj...

KESI TUHMA YA KUUA KWA MAKSUDI PEMBA: 'PP HATUJAMALIZA MAELEZO YA MASHIDI KWANZA'

  NA MARYAM NASSOR, PEMBA @@@@  WATUHUMIWA wa kesi ya kuua kwa  makusudi, inayowakabili vijana wanne akiwemo Yassir  Mussa Omar ‘Makababu’ na wenzake , wote wakazi wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake,  wameendelea kusota rumande, baada ya upande wa mashtaka, kushindwa kukamilisha maelezo ya kesi na mashahidi kwa wakati. Mara baada ya watuhumiwa hao kuwasili mahakamani hapo wakitokea rumande, Mwendesha Mashtaka kutoka   Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Pemba, Mohamed Abdallah Juma, alidai kutokamilisha kwa baadhi ya mambo muhimu.   Alimueleza, Jaji wa Mahakama kuu Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa, kesi hiyo ipo mahkamani hapo kwa ajili ya kutajwa, ingawa bado maelezo ya shauri hilo hayajakamilika. “Mheshimiwa Jaji leo (jana), kesi hii ipo kwa ajili ya kutajwa,   lakini bado hatujakamilisha maelezo ya   kesi na mashahidi , hivyo tunaomba utupangie tarehe nyengine kwa ajili ya kutajwa tena,”alidai. Baada ya maelezo hayo, Jaji wa mahak...

'Wanaume ungeni mkono uzazi wa mpango'

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA LICHA ya elimu ya uzazi wa mpango inayotolewa kwenye vituo vya afya lakini bado kuna baadhi ya akinababa huwazuia wake zao, jambo ambalo linaweza kusababisha athari kwa mama mwenye matatizo katika mfumo wake wa uzazi. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wananchi wa shehia ya Shungi Wilaya ya Chake Chake walisema, madaktari wanajitahidi kutoa elimu kuhusiana na uzazi wa mpango, ingawa kuna baadhi ya wanawake wanaendelea kupata athari kutokana na kutofuata huduma za uzazi wa mpango. Walisema kuwa, uzazi wa mpango ni muhimu kwa wanawake kwani wanapata kupumzika, kuimarika kiafya na kumfanya mtoto akue vizuri, hivyo ipo haja kwa akina baba kuangalia hali ya afya kwanza, ndipo wakatae uzazi wa mpango. ‘’Elimu ipo kwa sababu tunapokwenda vituo vya afya madaktari wanajitahidi kutuelimisha, lakini baadhi ya wanaume wanahisi kama tunataka kufungwa uzazi, jambo ambalo sio sahihi,’’ walisema wananchi hao. Mwananchi Fatma Said Khalfan alisema kuwa, kuna b...

KESI TUHMA ZA KUUA KWA MAKSUDI PEMBA KUNGURUMA ASUBUHI HII MAHKAMA KUU

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KESI ya tuhma ya mauwaji kwa maksudi, inayowakabili vijana wanne, akiwemo Ali Mussa Omar ‘Mkapa’ na wenzake, wote wakaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba, inatarajiwa kunguruma tena leo Mahakama kuu Zanzibar kisiwani Pemba. Watuhumiwa wingine wanaotarajiwa kuwasilia mahkamani hapo wakitokea rumande ni Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 na Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, ambao wanatuhumiwa kumuua kwa maksudi kijana Said Seif Kombo. Awali kesi hiyo kwa mara ya mwisho ilinguruma mahkamani hapo, ingawa kwa siku hiyo ya Novemba 30, mwaka jana, haikuendelea kusikilizwa wala kutolewa ushahidi, baada ya Jaji wa mahkama kuu Pemba, kutokuwepo mahkamani hapo. Ambapo kwa siku hiyo kesi hiyo, ilisikilizwa na Hakim wa mahkama ya mkoa Chake chake, ambae kisheria hana mamlaka ya kusikiliza kesi za mahakama kuu, vyenginevyo kuwe na utaratibu maalum. Hakimu wa Mahkama ya Mkoa Chake chake aliyepokea watuhumiwa Ziredi A...

Ushirika 'Hufedheheki' wamsifika kiongozi wao anavyopigani kuimarisha kikundi

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA   WAJASIRIAMALI wa kikundi cha mboga na matunda cha ‘Hufedheheki’ kilichopo Kwale Mpona Finya wamesema, wanafurahia uongozi wa Katibu wao Subira Mkubwa Mohamed namna anavyopigania katika kuhakikisha kikundi hicho kinapata maendeleo.   Walisema kuwa, amekuwa akiwashirikisha hatua kwa hatua katika masuala yote ya kikundi, jambo ambalo linawapa faraja kwani wanakuwa na uhuru wa kutoa maoni yao na baadae kuyafanyi kazi kadiri anavyoweza.   Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wanakikundi hao walisema, Katibu wao huyo anapambania kwa hali na mali kuhakikisha kikundi kinazalisha zaidi na kujipatia kipato kitakachowakwamua kimaisha.   Mwanakikundi Khamis Ali Khamis alisema, mama huyo ni kiongozi mchapa kazi na mchakarikaji kiasi ambacho na wao hupata nguvu ya kuzalisha zaidi bidhaa zao kwa lengo la kujipatia mafanikio.   Alisema, wamepata manufaa mengi kupitia kiongozi huyo mwanamke kutokana na kuwa anawah...

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE CHAPATA VIONGOZI WAPYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa Chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa Chake chake kichama, wamekamilisha uchaguzi wao mkuu, baada ya kuwapata viongozi wapya, watakaokiongoza chama hicho, kwa miaka mitano ijayo.   Katika uchaguzi mkuu huo, umemrejesha tena kwenye nafasi ya Katibu, aliyewahi kuwa Mwakilishi wa majimbo ya Vitongoji na Wawi wakati huo, Saleh Nassor Juma, baada ya nafasi yake kukosa mpinzani. Ambapo katika uchaguzi huo, uliofanyika Gombani Chake chake Pemba, alijizolea kura 65, kati ya kura 73 zilizopigwa, huku kura mbili zikiharibika na kura sita zikimkataa. Aidha Msimamizi wa uchaguzi huo Rashid Ali Abdalla, alimtangaaza Yussuf Salim Khamis, kuwa ndie Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, baada ya kupata kura 39 na kumshinda mpinzake Mohamed Juma Khatib aliyepata kura 34. Katika uchaguzi huo, ulimchagua Khadija Ali Abeid kuwa Mshifa fedha wa Mkoa wa Chake chake kwa kura 36, baada ya kumuangusha mgombea mwenzake, Khadija Anuwar...

WANANCHI PEMBA WASEMA JAMBO FEDHA ZA UVIKO19 KWENYE AFYA

     NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wamesema fedha za ahuweni ya UVIKO 19, zilizoelekezwa kwenye miradi ya wizara ya Afya kisiwani humo, zimetumika vyema, na sasa wanaendelea kunufaika nazo. Walisema, serikali iliweka wazi mgao wa fedha hizo na matumizi yake, ambapo kwa upande wa Wizara ya Afya na hasa kisiwani Pemba, zilizitumia kwa ujenzi wa hospitali za kisasa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya kumalizika na kuanza kazi kwa hospitali hizo, walisema majengo hayo yamekuwa ya kiwango cha juu, ujenzi wake. Walieleza kuwa, sasa wameshaachana na majengo ya zamani, ambayo hayakuwa na nafasi, kwa ajili yao na madaktari wanapotoa huduma kwa wagonjwa. Maryam Himid Mjaka wa Micheweni, alisema sasa wamekuwa na nafasi kubwa ya kukaa kumsubiri daktari, ikilinganishwa na hospitali yao ya zamani. Kazija Haji Mshamata wa Konde, alisema sasa wamekuwa na hamu ya kwenda kutafuta huduma kwenye hospitali ya Micheweni ama Kinyasini, kutokana na...

MJUE MWANAMKE ANAYEZIPENDEZESHA FUKWE KWA USAFI

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ Maisha ya binaadamu huwa   salama na ya afya njema kama mazingira yanayomzunguka yapo safi na salama na yanapokuwa yameharibika huwa hatarishi kwake, wanyama, wadudu na mimea. Hali hii ndio inayopelekea kusikia kila kukicha   wizara ya afya   kwa kupitia wataalamu wake mbali mbali inasisitiz umuhimu wa kuweka mazingira safi ndani na nje ya nyumba zetu, mitaani, vijijini na katika maeneo ya biashara kama masoko au ya kuuza na kununua chakula. Mwanamke amekuwa akionesha uongozi mzuri kwenye jamii zetu kwa kuanzia kwenye familia na kutokana na jamii yetu, katika miaka ya karibuni kutotilia maanani sana usafi wa mazingira kumepelekea kujitokeza watu kuongoza jamii kufanya marekebisho yanayohitajika. Miongoni mwa wana jamii waliojitokeza   kuwa mstari wa mbele kuongoza juhudi za kutunza mazingira ni mwana mama anyeiingoza Kikundi cha Ulinzi wa Mazingira, Siwema   Mshenga   Issa, kutoka Sheiha ya Bubwini Makoba. Yeye ...

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE: 'CHAGUWENI VIONGOZI WATAKAOKIVUUSHA CHAMA 2025'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa mkutano mkuu maalum wa chama cha ACT-Wazalendo, mkoa wa Chake chake kichama, wametakiwa kuwachagua viongozi wenye uwezo na nia thabiti, ya kukivuusha chama katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025. Ushauri huo,Januari 14, 2024 umetolewa na Mjumbe wa Kamati kuu taifa ya chama hicho, Isihaka Mchinjita, wakati akiufungua mkutano huo, uliofanyika ukumbi cha Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba. Alisema, wajumbe wa mkutano huo mkuu maalum, ndio wenyejukumu la kuwapata viongozi watakaoshirikiana na wale ngazi ya taifa, katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao. Alieleza kuwa, ikiwa watafanya makosa kwa kumchagua kiongozi kwa sifa za juu juu pekee, wanaweza kukipa wakati mgumu chama, wakati kinapoingia kwenye chaguzi mbali mbali. Alifahamisha, ili chama kiwe na nguvu, mwelekeo, dira inayotekelezeka, lazima kuwepo kwa viongozi imara kuanzia tawi, jimbo, mkoa na kisha taifa. ‘’Wajumbe wa mkutano huu mkuu maalum wa ACT-Wazalendo hapa mkoa C...